Hebu malizeni huu Ubishani wetu wa 'Kijiwe Nongwa' chetu je, kati ya hawa Wawili nani anamtuma na kumvimbia Mwenzake Kicheo?

MINOCYCLINE

JF-Expert Member
Joined
Apr 2, 2015
Posts
8,018
Reaction score
16,802
Je, Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari ya nchini Tanzania Dkt. Hassan Abbas na Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais Ikulu na Msemaji wa Serikali Gerson Msigwa nani ni 'Boss' wa Mwenzake na nani pia anatakiwa kuwa Mnyonge kwa Mwenzake?

Sasa Generalist nasubiri Mirejesho yenu.
 
Reactions: SMU
Ukishajua mnyonge na asiekuwa mnyonge kati ya hao wawili ndo itakusaidiaje katika maisha yako?
 
Ukishajua mnyonge na asiekuwa mnyonge kati ya hao wawili ndo itakusaidiaje katika maisha yako?
 
Ndiyo mlikojiajiri huko kwenye kijiwe nongwa mkuu? Tukikujibu tutafaidikaje pia?
 
Wakurugenzi wa Idara za serikali wapo chini ya Katibu Mkuu wa Wizara. Gerson akiwa Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Ikulu bosi wake ni Katibu Mkuu Ikulu, Dr. Kusiluka na akiwa Mkurugenzi wa Habari Maelezo bosi wake ni Katibu Mkuu wizara ya habari, dokta Abass. Natumai umepata jibu la maswali yako

NB: Hapa lazima Gerson ataondolewa cheo kimoja,maana hawezi kuripoti kwa ma-KM wawili
 
Gerson alishaondolewa na Leo nadhani imefanyika teuzi mpya. But yeye kama Mkurugenzi wa Habari na Maelezo ambapo anakuwa kama msemaji mkuu wa serikali kicheo yupo chini ya Katibu Mkuu wa wizara ya Habari. Wanapishana cheo kimoja, yeye anakuwa katika list ya wakurugenzi.
 
Hajaondolewa Ikulu, bado anafanya kazi kama Mkurugenzi wa Mawasiliano Ikulu. Taarifa ya Ikulu kwa umma ya TEUZI za jana Gerson ndiye ameisaini pamoja na nyingine zote zilizofanywa na Rais SSH. Amesaini kama Mkurugenzi wa Mawasiliano Ikulu na sio kama Mkurugenzi wa Habari Maelezo.
 
Mama anapata kigugumizi kumteua Maria Sarungi Ikulu kama msemaji wake!! Yeye mwenyewe kasema MCHAWI MPE AKULELE MWANAO sasa anapata wapi kigugumizi na mwana anae!!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…