Hayati Magufuli alivyoalika wazee wa kimila Ikulu kupiga dua(kutambika) ili mvua zinyeshe

Hayati Magufuli alivyoalika wazee wa kimila Ikulu kupiga dua(kutambika) ili mvua zinyeshe

Hizi nyuzi za Magufuli kuwa nyingi kulikoni?
Hadi 2025, tunabadili gia na tutaendelea nae hadi 2030,
hakwepeki, yaani kachukua nafasi ya nyerere ati, JPM the best president in tz ever, kurukaruka kwa maharage ndio mwanzo wa kuiva, acha warukeruke tu, kosa pekee wanafanya ni kumpuuza na kumponda, wange m'bless whuku wakipenyeza agenda zao tungemsahau mapema, lkn kwa miondoko yao hiyo watafeli sana,
Kitu pekee kitawasaidia ni kwa kuwa turn out 2025 itakuwa ndogo sana na watu hawatajali nani kaingia nani kakosa, labda kny ubunge na udiwani kwa maeneo ambayo yanawabunge na madiwani tegemeo.
 
Kwenye ile sherehe mzee mmoja akaomba kilo tatu za nyama. Mwenye sherehe akasem huyo babu mpeni kilo nne za nyama. Wahinjaji wakamyima eti ni mchoyo. Sherehe ikaanza saa 6mchana nyie tulinyeshewa nvua non stop.

Mwenye sherehe akauliza kwani yule mzee hakupewa nyama? Wakajibu mchoyo yule aje ale na wengine, aiseee mwenye sherehe alichukuwa kilo tano fasta akakimbia kwa yule babu saa 10 jion mvua ikakata na miziki ikaanza.
Aiiiiiiii walokuja na nguo zao mpya ungeziona nyie msicheze na hawa wazee.
Mwenye sherehe alikuwa anamjua nn
 
Kwenye ile sherehe mzee mmoja akaomba kilo tatu za nyama. Mwenye sherehe akasem huyo babu mpeni kilo nne za nyama. Wahinjaji wakamyima eti ni mchoyo. Sherehe ikaanza saa 6mchana nyie tulinyeshewa nvua non stop.

Mwenye sherehe akauliza kwani yule mzee hakupewa nyama? Wakajibu mchoyo yule aje ale na wengine, aiseee mwenye sherehe alichukuwa kilo tano fasta akakimbia kwa yule babu saa 10 jion mvua ikakata na miziki ikaanza.
Aiiiiiiii walokuja na nguo zao mpya ungeziona nyie msicheze na hawa wazee.
Sherehe gan[emoji23][emoji1787][emoji28][emoji1787][emoji23][emoji23][emoji1787][emoji1787][emoji23][emoji23]
 
Hivi nyie mnao jiongelesha hapa mnajua siku ya send off au ndoa ni mangapi yanafanyika nvua isinyeshe?

Tatizo lenu mkishakulaga mkavimvea hamjui imekuwaje sherehe ikaisha vizuri.nyie ni kula tu na kulewa hamjui kazi kubwa inayofanyika usiku wa kuamkia sherehe.

Iko hivi sherehe ni kesho leo atatafutwa mtaalamu wa nvua akiamka asubuhi atafanya yake ila haruhusiwi kugusa maji siku hiyo hakuna kupiga hata mswaki.

Anavaki ndani siku nzima mpaka bibi harusi na wageni watakapo ondoka chakula anakula kwa kijiko hanywi hata maji.

Kama nadanganya wewe siku ya sherehe kwenu kawaulize shangazi zako na bibi zako kuna vibibi vinakaaga huko chumbani siku nzima havitoki hivyo vitaalamu.
Hiyo niliona huko Bukoba kibibi kinakaa nyuma ya mlango hakiendi hata chooni siku nzima
 
Nikiri tu kuwa mimi nimezaliwa kwenye jamii zenye zinazodumisha mila zetu za asili(matambiko nisehemu ya maisha yetu).
Bibi yangu na babu yangu wapo vizuri.
Waliwahi kuniambia kuwa hakuna kazi nyepesi kama wa kuzuia au kuleta mvua.

Wazee wetu hawa wakiwa field huwa wanajaribiwa kwa hicho kitu,ukifeli unarudia somo.kuleta mvua au kuzuia mvua ni somo rahisi katika mitaala ya wazee wa kimila

Tangu uzaliwe ni lini ukaona mkutano wa vyama vya siasa ukavunjika kisa mvua?kwa taharifa yako mikutano hii huwa kuna kamati ya ufundi kuzuia mvua.

Hayati Magufuli baada ya kuingia madarakani aliwaita hawa wazee wa kimila (tamka wachawi)
toka kila mkoa Ikulu na kuwaambia kuwa anawapenda watanzania na asingependa kuona wanakufa njaa.hivyo aliwaomba wamsaidie kupiga dua(tamka kuroga) ili nchi iwe na mvua za kutosha.

Baada ya dua kila mzee alikutana na baasha nene ya kaki ikiwa na nauli na posho ya maana,

Wazee hawa hawakumuangusha ,mvua tuliziona,sasa mama Samia unafeli wapi?Babu yangu ni mmoja kati ya hawa wazee,mwaka wa pili sasa sijasikia simu yake kuwa anakwenda Dar au Dodoma Ikulu kupiga dua

Tangu mama aingie mjengoni mvua hazieleweki,sio mbaya kuiga mazuri ya JPM ,njaa zitatuua,mchele kilo 3500!!!
Zile zilikuwa ni siasa za kukutanisha watu tu. Hivi kweli unamini mvua zinaweza kuleta na wazee wa dini za jadi kweli?
 
Zile zilikuwa ni siasa za kukutanisha watu tu. Hivi kweli unamini mvua zinaweza kuleta na wazee wa dini za jadi kweli?
Inawezekana kiranga japo huamini uwepo wa Mungu wala shetani ila kuna watu wana nguvu za asili
 
Yule Mzee alikuwa Mchawi Mungu katupishilia mbali.
 
Back
Top Bottom