Hebu tujiulize undani wa hili ‘Tishio la UGAIDI’

Hizo ni propaganda za Wamarekani tu tena SAA nyingine ni sabotage ya kiuchumi.

RAIA wao wakipata alert kama hiyo wana cancel safari zao za kuja Tanzania, tunaoumia ni sisi, kwahiyo lazima uende sawa na Mmarekani.
 
Mkuu kama haujui mambo ya intelligence bora usiyagusie.
Unajua jinsi gani wnakusanya hizo taarifa za intelligence, jinsi wanavyozichambua na jinsi wanavyozishughulikia!?
Haoluna tofauti na wale wanaohofia kumjadili Mungu kwa sababu hawajasoma theolojia.

Intelejensia ni jambo la watu kwa ajili ya watu. Pia wapo wanaifahamu vyema bila hata kupitia vyuoni kwenu.

Umeisoma sheria ya usalama wa Taifa na marekebisho yake? Ipitie vyema utagundua matundu yalipo
 

Hapana kusahau pia kuna nchi zinazotuzunguka. Kuna wenye kukaanga mbuyu. Isidhaniwe nchi zote hizi ziko na furaha sana sisi tukiishi kwa amani.

Fikiria Chadema wakipigwa tukio hata na maadui zetu wa nje tu. Haitakuwa kumemwagiwa petroli kwenye moto?

Hakutakuwa tumeachiwa wenye meno kuumana?

Nani ataamini Mama hakuhusika?
 
Nyie hamuoni, Lissu aliporudi tu, na tishio likawepo!!
Haya dadavueni, sitaki matusi.
 
Jirani mtaa wa saba anatambua hatari ya nyumbani kwako
zile meli zilizokua zinaiba gesi kule Mtwara,
Israel ndiye aliyemshtua Tz ( wame sync transponders za meli kwenye database zao )
nyie mda huo mpo mmelala mnakoroma
 
zile meli zilizokua zinaiba gesi kule Mtwara,
Israel ndiye aliyemshtua Tz ( wame sync transponders za meli kwenye database zao )
nyie mda huo mpo mmelala mnakoroma
Sisi tupo bize kusoma msgs za mipasho za raia.

Serikali inapoweka raia wake ndo adui namba moja maana yake ni kuwa dola hiyo inajifitini inapaswa kubadilishwa waje wenye uzalendo na mahaba na Tanzania
 
Mkuu ukiwa na maarifa sahihi ndio unaweza ukajadili kitu kwa usahihi na hata maamzi yako yakawa na usahihi.
Ndio maana shambulio linapofanywa na magaidi moja kwa moja huwa wanajitanganza kama ni Al-qaeda au kikundi husika.
I agree to disagree, truth will prevail
 
Kuna ujinga mwingi sana umemezeshwa kwa watz na wakristo.

Kuwa unapotajwa ugaidi moja kwa moja wanahusishwa waislam.

Ndio maana hata kipindi kile waliposema mbowe si gaidi walikuwa wanamaanisha magaidi kweli wapo lkn mbowe si mmoja wapo.

Athari ya sheria ya ugaidi inayowalenga zaidi waislam imesababisha hadi sasa kukamatwa waislam zaidi ya 300 na wakristo wasiozidi 3.

Mbowe, Joseph na Rwakatare.

Kwa wotw waliokamatwa hakuna hata mmoja alipatikana na hatia. Lkn sio hatia tu Bali upelelezi haujakamilika wakiendelea kuoza ndani ya mahabusu wengine zaidi ya miaka 10.

Sheria ya ugaidi ilitungwa kwa shinikizo la marekani.

Kwa kabla ya sheria hiyo ipo sheria ya uhalifu nchini.

Ili madai ya kutumgwa kwa sheria hii yaweze kutimia kila Mara serikali ya marekani imekuwa ikitengeneza hofu kwa nchi kuwa kina tishio la ugaidi. Na wakati mwengine wao wenyewe hutengeneza tukio bandia.

Kwa mfano ktk moja ya matukio ya kutengenezwa lilitokea arusha ktk mkutano uliomuhusisha muwakili was papa kutoka Vatican.

Kwa wale wataokumbuka, ulitokea mlipuko ktk mkutano ule ambapo taharuki ile alionekana kijana mmoja akitoka mbio huku akiwa kavaa kanzu na barakashea au kofia. Na polisi ilifanikiwa kumkana na baada ya kumhoji ilibainika kijana yule alikuwa mkristo na alifahamika kwa jina LA Joseph. Hadi Leo hii hatujui kesi yake iliishia VP.

Matikio hata ya kutenfenezwa hujulikana kama false flag terror.

Mifano iko mingi ya mchezo huu was wamarekani.

Nimalizie kwa kusema kama kweli wamarekani wamenasa mawasiliano ya magaidi basi wapeleke taarifa za namba za hao magaidi polisi.

Haiyumkini maeneo waliyotaja yanapangwa na watu wanaotumika na wamarekani kutenfeneza tukio bandia.

Kutiwa kama nchi inaelekea kutaka maridhiano ili kurwjesha umoja. Umoja hauwezi kuwapo kama watu hawaelewani. Na ili tuelewane lazima tuvumiliane kuwa sisi watz tuko na tamaduni tofauti.

Utamaduni wako usolazimishe wengine wafate Bali washawishi.

Waislam ni watu wema. Chuki dhidi ya waislam umepelekea mchungaji kama kimaro amesimamishwa utumishi kwa kusema tu vijana wa kiislam wana maadili. Hii inaonyesha kama angesema kinyume chake angepandishwa hata cheo.

Mtakumbuka kiongozi mmoja mwandamizi aliwahi kutamka kuwa znz hatuwapi upinzani kwa sababu wataleta watu wenye ndevu nyingi.
Chuki, chuki, chuki

Hivi majuzi ulitokea pia mjadala was kitaifa kuwa kuna ndege kutoka uarabuni zimetua uwanja was KLM na ARUSHA. Lkn ndege za mizogo za wazungu zinatotua ktk migodi yetu kila kukicha wao hawaoni kuwa ni tatizo.

Kwa upande mmoja nasema tu bora chadema ichukuwe nchi na ianzishe seerikali za majimbo yatayokuwa huru kujitawala. Kila mmoja abebe fito zake.
 
Somalia ni divided state ambapo mpaka sasa bado hawajaweza kusimama kama Taifa moja.

Hali ya Tanzania ni amani hakuna guerilla wala civil chaos na serikali imerelax ambapo imewekeza kuchunguza wanachowaza wananchi dhidi ya viongozi
Imewekeza kukamata walevi wanaopitiliza muda wa Mama Samia na wanaobet.
 
Mkuu umeweka hoja nzito sana sana.
Hongera umezungunza ukweli
 
Kuna mdau humu anajitahidi tusijadili suala la usalama wetu kama raia kwa sababu HATUJUI LOLOTE.

Hizi akili za ajabu sana
Unajua lolote kuhusu usalama,au elimu yako kuhusu usalama imejengwa na movie za James bond na 24!?
 
Acha udini
 
Nimeona KLM same to a statement inayokaribiana na ya US embassy Dar.


Ni muhimu Watanzania tujadiliane haya mambo kama yapo kweli au tunatengenezewa mkwamo ambapo tutaweza kusingiziwa kuwa tunashirikiana na vikundi vya kigaidi halafu tuchezee vikwazo ilihali maisha halisi ni full vikwazo
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…