Heko Usalama wa Taifa

uumhh, mwandishi happiness angeweka bayana yale ambayo yeye anawasifia hawa jamaa au kwa sababu siku hizi hakuna vile vifungo vya nyumbani au kubebwa na kupelekwa kusikojulikana kama tu ukiisema vibaye serikali?

kakuambia nani akuna vifungo vya om au kuwekwa kizuizini we ropoka uone ndo utajua
 
Hii idara inariport wapi serikalini? nisaidieni? - na nani ni bosi wao kwa serikali yate ya sasa?
 
Hawa jamaa wana mchango wao mkubwa tu kwenye AMANI na UTULIVU tuliyonayo Watanzania. Tunaweza kubishana sana kwa hili. Wakubwa wao tu ndio wamekuwa wakiwaunga mkono hata mafisadi wa wazi kabisa.

amani gani hiyo na utulivu gani huo amani ya kuwalinda mafisadi na utulivu wa kuiweka na kuilinda ccm kwa nguvu zote na gharama zote wanakazi ipi ingine wachina wanaingia hovyo na kufanya kilabiashara wageni wanaingia hovyo nakufanya lolote ili mradi tu asiingilie amani na utulivu wa ccm.
kweli hii ndo kai stahiki kwa usalama wa taifa naona wanalitia ata aibu jina lenyewe hope lingebadilishwa
 
Mwandishi wa Tanzania Daima angeeleweka na HEKO zake kama angechambua Usalama wa Taifa kwa miaka yote 40.

Katika intaneti kuna masuala ya Usalama wa Taifa, kushindana na majasusi wa Kireno toka Mozambique, majasusi Weupe wa Rhodesia(Zimbabwe), makaburu (South Africa) n.k n.k ndio maana hata leo hicho kituo cha polisi salender bridge DSM ni kutokana na usalama wa Tanzania kutishiwa na makomandoo majasusi kutaka kulilipua daraja kuiadhiri kisakolojia Tanzania.

Kina Samora Mache, Nujoma, Savimbi, Kabila, Chissano, Che Guevara n.k waliishii Tanzania kwa kutegemea ulinzi wa Usalama wa Taifa, inagawaje mara moja moja kulitokea changamoto kama la Eduardo Mondlane raisi wa kwanza wa Frelimo kuletewa kifurushi cha bomu DSM na kikamlipukia na kuchukua uhai wake.

Pia huko kusini mwa Tanzania, helikopta za mreno zilikuwa zinatua na kuleta kashikashi.

Mbali ya hilo 'vetting' wa viongozi wa umma Tanzania ilikuwa inafanywa kwa uzalendo wa hali ya juu, wazee wetu kabla ya kupewa uongozi sisi watoto barabarani tulikuwa tunaona 'vijana' tusiowajua wakifuatilia mienendo ya wazee wetu vigogo kwa kushinda mtaani na 'gari bovu' geresha ya kusubiri mafundi, mzee akitoka na gari mara 'gari bovu' limepona linawafuata wazee wa umma mienendo yao.

Hivyo kama Usalama wa Taifa bado wanafanya hivyo kwa staili mpya ya 'sayansi na technolojia' basi HEKO, lakini siamini hilo maana mafisadi kibao sana sasa.

Juzi juzi yule mjamaica aliyeleta kasheshe alikatiza toka kusini mwa Tanzania mpaka Tanga na kuingia Kenya, bila Usalama kushugulikia huko kusini mwa Tanzania, labda ndio changamoto hizo.

Hivyo kichwa cha habari kingekuwa 'Usalama wa Taifa wanakabiliwa na Changamoto kubwa''
 
Wajinga kibao mitaani wanatambiana wako usalama wa taifa, kumbe mission town.
 
Hii idara inariport wapi serikalini? nisaidieni? - na nani ni bosi wao kwa serikali yate ya sasa?

Wako ofisi ya raisi chini ya waziri wa utawala bora, Mh. Sophia Simba.
 
mdogo wangu Happiness ameingizwa katika somo ambalo sidhani kama anauwelewa nalo wa kutosha. TISS ilivyo sasa ni aibu kwa vyombo vya usalama wa taifa duniani. Believe me I know.

Ni rahisi sana kumchora simba na kumpaka rangi nzurii akapendeza, pamoja na kufanya hivyo bado akikukuta anga zaki atakutafuna bile kujali kama wewe ni mchoraji wake. Pamoja na mazuri aliyoandika huyu dada hayabadili ule mtazamo wa ubinafsi na kazi ya kutetea maslahi ya wachache inayoyafanywa na TISS . Huenda Happiness ni beneficiary pia.
 
Tuwapongeze kwa yapi? kukiri kwamba EPA ni wazito hawakamatiki?kukiri kwamba mikatapa yote ya kitapeli ni sahihi? huyo kalewa tu.
 
tabu ya TISS ni kuwa ipo kuwalinda wanasiasa tena wa chama tawala basi, daily utasikia mtu anajitamba mimi nipo usalama wa taifa, je tunafaidi na yapi?wageni kibao wanafanya madudu hawaoni hadi wananchi wapige mikeleel ndo unaona serikali inashtuka na kufunika mauozo, hatuna national security dhabiti,hata kidogo, miongozo gani ya kujenga nchi wametoa?au kupeana vyeo tuu?
 
mdogo wangu Happiness ameingizwa katika somo ambalo sidhani kama anauwelewa nalo wa kutosha. TISS ilivyo sasa ni aibu kwa vyombo vya usalama wa taifa duniani. Believe me I know.

tatizo wakiona mada zako mwana k
awafungiii wanahisi wimbo wa taaifa
matokeo wanaimba"kichaga" kama mada isemavyo
hilo ni danguro ndugu-TISS
 
Hawa jamaa wana mchango wao mkubwa tu kwenye AMANI na UTULIVU tuliyonayo Watanzania. Tunaweza kubishana sana kwa hili. Wakubwa wao tu ndio wamekuwa wakiwaunga mkono hata mafisadi wa wazi kabisa.

You could be right. Kuna kauli kwamba wataalamu wa chini katika Idara hiyo hufanya kazi ya uhakika kukusanya ushahidi na kuandika ripoti za uhakika juu ya maovu mbalimbali yanayotokea lakini zinaishia kuwekwa pembeni na mabosi wao wenye malengo tofauti. Maelezo ya aina hii utayasikia sehemu nyingi hata kwenye vyombo vya habari kati ya waandishi na wahariri: wakubwa ndio wanaoamua final output ya taasisi.

Hapo ndipo tunaposema hakuna cha maana kinachotoka Idara hiyo siku hizi zaidi ya kulinda hujuma. Hata huyo mwandishi inaonekana ama yeye au gazeti lake limetishiwa kwa kuandika habari mbofu kuhusu Idara hiyo huko siku za nyuma (kama wadau walivyotuthibitishia hapa) ikabidi "wajisahihishe" kabla rungu halijatua.
 
Hakuna usalama wa Taifa hapa!
Ulibadilishwa na kuwa usalama wa matumbo ya watu fulani fulani tangu mwaka 1977 alipoogopa marehemu Julius Kambarage Nyerere na kuanza kuingiza vijana kwa undugu badala ya kutumia special skills na taaluma matokeo yake watu waliopo KWENYE taasisi hiyo ni zaidi ya pumba na ndio maana mambo hayaendi. Kama Director of intelligence ni chagua la Rostam Aziz sasa tuna usalama gani. Look at Pinda the current Prime Minister ni aibu kwa taifa kujivunia usalama ambao actually haupo. Nawasilisha mwenye munkari na hizo heko akameze wembe tusipotezeane muda. How Could EPA come and go and the Govt. Boys are fast asleep kwa ulevi!!!
 
..usalama wa Taifa wapo pale kuhakikisha kwa CCM inaendelea kutawala.

..binafsi naamini wanafanya kazi nzuri sana ktk kufanikisha lengo lao hilo.

..usalama wa Taifa wamewezesha kufanikiwa kwa hujuma na wizi mkubwa-mkubwa kama EPA bila ya serikali kutetereka.

..binafsi nashawishika kusema kwamba TISS wanajua wanachokifanya, na wametekeleza kwa ufanisi mkubwa jukumu lao la kuhakikisha kwamba CCM inaendelea kudumu madarakani.
 
Jokakuu!
Kama hadidu za rejea ni kulinda CCM itawale for 50 years to come then hawa jamaa wamefanikiwa kwa asilimia miambili then Joka kuu uko sahihi! Ila kama ni Usalama wa Taifa hakuna kitu . Kwa lugha swaswa it is a dead body and long burried hata wakati JKNyerere akiwa madrakani take it easy buddy!
 

Naungana na wewe mkuu. intelligence agency za wenzetu zinajishughulisha kwa kuwezesha nchi zao kupata nation state competitive advantages TISS yetu inakazana kuliangamiza taifa. kila ufisadi unapitishwa kwenye hizo taasis ambazo zilitakiwa kusaidia kuzuia huo uozo.
 
Hamna kitu hapa, kama MKJJ alivyosema Happiness bado hajui usalama wa taifa ni nini.

do I need to describe??
 
Enzi zile za USSR, kulikuwa na watu wanaitwa political commissars. Kazi zao ilikuwa ni kueneza propoganda za mafanikio ya USSR. Hawa jamaa walikuwa na nguvu sana mpaka ndani ya REd Army.

Waliweza kwenda kwenye viwanda visivyofanya kazi, kuwavalisha watu uniform na kupiga picha jinsi USSR ilivyokuwa na maendeleo makubwa. Walienda kwenye mashamba wakapiga picha jinsi USSR ilivyojitahidi katika kuendeleza kilimo kwa wananchi wake. Mara nyingine hayo yote walifanya purposely ili kutufanya watu wengine tuamini mambo ambayo hata hayakuwepo.

Ila bwana kilichowaumbua ni zile foleni za kupata nyama na mkate.

Pengine mwandishi naye alishawahi kuwa political commissar...anajaribu kutuonyesha picha ambayo haipo. Kwa bahati mbaya leo hii kuna freedom of speech kwahiyo watu wanauwzo wa kujiuliza kama haya anayosema yana ukweli. Time will prove her right or wrong. Mimi kwangu naona hizo ni hadithi zisizo na ukweli
 
Usalama wa kwetu ni siasa na majungu kuliko kazi za kiuchunguzi na uhakika. Wangekua mahsusi kwa maudhui ya uwepo wao nchi isingeingizwa kwenye ukwapuaji mkubwa kama wa meremeta, tangold, import support, EPA, richmond na kdha wa kadha bila wao kujua. Na kama walijua wakauchuna basi kazi yao ni pamoja na ...
 
mdogo wangu Happiness ameingizwa katika somo ambalo sidhani kama anauwelewa nalo wa kutosha. TISS ilivyo sasa ni aibu kwa vyombo vya usalama wa taifa duniani. Believe me I know.
Mzee Mwanakijiji nakuunga mkono kwa shingo nyyofu kabisa na kwa 100%.

Hapa Binti wa watu amekweda chaka kabisa kwa kuelezea yale ambayo yapo wazi kwa wengi. Hajui kuwa magezi ya kiuchumi na kisiasa ndiyo yaliyopelekea hitaji la watawala kuona haja za kuimarisha kisiasa zaidi vyombo vya usalama vya kuwalinda na hapo ndipo unakuta hata sheria nyingi zimetungwa kati ya miaka ya 90 na 2000 pengine kuhalalisha au kuzuia masuala fulani yenye maslahi ya watawala.

Nina shaka kuu kama huyu Happiness anajua utendaji wa hicho chombo kwa undani, na sijui kama anajua hiyo sheria inayoanzisha TISS imeleta mafanikio gani kwenye utendaji wa hawa jamaa anaowasifia.Hata hiyo makala yake haibainishi nini wamefanya cha kuweza kuwapongeza hivyo. asingethibutu

Kwa mfano tu angejua huko "field" jamaa (TISS, TAKUKURU, Polisi, JWTZ, Mgambo, JKT, Kampuni binafsi za ulinzi na "personal bodyguards") wanavyogongana kuhangaikia ulaji badala ya kazi asingethubutu kuandika haya.

MUNGU WABARIKI WATANZANIA WASIO IJUA NCHI YAO VIZURI ILI WALIELEWE SOMO WANALOTAKA WENGINE WALIJUE!!.
 
Tanzania haijawahi kuwa na usalama wa taifa hata mwaka mmoja kama wapo basi watakuwa hawajui kazi na maana ya usalama wa taifa ninaweza kusema Tanzania tuna watu wa usalama wa viongozi wa taifa kazi inayoweza kufanywa na jeshi la polisi.

FBI au CIA kwa mfano vina vitengo vya kulinda maslahi ya mataifa yao CIA anaweza kuja kuishi Tanzania kwa muda mrefu tu anaweza kuja kama Mwalimu na ukiangalia wanaokuja wachache sana hufudisha masomo ya maana sana sana watafundisha PE au kwaya ya shule

Wengine huja kujifunza tamaduni zetu lakini hao wote lengo si tamaduni wanapiga mahesabu ni vipi nchi yao itafaidika na kitu gani toka Tanzania madini maliasili nk na kila siku wanapeleka ripoti makao makuu.

Angalia walivyo wepesi kukimbilia sehemu za majanga kama Haiti ni kweli watatoa misaada ya nguvu lakini ujue kuna kitu kinatafutwa kwa manufaa ya nchi zao hao ndio usalama wa taifa.

Tofauti na watu wetu kama nilivyosema tuna watu wa usalama wa viongozi wa taifa mtashinda nao bar mitaani hakuna wanachofanya cha maana hawana plan yeyote zaidi ya kuvizia vimagendo vidogo vidogo na dili za ujambazi ambazo nazo nyingi huwa wanahusishwa nazo utasema huo ni usalama wa taifa sasa polisi afanye nini.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…