HEDGE WITCH: Uchawi usiopendwa zaidi duniani

Naomba vigezo vya kujiunga na hicho chuo uchawi huko marekani........elimu haina mwisho
 
Wachawi wa Afrika wako vizuri. Wanapanda nyungo wakati wenzao wa ulaya wanakalia vimifagio.
 
Wachawi wa Afrika wako vizuri. Wanapanda nyungo wakati wenzao wa ulaya wanakalia vimifagio.
 
Naomba vigezo vya kujiunga na hicho chuo uchawi huko marekani........elimu haina mwisho
Yaani umekosa vyuo vyote vya kujiunga umeamua kutaka kujiunga na chuo cha uchawi [emoji848][emoji848][emoji848][emoji848]
 
Kenya wameanzisha chuo wamechoka na hedges
 
NITAANDIKA PAREFU, JITAHIDI KUSOMA YOTE UTABARIKIWA. kitu cha muhimu kuelewa ni kwamba, uchawi ni spiritual force, kama ulivyo utauwa pia. shetanina taratibu zake zote huwa anaoperate kiroho, na Mungu pia anaoperate kiroho sio kimwili. ukitaka kuushinda uchawi operate kiroho against them, yaani vaa nguvu ya kiroho iliyo kubwa kuliko nguvu zao, na nguvu hiyo pekee unaipata baada ya kuokoka na kujazwa Roho Mtakatibu na kuishi ukiwa na uwepo wa Kimungu.

why uwepo wa Kimungu? Ni kwasababu mchawi/shetani anapokuja kwako haji kwa cheo chako kama labda anajiandaa kuja kwako mchungaji au mtu fulani wa Mungu, hilo halipo kwake, yeye anaangalia kwa macho ya kiroho hivyo tunaweza kuwa tunawaona watu katika ulimwengu wa mwili kama ni watu wa Mungu kumbe hawana nguvu za Mungu na shetani au wachawi hawawadefine kama hao ni watu wa Mungu, hivyo anapokuja kwako atakuja kwako kama mtu wa kawaida tu na anao uwezo wa kukudhuru hata kama umetoka dhehemu la kilokole (nasema hivi kwasababu madhehebu mengine yooote ambayo sio ya Kipentecost, imekuwa proven kwamba wanalogeka, uliza ex-mchawi yeyote atakwambia).

namna ya kuwashinda, hakikisha unaishi na uwepo wa Mungu, uwepo wa Mungu ndio pekee unaofanya uchafu wa dunia hii usikusogelee, na ndio unaoattract malaika wa Mungu washuke ghafla kushambulia maadui zako/kukutetea pindi unapokabiliwa na maadui. kwa wale waliookoka, unaweza kuwa unatembea sehemu flani pengine hata kama haupo vizuri sanaa kiroho lakini una kapasentegi fulani ka uwepo wa Mungu, unakuta ghafla kuna hali fulani ya uwepo wa Mungu kwa dakika fulani, na baadaye unakuwa katika hali ya kawaida, ile huwa ni Malaika wa Mungu ametumwa kuja kukuokoa kwenye kitu fulani, na ile hali ya hewa ndio mfano mdogo wa hali ya hewa ya mbinguni, malaika kwa kuishi kule ameambukizwa uwepo kiasi kwamba akiwa karibu yako unauhisi kabisa huo uwepo.

Mungu akikusaidia ukawa umejazwa Roho Mtakatifu, ndio utakuwa unaishi na uwepo wa Mungu muda wote moyoni kwasababu Roho Mtakatifu ndio Mungu mwenyewe, na atakufunulia hata mambo yajayo, na yale magumu sana atayasambaratisha hata bila wewe kujua kwasababu katika dunia hii ukifunuliwa mambo yote uyajue hautalala usingizi, kwenye ulimwengu wa roho kuna maajabu mengi sana mengine ya kutisha kwa akili ya kimwili hauwezi kuyaangalia kabisa.

kwenye suala la nyota sijui nini etc, what I have learned in life ni kwamba, wala hautakiwi kupambana na kuhangaika ati unalinda nyota, utapiga sana maombi ya vita, utaletewa hadi vitabu uwe unavisoma na kutamka maneno ati unapambana, utapakwa mafuta, utakula chumvi za upako, utakula keki za upako na kuna siku wataleta wanawake wa upako mtawala (kwa jinsi manabii wa siku hizi walivyocharuka kimwili), hautafaniniwa kwasababu gani? JUA HILI KUANZIA LEO, kwa uwezo wetu hatuwezi kufanya lolote like bila Roho Mtakatifu, hata vita utakayopigana ukifikiri umeshinda ushindi sio w akudumu, unaweza kuwa wa siku moja au mbili keshokutwa adui huyo hapa....vita pekee utakayo shinda, au maombi pekee utakayooomba yakaleta majibu au ukawa na uhakika kabisa kwamba yamefika mbinguni na yatajibiwa, ni maombi ambayo Mungu mwenyewe anaomba,

maombi ambayo Mungu mwenyewe anaomba ni maombi ya Roho Mtakatifu, yaani kunena kwa Roho, pale Roho Mtakatifu anapokuwa anaomba ndani yako kwa lugha nyingine na kwa kuugua kusikoweza kutamkwa, kwani yeye ndiye anayojua unachohitaji, na maombi ya namna hiyo lazima yajibiwe. Yesu angeona tunaweza sisi wenyewe bila Roho Mtakatifu asingesema hawezi kutuacha yatima, aliwaambia wanafunzi wake wakae Yerusalem hadi Roho atakapo kuja. hivyo ukiomba kwa Roho, ukaimba kwa Roho, ukaabudu kwa Roho, kila kitu kwako kitakuwa fayaaaa.

ni kwasababu, Mungu ni Moto ulao, hivyo akiwa moyoni mwako huyu Roho ni kwamba ndani yako kuna moto ulao, unakula uchafu/unaunguza, shetani akijaribu kukusogelea, ataungua kabisa hivyo akiwa mbali tu atajua kuwa mahali pale sio pa kusogelea. kuna mchawi mmoja alinishuhudia anasema walipokuwa wanaruka, nyumba za walokoke walikuwa wanaona kuna moto unawaka kwa juu hivyo hawazisogelei kabisa. though kuna walokole wale wadanganyifu huo moto unakuwa haupo kabisa na mchawi anaweza kumfanya chochote hata kama anasali kanisa la kilokole.

kwa kusema haya, simaanishi kwamba siamini maombi ya kimwili, kuna kuomba kwa Roho, n a kuomba kwa akili pia. lakini ndugu yangu hata kuomba kwa akili, kama huna Roho hayo maombi ni bure na wewe mwenyewe moyoni utajikuta haina uhakikisho wowote, ni kwasababu ukiwa na Roho hata ukiomba kwa akili kuna kuwa na uvuvio fulani wa Roho, na ukitaja Jina la Yesu (kwasababu katika maombi yako lazima uombe kwa njia ya Jina la Yesu ndio yatajibiwa), ukitaja Jina hili wakati moyoni mkavu huna Roho, hakuna chochote kitatokea kwasababu hata wachawi hilo jina wanalitaja. unakumbuka wale waliokuwa wanamwigiza paulo, watu wasiookoka walienda mtaani ati wanatoa mapepo wakawa wanasema "kwa Jina la Yesu yule anayehubiriwa na kina Paulo/au Petro kama sikosei, Toka, mapepo yakawaambia, Paulo tunamfahamu na ninyi tunawafahamu, yakawarukia na kuwacharua walikimbia bila hata nguo. kwahiyo hata kutaja Jina la Yesu ili kufanye kazi unahitaji uvuvio wa Roho Mtakatifu, chochte kinachofanywa bila Roho Mtakatifu hicho hakina baraka ya Mungu, na ni hivyo kwasababu Yesu alipopaa alisema huyo Roho atafanya yale ambayo atayapokea toka Juu, na ni kwasababu kwa utatu mtakatifu Roho ndio Mungu yuleyule, basi ukamilifu wetu upo tukijazwa na kuishi na Roho Mtakatifu. hii ndio dawa pekee ya kuyashinda mashetani, mapepo, wakuu wa anga, wakuu wa giza, famla na mamlaka na majesho ya pepo wabaya katika ulimwengu wa roho.

nje ya hapo, hakika utakuwa mtu wa vita peke yako na hautashinda kwasababu kujifanya unapambana kwa kutumia nguvu zako za kimwili ni abomination, ni kama unasema Mungu hawezi ila wewe ndio unaweza, God has made it available to us all what its needed to have us redeemed katika kila kitu, ameweka mazingira yoote ya kutufanya tushinde, hata majaribu halijawahi kula lile lililo nje ya uwezo wako, sasa unapoacha channel ambazo Mungu amekuelekeza ufuate ili ushinde ukaanza kupambana kwa nguvu zako mwenyewe hautashinda na ni dharau kwa Mungu. mbarikiwe.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…