Hebu tuanzie hapa: Ben Saanane alitoka kwao saa mbili asubuhi ila hakurudi mpaka leo. Yupo hai? Kuna huu ujumbe aliotuambia

Sasa mzingira ya MO yalivyokuwa ya Kipumbavu vilee wewe unashindwaje kuamini wahusika wale wale wamefanya Movie ya Kipumbavu kwa lissu...???

Sent using Jamii Forums mobile app
Tufanye wahusika ni walewale. So tukubaliane ni fake movie. Na tukubaliane wahusika hawakuwa na lengo la kuua na sio wauaji na ndio maana waliishia kupiga ovyo risasi na hakuna risasi iliyompata kwenye spinal cord. Kama lengo lingekuwa ni kuua hakuhitaj risasi 38.wala kuingia na gari hadi ndani kwa lisu.

Sent using Jamii Forums mobile app
 

Mkuu hakuna kisingizio chochote kinacho halalisha umauti wa mtu. Uhai wa mtu ni wa umuhimu wa hali ya juu hata katiba ya nchi inalitambua hilo.Ndio maana sheria hairuhusu mtu kujinyonga wala watu kuchukua sheria mkononi kumuua jambazi au mwizi. Vipi dola isichukue hatua stahiki na kutoa taarifa za kina za uchaguzi za kupotea, ama kuuwawa kwa Ben Saanane na wengine waliotajwa, ama kwa jaribio la kumuua Lisu. Vipi dola lichukulie uhai wa mtu kama wa kuku au bata. Mkuu kama mtu hutaki mambo yako ya hojiwe ni vyema usiingie kwenye mawala ya siasa na kuwa public figure. Ukiingia kwenye ulingo huu raia wanahaki ya kuhoji uhali wa elimu yako, ndoa yako na hata uraia wako. Mkuu nikumbushe miaka ya nyuma alikuwepo mheshimiwa mmoja akiitwa kihiyo alikuwa mbunge na naibu waziri. Kuna raia walihoji elimu yake na uhalali wa vyeti vyake, na mwishoni ya yote ilibidi ajiuzuru. Na ndio usemi wa vyeti kihio au elimu kihio ulipo anzia.
 

Mkuu mtapata taabu sana kujisafisha, kama maelezo ni rahisi kiasi hicho jeshi letu maakini linalofanya kazi kwa weledi mkubwa na inteligensia ya hali ya juu, limeshindwaje kulibaini hilo na kutoa taarifa ya uchunguzi kwa mbwembwe, kama wanavyotoa taarifa za kuzuia mikutano ama maandamano. Na alieng'oa cctv cameras za eneo hilo ni nani? Kama kwaida yenu likitajwa jina la Lisu lazima mjiharishe.
 

Samahani mkuu unataka kituaminisha kuwa hiyo PhD ya mkulu ina mazonge mazonge?na yoyote atakaeihoji itakula kwake? Nauliza tu mkuu.
 
Mkuu elewa tu ni tukio fake

Sent using Jamii Forums mobile app
 
So unataka kusemaje kulingana na mada tajwa hapo juu, inaonekana inajua mengi.
Hiyo ilikuwa na warning ya patron wetu tulipokuwa tunakua, he's been there probably done it; kwa hiyo akikwambia you know he's knows what he's talking about.

Point kubwa ni hii, kupambana na mamlaka; ukiwa uko right au wrong inakuja na risks; na hiyo ni dunia nzima. Kwa hiyo ujipange, haina tofauti na Russian Roulette. Check interview ya former Head of ISI Pakistan Head to Head with ISI - Head.

Statecraft sio kitu ya kuchezea wakati mwingine, na ukichezea ujue risk zake.
 

Mkuu hujasikia viongozi wa chadems wakiomba ruhusa kwa wachunguzi wa nnje kuja kuisaidia kufanya uchaguzi lakini wamekataliwa na serekali sababu jeshi letu la polisi lina uwezo mkubwa wa kuchunguza, hivyo hadi leo wanasubiri taarifa ya huo uchunguzi. Kumbuka mkuu huwezi kuwapangia polisi lini wakupe taarifa.
 
So point ya mwisho wahusika wa hayo matukio ni Wapumbavu sana...!! na suala la risasi kwenye spinal cord ni Dr tu anaweza sema kama ni kweli ausioo kwelii..

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ben Saanane alitumwa na Mbowe Afrika Kusini, kumbe ilikuwa janja ya kumuuwa ili kuficha wizi wa ruzuku ya chama.

Ni kama Chacha Wangwe tu alichofanyiwa

Sent using Jamii Forums mobile app
Iko hivi, kwa jinsi serikali ya CCM inavyotaka kuumaliza upinzani, kama kweli CHADEMA au MBOWE angekuwa amehusika na kifo cha Chacha Wangwe, na kama angehusika kweli na "Kupotea" kwa Ben Saanane, basi system ingemshughulikia mara moja. as it is, hawajadiriki hata kusema hayo. na kama hivyo ndivyo, basi kwa nini Serikali inakataa kuita wachunguzi wa nje waje waseme hayo unayosema? Maana kama serikali ingekuwa hata na shaka tu, ingewaita ili hao wa nje waitaje CHADEMA kwamba imehusika. hapo si ingekuwa ndiyo mwisho wa ADUI namba moja wa CCM na Serikali yake? maana kama serikali ingewahusisha CHADEMA watu wangesema serikali inawasingizia, kama katika suala la AKWILINA,
 

Mkuu isejekuwa ndio mliooneka moro kwa spidi kali mkitokea dodoma baada ya shambulio. Juhudi zako kubwa zkujisafisha na kupotosha hii habari zinaoneka. Lakini ni za kipuuzi na kilofa. Jaribu lingine labda utafanikiwa, lakini sio kwa hili. Kwa akili yako unaweza kutekeleza kuwa mheshimiwa Nape alijinyooshea mwenyewe bastola mbele ya waandishi wa habari.
 
Ni yaleyale kwamba eti wauaji wakaanza kurud Dar kwa speed hahahahahahah

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…