Jamani, ni hulka ya wanadamu kutotangaza mema ya watu lakini wepesi sana kutangaza mabaya ya watu.
Hivi karibuni kuna madaktari kadhaa walitangazwa na wanafunzi wao kwa ubaya sana! Sijui kama tuhuma walizotangazwa kwazo zilikuwa na ukweli au la!
Huu uzi naomba tufanye kinyume, tuwaseme wakufunzi wetu wa vyuo vikuu kwa majina yao kwa namna walivyo 'committed', 'fair' na mahiri katika kutoa mashule na hata walivyo fair katika kutoa na ku'mark' mitihani yenu!
Kama hukujariwa kufika chuo kikuu ww muweke mwalimu aliyekufurahisha kwa umahiri wake wa kufundisha ktk kiwango cha juu kabisa cha cha elimu ulichofikia!
Tafadhari bandugu, muelezee kidogo kivipi alikufurahisha ili kama atajua basi atiwe moyo na hayo afanyayo! Kumbuka tukitaka kuwananga huwa walimu wetu kwa ubaya huwa hatuishii kutaja majina tu bali tunaelezea kwa kirefu hata kujaza gazeti. Leo eleza hata kwa mstari mmoja tu kumjurisha alivyougusa moyo wako!
Niishie hapo