Hebu tuzungumzie scientific research

Hebu tuzungumzie scientific research

mamanalia

JF-Expert Member
Joined
Nov 7, 2009
Posts
666
Reaction score
146
Hapa kwetu TZ siku hizi kuna watu wengi wanaitwa Dr. somebody au Prof. somebody. Lakini ukienda kwenye strong journals duniani huwakuti kabisa majina yao katika articles. Hivi huwa wanapata hizo PhDs na uProf. vipi? Yani mtu anajiita Prof halafu anakaa miaka hajafanya publication? hata wanafunzi wa masters tu amewakosa ili waweze kuproduce papers! Inabidi tuchunguze au nako huko vyuoni kuna ufisadi wa kuinuana tu na kupeana u prof kwa reports za hapa na pale na vijiconference vya morogoro, arusha na dar?
 
Hapa kwetu TZ siku hizi kuna watu wengi wanaitwa Dr. somebody au Prof. somebody. Lakini ukienda kwenye strong journals duniani huwakuti kabisa majina yao katika articles. Hivi huwa wanapata hizo PhDs na uProf. vipi? Yani mtu anajiita Prof halafu anakaa miaka hajafanya publication? hata wanafunzi wa masters tu amewakosa ili waweze kuproduce papers! Inabidi tuchunguze au nako huko vyuoni kuna ufisadi wa kuinuana tu na kupeana u prof kwa reports za hapa na pale na vijiconference vya morogoro, arusha na dar?

Mama... hilo umeligundua leo? Lipo tena kwa sana. Jaribu kuchukua majina ya walimu wako (Ma-Dr na Ma-Prof) halafu uyachape kwenye search engine za maana kama Pubmed, usishangae kukuta mtu hayumo! Kuna mwalimu wangu ana paper moja tu kwenye Pubmed!!

Hata hivyo mambo ya Sayansi hayana mshiko hapa JF. Ni siasa kwa kwenda mbele!!🙄
 
Hata hivyo mambo ya Sayansi hayana mshiko hapa JF. Ni siasa kwa kwenda mbele!!🙄

Yeah,JF haina mshiko sana kwenye Science.Siasa imezidi sana humu ndani.Hata hivyo ili ku-improve ushiriki wa watu kwenye category ya science and technology....wakuu wangevunja badala ya kuwa na science and technology tungekuwa na categories nyingi nyingi ndogo ndogo ambazo ziko very particular mfano MEDICINE,COMPUTER SCIENCE etc.....yaani maeneo ya namna au tunaweza ku-break down further ili mtu achague interest yake....

Mtazamo tu...
 
Yeah,JF haina mshiko sana kwenye Science.Siasa imezidi sana humu ndani.Hata hivyo ili ku-improve ushiriki wa watu kwenye category ya science and technology....wakuu wangevunja badala ya kuwa na science and technology tungekuwa na categories nyingi nyingi ndogo ndogo ambazo ziko very particular mfano MEDICINE,COMPUTER SCIENCE etc.....yaani maeneo ya namna au tunaweza ku-break down further ili mtu achague interest yake....

Mtazamo tu...


Labda hiyo inaweza kusaidia lakini uzoefu wangu wa hapa jamvini unaonesha kuwa ni watu wachache sana wanapenda kusoma mambo ya kisayansi hata kama ni habari tu! Inasikitisha sana kwa sababu post za siasa zinapaa sana kuliko nyingine zote. Hata mambo ya mapenzi yana washabiki wengi tu lakini siyo sayansi ya aina yoyote (be it social or natural science)!! Labda tupate maoni ya wadau wengine ila kama ingewezekana huu ukumbi ungesaidia sana kuwa tunapeana habari kuhusu breakthroughs zinazofanyika katika anga mbali mbali za S&T.
 
Hapa kwetu TZ siku hizi kuna watu wengi wanaitwa Dr. somebody au Prof. somebody. Lakini ukienda kwenye strong journals duniani huwakuti kabisa majina yao katika articles. Hivi huwa wanapata hizo PhDs na uProf. vipi? Yani mtu anajiita Prof halafu anakaa miaka hajafanya publication? hata wanafunzi wa masters tu amewakosa ili waweze kuproduce papers! Inabidi tuchunguze au nako huko vyuoni kuna ufisadi wa kuinuana tu na kupeana u prof kwa reports za hapa na pale na vijiconference vya morogoro, arusha na dar?

Wasomi wengi wamegeuka wanasiasa!
Sasa watu kama Prof. Msola ndio hao wameamia kwenye siasa, huo utafiti utafanywa saa ngapi?! Tatizo letu bongo ni misallocation of resources (ikiwemo rasilimali watu) na kushindwa kutofautisha politik na academics.

Utafiti wa kisayansi unahitaji kuwekeza pesa nyingi sana jambo ambalo Tz hatujalipa kipaumbele. Nadhani kama kungekuwa na tafiti za kutosha, ugonjwa kama malaria lisigekua tatizo kwa sasa!
 
Professor Majimarefu,Professor Vulata(RIP),Dr Remmy Ongala...hawana research papers
 
wengi hapa bongo ni vyakupewa kisiasa siunajua tumetawaliwa kisiasa zaidi
 
Mama... hilo umeligundua leo? Lipo tena kwa sana. Jaribu kuchukua majina ya walimu wako (Ma-Dr na Ma-Prof) halafu uyachape kwenye search engine za maana kama Pubmed, usishangae kukuta mtu hayumo! Kuna mwalimu wangu ana paper moja tu kwenye Pubmed!!

Hata hivyo mambo ya Sayansi hayana mshiko hapa JF. Ni siasa kwa kwenda mbele!!🙄

Kwi kwi kwi,
Nafasi ya kupenya BOT kama wewe mwanasayansi utaipata wapi? Hata hiyo ya kufundisha tu huipati hata kama uwezo unao kama wewe sio ndiyo mzee! Kamulize Prof Baregu!

Wakati wenzenu wanagawana keki mil 30, 50, 100, nyie mnagawana mmba kwa ajili ya kukuna kichwa, eti sayansi!

Hadhi Tz itarudi pale wasomi watakapoona nafasi yao na kuacha kuwabeba wanasiasa kwa mbeleko. Wajisikie huru kusimama popote sio ndani ya ccm tu, na hapo ndipo wanapoweza kuwa na nguvu ya kuanisha pumba na mchele uko wapi! Hatujiulizi ni kwanini wanasiasa uchwara wana nguvu ya kupindukia?
 
Kwi kwi kwi,
Nafasi ya kupenya BOT kama wewe mwanasayansi utaipata wapi? Hata hiyo ya kufundisha tu huipati hata kama uwezo unao kama wewe sio ndiyo mzee! Kamulize Prof Baregu!

Wakati wenzenu wanagawana keki mil 30, 50, 100, nyie mnagawana mmba kwa ajili ya kukuna kichwa, eti sayansi!

Hadhi Tz itarudi pale wasomi watakapoona nafasi yao na kuacha kuwabeba wanasiasa kwa mbeleko. Wajisikie huru kusimama popote sio ndani ya ccm tu, na hapo ndipo wanapoweza kuwa na nguvu ya kuanisha pumba na mchele uko wapi! Hatujiulizi ni kwanini wanasiasa uchwara wana nguvu ya kupindukia?


Nono, nimekupa senksi na kama ingeruhusiwa ningekuongezea.

Tz ni nchi ya ajabu. Juzi nilisikia Pinda anamfokea Injinia huko A-town. Heshima kwa wataalamu hakuna na wasomi badala ya kupigania haki yao ili waheshimiwe na kuthaminiwa wameingia mkenge wa kukimbizana na kura ili wakapige porojo. Wakati Sarungi alipoikimbia MOI pale Muhimbili na kuwa mwanasiasa tulimshangaa sana. Kwa sasa hakuna tatizo tena. Baraza la mawaziri tu lina maprofesa kibao na PhD za kumwaga (ingawa nyingine ni za kichina). Hapa hatutoki kabisa. Tumetumbukia kwenye matope!!
 
huko vyuoni kuna ufisadi wa kuinuana tu na kupeana u prof kwa reports za hapa na pale na vijiconference vya morogoro, arusha na dar
habari ndiyo hiyo! katika nchi za wenzetu mtu anakuwa Dr. lkn sio prof. kwani unaweza kuwa Dr. kwa kusomea degree tu (baada ya masters), baada ya hapo kama hujafanya mambo ya risachi zaidi wewe utabakkia Dr. fulani tu...ukifanya risachi na ukafanikiwa ku publish 'journals', kuhudhuria international conferences ndio wanaangalia namna ya kukupandisha kwenda assnt prof, assoc prof na prof. hatua hizi zote ni mpaka uwe na uzoefu kazini na publication za maana. lkn bongo sivyo...kamati zinakaa tu na kuamua aaah fulani sasa ni Prof teh teh teh teh...
 
.................. Baraza la mawaziri tu lina maprofesa kibao na PhD za kumwaga (ingawa nyingine ni za kichina). Hapa hatutoki kabisa. Tumetumbukia kwenye matope!!

mzee, nimelazimika kuchangia baada ya kuona hilo nililokoleza wino! hujatembea wewe!!!!!!!, ukifika china na kuona maendeleo waliyopata kwa miaka 60 ya uhuru wao, hutadharau tena elimu yao na wala hutasaga bidhaa za china kwa greda eti "feki".

china leo wanamalizia kuweka metro kwenye tu-miji tudogotudogo, tena bila msaaada wa kiufundi, wala wa kifedha toka kokote nje ya china!!! we hapo bongo tunaweza kufanya nini??? hata barabara korofi hazitengenezwi hadi tutemewe mate na wazungu!!

hata huyo sijui sarungi aliyekuwa na elimu unayoiabudu, alipokuwa moi alifanya nini? wagonjwa walikuwa hawapelekwi nje kwa matibabu ya mifupa? ndi maana alipoona hafanyi kitu akajisalimisha kwenye siasa! tafakari kidogo ndugu kabla hujaingia jamvini!
 
mzee, nimelazimika kuchangia baada ya kuona hilo nililokoleza wino! hujatembea wewe!!!!!!!, ukifika china na kuona maendeleo waliyopata kwa miaka 60 ya uhuru wao, hutadharau tena elimu yao na wala hutasaga bidhaa za china kwa greda eti "feki".

china leo wanamalizia kuweka metro kwenye tu-miji tudogotudogo, tena bila msaaada wa kiufundi, wala wa kifedha toka kokote nje ya china!!! we hapo bongo tunaweza kufanya nini??? hata barabara korofi hazitengenezwi hadi tutemewe mate na wazungu!!

hata huyo sijui sarungi aliyekuwa na elimu unayoiabudu, alipokuwa moi alifanya nini? wagonjwa walikuwa hawapelekwi nje kwa matibabu ya mifupa? ndi maana alipoona hafanyi kitu akajisalimisha kwenye siasa! tafakari kidogo ndugu kabla hujaingia jamvini!

Naona unajaribu kuchukulia issue hii personal wakati mimi nimechangia kiujumla. Kama unaishi Tanzania kwa sasa utakuwa unaelewa maana mtu anaposema kitu ni cha kichina. Kama hujakutana na hilo neno basi pole na omba watu wakusaidie, badala ya kuanza mashambulizi yasiyo ya lazima. Kwani bidhaa za feki za kichina hazipo Kariakoo na kwingineko? Kama ulitaka kueleza kuwa wachina wanafanya vitu genuine basi tueleze viko wako wapi katika soko letu? Watu wanaongelea wanachokiona na siyo hadithi. Kama kwao wanatenegeneza vitu vya maana wakati sisi tunaletewa feki bado tutawaponda tu!
 
Mimi siwalaumu sana kwenye ku-publish, maana hata huko kwenye majournal 'siasa' imeshaingia na ku-dominate kwa kiasi flani. Tatizo ninaloliona mimi ni mchango wao ktk fani husika. Je wana input yeyote hata kama ni ndogo? Wana-website kuonesha currently wanafanya nini? au wapo kwenye initiative ipi? wanaendaje na mabadiliko ya haraka ktk uvumbuzi..etc..
 
Naona unajaribu kuchukulia issue hii personal wakati mimi nimechangia kiujumla. Kama unaishi Tanzania kwa sasa utakuwa unaelewa maana mtu anaposema kitu ni cha kichina. Kama hujakutana na hilo neno basi pole na omba watu wakusaidie, badala ya kuanza mashambulizi yasiyo ya lazima. Kwani bidhaa za feki za kichina hazipo Kariakoo na kwingineko? Kama ulitaka kueleza kuwa wachina wanafanya vitu genuine basi tueleze viko wako wapi katika soko letu? Watu wanaongelea wanachokiona na siyo hadithi. Kama kwao wanatenegeneza vitu vya maana wakati sisi tunaletewa feki bado tutawaponda tu!

kwa sasa siko tz lakini huo msemo naufahamu, nieshawishika kutahadharisha baada ya kuona hata great thinker anaponda bidhaa za china!

labda nikuulize, kama kitu ni feki na kinafanya kazi iliyokusudiwa na kinauzwa kwa bei nafuu ili kila mtu amudu kununua, kuna madhara gani? ningefurahi kama wangefanya kazi ya kuvi-study vtu ivyo ili kuangalia namna ya kukopy technolojia rahsi badala ya kuviponda ukiwa huna kitu katika soko lako cha kujivunia!

tunapaswa kuacha kasumba ya kushabikia vitu vya ulaya kwani hata huko nako kunatoka feki.

ili utengeneze genuine unaanza na na kitu (whether feki or otherwise) kisha unaendelea kuboresha. ndivyo walivyofanya hata ulaya na wanaerndelea kufanya hivyo hadi leo. hivi vitu mnavyoita feki huwa vinatolewa kwa bei nafuu ili kila mtu amudu kununua. ndivyo ilivyo hata kwa magari yaliyotumika. wangecrash magari yote ya mitumba, wangapi dar wangekuwa na magari? achilia mbali nguo!

tuamke,tujitetee,

hao wanaocrash vitu kwa madai ni feki wamo kwenye payrol ya mafisadi na wanwasafishia njia wauze mizigo bila ushindani, kama ulikuwa hujui, habai ndiyo hiyo!
 
Mgombea Ubunge;705099]kwa sasa siko tz lakini huo msemo naufahamu, nieshawishika kutahadharisha baada ya kuona hata great thinker anaponda bidhaa za china!

labda nikuulize, kama kitu ni feki na kinafanya kazi iliyokusudiwa na kinauzwa kwa bei nafuu ili kila mtu amudu kununua, kuna madhara gani? ningefurahi kama wangefanya kazi ya kuvi-study vtu ivyo ili kuangalia namna ya kukopy technolojia rahsi badala ya kuviponda ukiwa huna kitu katika soko lako cha kujivunia!

Mimi sina ugomvi na vitu vya bei rahisi au vya kutoka china. Kwenye ile post yangu nilitumia neno kama wanavyotumia wengine (loose meaning). Hata hivyo napata shida kwa jinsi hali ilivyo sasa hapa Tz ambapo mtu unahahikikishiwa na wauzaji kuwa kitu ni genuine kumbe ni feki toka china. Hapo ndipo ugomvi unapoanzia. You pay deally to get fake stuff! Kama tungeletewa genuine kama bidhaa zinazopelekwa Ulaya na US hayo huo ugomvi usingekuwepo. Wachina kushirikiana na wahuni na mafisadi kutuibia kunaleta damage kwa pande zote mbili. Kwa hiyo Wachina hawawezi kukwepa lawama ingawa ujinga ni wetu na sisi (Watanzania) ndio tunabeba lawama kubwa!

tunapaswa kuacha kasumba ya kushabikia vitu vya ulaya kwani hata huko nako kunatoka feki.

ili utengeneze genuine unaanza na na kitu (whether feki or otherwise) kisha unaendelea kuboresha. ndivyo walivyofanya hata ulaya na wanaerndelea kufanya hivyo hadi leo. hivi vitu mnavyoita feki huwa vinatolewa kwa bei nafuu ili kila mtu amudu kununua. ndivyo ilivyo hata kwa magari yaliyotumika. wangecrash magari yote ya mitumba, wangapi dar wangekuwa na magari? achilia mbali nguo!

tuamke,tujitetee,

hao wanaocrash vitu kwa madai ni feki wamo kwenye payrol ya mafisadi na wanwasafishia njia wauze mizigo bila ushindani, kama ulikuwa hujui, habai ndiyo hiyo!

Hapo tuko pamoja. Ndio maana tunalalama kuwa kama siyo kutelekeza sayansi na elimu kwa ujumla tusingekuwa tunaagiza hata viberiti toka China.
 
Wasomi wengi wamegeuka wanasiasa!
Sasa watu kama Prof. Msola ndio hao wameamia kwenye siasa, huo utafiti utafanywa saa ngapi?! Tatizo letu bongo ni misallocation of resources (ikiwemo rasilimali watu) na kushindwa kutofautisha politik na academics.

Utafiti wa kisayansi unahitaji kuwekeza pesa nyingi sana jambo ambalo Tz hatujalipa kipaumbele. Nadhani kama kungekuwa na tafiti za kutosha, ugonjwa kama malaria lisigekua tatizo kwa sasa!


Unachosema ni kweli kabisa. Kuna mkanganyiko mkubwa sana, kila kitu kinawekwa kisiasa zaidi kuanzia uandikaji wa proposal hadi kupata permit ya kufanya research sasa haishangazi kuona hata wanascience wenyewe wamegeuka wanasiasa.
Ukweli ni kuwa watu tuko after money zaidi,na hizi pesa za tafiti za kisayansi mara nyingi zote zinaishia hukohuko kwenye tafiti kwa hivyo haziwapi watu ushawishi.
 
Thread na posts nimezipenda.
Kila mdau afanye homework vizuri,tusiridhike na tulipofikia,tuzidishe kusoma,kufikiri ,ku share idea...tuondoe kubaniana vyuoni,tuwe more practical na tujiamini kuwa tunaweza kufanya.
 
Mimi sina ugomvi na vitu vya bei rahisi au vya kutoka china. Kwenye ile post yangu nilitumia neno kama wanavyotumia wengine (loose meaning). Hata hivyo napata shida kwa jinsi hali ilivyo sasa hapa Tz ambapo mtu unahahikikishiwa na wauzaji kuwa kitu ni genuine kumbe ni feki toka china. Hapo ndipo ugomvi unapoanzia. You pay deally to get fake stuff! Kama tungeletewa genuine kama bidhaa zinazopelekwa Ulaya na US hayo huo ugomvi usingekuwepo. Wachina kushirikiana na wahuni na mafisadi kutuibia kunaleta damage kwa pande zote mbili. Kwa hiyo Wachina hawawezi kukwepa lawama ingawa ujinga ni wetu na sisi (Watanzania) ndio tunabeba lawama kubwa!

nimekupata mkuu ..............

Hapo tuko pamoja. Ndio maana tunalalama kuwa kama siyo kutelekeza sayansi na elimu kwa ujumla tusingekuwa tunaagiza hata viberiti toka China.

nimekupata vizuri sana mkuu, sasa tumewekana sawa. muhimu tuendeleze harakati za kuleta mapinduzi ya technolojia ya viwanda nchini mwetu..............

asante pia kwa kujadili nami kwa lugha njema
 
Back
Top Bottom