Hebu tuangalie hoja hizi zilizotumika kupinga Uchunguzi wa Rais Magufuli Maabara kuu ya Taifa

Nadhani mkuu wewe ndio una tatizo kwa kutaka wafanye unachokitaka wewe tu kuwa ndio kiwe sasa,

Hoja hupingwa kwa hoja na si porojo na viroja.
 
Wewe umesomea wapi utaalamu wa maabara? Unatoa hukumu halafu unasema unaunda tume, ya nini wakati umeshatoa hukumu? Nani mwenye ubavu wa kwenda kinyume na tamko la mzee?
 
Baki na Siasa kwanza mkuu...Mwanafunzi wa kidato cha kwanza amepewa mtihani wa kidato cha sita na kufeli ila watu wanacheka eti huyu mwanafunzi ni mjinga maana atafeli kivipi wakati ni mwanafunzi.
Baba asiongee kama kaka wala baba mdogo.
 
Wewe umesomea wapi utaalamu wa maabara? Unatoa hukumu halafu unasema unaunda tume, ya nini wakati umeshatoa hukumu? Nani mwenye ubavu wa kwenda kinyume na tamko la mzee?
Wewe kama una hoja tofauti na zilizo tolewa lete hoja yako hapa tuijibu mkuu na si porojo kama unavyotaka.
Yeye kafanya uchunguzi wake na kaeleza shaka aliyo nayo juu ya vipimo na wataalam ndio mana kaitisha tume yya uchunguzi, hao wataalam nao wakaja na hoja zao kumpinga lakini bado zinaleta ukakasi kama nilivyo eleza hapo kwenye mada.

Sasa kama wewe una utetezi mwingine wa hizo hoja ama hoja mpya ilete hapa tuijadili.
 
Baki na Siasa kwanza mkuu...Mwanafunzi wa kidato cha kwanza amepewa mtihani wa kidato cha sita na kufeli ila watu wanacheka eti huyu mwanafunzi ni mjinga maana atafeli kivipi wakati ni mwanafunzi.
Baba asiongee kama kaka wala baba mdogo.
Wewe ndio unayeleta siasa kwa kuacha kujadili hoja na kuleta maneno mengi, hoja ziko mezani hapo chagua inayo kufaa tuijadili tuone kosa liko kwa nani na si maneno maneno mkuu.
 
sijakielewa ndiyo maana nikawauliza ?
Basi hayo yatakuwa ni matatizo yako binafsi ya kuelewa mkuu, labda usome tena mada hapo juu labda waweza kupata neema ya kuelewa.
 
Sijaona hoja ya maana hapa, thread nyingine ni kupoteza muda, full upupu...
 
Unachekesha sana mkuu,yaani unaniletea mfano wa simu kweli?Mambo magumu unatumia mfano mwepesi namna hiyo?Nimesema kutest ubora wa kifaa huwa zinapelekwa known specimen!Ndio maana nikasema ilipaswa zipelekwe sampuli tofauti ambazo zinajulikana matokeo yake ili kubaini accuracy ya vifaa!Sasa hizo sampuli zilizoenda si za binadamu,suala la kubaini kwanini zimeleta matokeo hayo inahitaji uchunguzi!Maana huwezi jua huenda zina element ambazo zinaleta matokeo sawa na za Covid 19!Kujua competence ya vifaa ilihitajika sampuli ambazo kifaa kimekuwa designed kupima!Hata waliotengeneza hizo machine lazima walitest kwa sampuli za binadamu na sio za wanyama na mapapai!Tuweni objective,yaani unajua ni process gani inapitiwa kujua sampuli ni ya kitu gani?Unataka sampuli zikienda,maabara waanze kupima DNA ili kujua ni sampuli za binadamu halafu ndio waanze kupima Corona?Kweli tuna hiyo luxury?Unajua itachukua muda gani kama kila sampuli inayofika ikianza kupimwa DNA?Kwa wale ambao wameshawahi kufanya vipimo vya DN! wanajua huwa inachukua muda gani!Halafu tupime DNA halafu tukishagundua ni za binadamu au sio binadamu inatusaidia nini?Maana tupo kwenye janga la Corona so sioni mantiki ya kupima DNA walati tunajua sampuli zinazokwenda huko ni za binadamu na tunataka kutest Corona!Tuache hizi siasa nyepesi kwenye mambo ya kitaaluma!Ningekubaliana na JPM kama angetuma known specimen za binadamu majibu yakawa tofauti!Ukifikiri kwa kina utaelewa hoja yangu!Weka mahaba pembeni na kuwa reallistic!
 
Usifaninishe PhD fake na wanasayansi.

Wanasayansi gani ambao hawawezi kupata fomula yao kwa uvumbuzi wowote, akili zao wanategemea kila kitu fomula itoke nje wao ni kukariri tu.
 
Mkuu tusichoshane bure hapa.

Umesema kipimo kinapima specimen maalumu, ikiwa tofauti maana yake haiwezi kuzitambua itakuwa Unknown.

Sasa sample za hayo mapapai vimeleta positive na negative

Ukasema imekuwa positive kwasababu labda sample iliyo letwa iko contaminated sawa hilo linawezekana ikiwa kama kuna uzembe ulifanyika.

Sasa je haya yaliyokuja negative nayo imekuawaje, mbona hicho kipimo hakikusema kuwa hiyo sample haitambuliki??
Hii negative nayo imekuwa contaminated na nini hadi jibu lije negative??
 
Wanasayansi gani ambao hawawezi kupata fomula yao kwa uvumbuzi wowote, akili zao wanategemea kila kitu fomula itoke nje wao ni kukariri tu.
Wanatuambia eti sample wakati mwingine zinakuwa contaminated, wakati wa ukusanyaji ama wakati wa upimaji.
Sasa kama ni hivi inamana kuna watu majibu waliletewa positive wakati kumbe labda sample zao zilikuwa contaminated wakati wa process nzima ya upimaji.

Tukisema wanakuwa wazembe hawataki kuambiwa.
 
PhD Fake ya maganda ya korosho na udaktari wa binadamu wapi na wapi
 
Hivi ukiwa baba na nyumbani kuna njaa,nani anapaswa kulalamika?

Mh. Yeye ndio baba, mpaka vinafika hapa nchini hivyo vipimo alipaswa kuwa na taarifa za awali za vipimo hivyo.

Nawaza tuu walioko huko sijui kantini na wako negative
 
Wanaposema test ni specific hawana maana kuwa ni PCR ni specific kwa ajili ya bacteria na Virus bali ni procedure/protocol inayotumika kutest hao virus ndiyo iko specific. PCR ni molecular based technique ambayo inatumika pia kutest mimea (kama vile GNO foods) na wanyama pia.

Vifaa havikuja kwa ajili ya Corona vilikuwepo na vilikuwa vinafanya test nyingine. Kilichofanyika ni kuvalidate method kabla ya kuitumia kujua kuwa inafanya kazi sawasawa. Hii iko recommended na WHO ambyo inazitaka maabara zote kupeleka walau vipimo kumi vya mwanzo (5 Positive, 5 negative) kwao ili kuverify.
 

Sample kuwa contamined haina maana kuwa contamination imetokea maabara. Kwa jinsi ilivyo contamination itakuwa imetokea kule sample zilipotokea au katikati. Kwa kuwa surfaces zinaweza kuwa contaminated kwa muda mrefu mpaka siku 8 inawezekana kama zilitoka sokoni basi hizo samples zinawezekan kuwa zimekuwa contaminated na surfaces za soko or anything which came into contact with those samples. Waliozichukua hizo samples kama hawako trained wanaeza pia kuasabisha contamination.

Kama contamination ingekuwa kwenye maabara basi control samples kama vile negatine na blank samples zingekuwa na majibu yenye walakini na Wataalamu wa maabara wangegundua hicho kitu.
 
Mkuu hebu ngoja kwanza, hivi vifaa vilikuwepo hapa nchini kabla ya corona na vilikuwa vikitumika kwa matumizi mengine!!?? Ama sijakuelewa vizuri.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…