Hela za MCC ni makusanyo ya masaa matatu tu kwa TRA

kama unataka kusema hivyo ilitakiwa heading ibadilike na kuwa,"pesa ya MCC ni makusanyo ya TRA kwa masaa 3 kila siku kwa muda wa miaka mitano"
Mkuu sio mm nilie toa mada. Lakin ndivo ilivo. Hivo ndivo unavotakiwa kuelewa. Sio tofaut na hivo. Huo ndo ukweli wa hiyo hela ya MCC
 
Maandishi kibao lakini yamejaa porojo za kishamba sana ! Kwanza Tanzania haikunyimwa hela za MCC tu bali pia IMETIMULIWA ndani ya MCC , lakini pia kunyimwa misaada kwa sababu ya kusigina katiba ni aibu kubwa sana , kingine si kweli kwamba Tanzania inaweza kujitegemea na ndio maana mwandishi anapinga EU kujitoa , sasa kama hela za japan na wachina zinawapa faraja mmejiandaa nini ?
 
ati shs trilioni 1.4 ni makusanyo ya masaa 3 ya TRA? hujui kuwa ni zaidi ya makusanyo ya mwezi mmoja ya kodi ya nchi nzima? mkuu rudi kasome ngumbaru au memkwa.

Ni tr. 1.04 sio 1.4,
just a point of correction mkuu.
Pia inaonekana hukumwelewa aliposema masaa matatu, vipi kama mimi ntakwambia kwamba wakati MCC wanachomoa trilioni 1.04 uwezo wa serikali ya sasa kufidia pengo hilo ni mara 33 utasemaje?
Maana kwa hesabu za wazi ziko hivi:
Kama makusanyo yaliyoongezeka (ambayo hayakutarajiwa) kwa mwezi ni bil 550 hii ina maana pengo hilo litazibika kwa miezi miwili tu kati ya miezi 60 ya matumizi ya fedha hizo na chenji ya bil 960 bila kuathiri wastani wa makusanyo ya serikali ya Kikwete.
Kama pesa za MCC zingeingizwa katika bajeti ya kila mwezi serkali ingelazimika kukusanya bil 17.3kwa mwezi kama kiasi cha kuzibia pengo, hata hivyo kwa hesabu za sasa kiasi hicho kingeweza kukusanywa kwa siku 1 tu nje ya kiasi kilichokadiriwa, yaani fedha ya ziada ambayo inakusanywa kwa siku ni sh. bil 18.3
UMEELEWA?
 
http:// kwako wewe kila alilosrma nyerere ni sahihi haahaa unaabudu akili ya mtu kama wewe .hiyo statement ya nyerere kuhusu coca cola is a false statement . Democrasia ni moja tu alieshinda ndio mshindi .eti unajidai eti demokrasia ina mila zake mara unajidai inadesturi zake mara inautamaduni wake mara unajidai inamatambiko yake acga kudanganya watu .demokrasia ni demokrasia tu .kwa hiyo ili uwe mzalendo ndio unajisi demokrasia .tumezikosa kwa sababu ya utapiamlo wa madarakavya chama kimoja kati ya zaidi ya vyama ishirini
 
Labda isemwe hivi, bajeti ya 16/17 ni tirioni 39.5. kati ya hizo misaada ni titooni 12. hela ya MCC tulionyimwa no trioni 1.4 ndio watu wazima wanavimba shingo ati nchi itayumba.
39-12 unapata 27!
TZ bado inategemea sana misaada ktk bajeti na hatukutakiwa tuipuuze hata Milion 100

Kumbuka na majigambo haya ya serikali hii lkn zaidi ya 30% ya bajeti yetu itategemea kuomba omba!Tungepata hii 1.4 ya bure % ya utegemezi ingeshuka kwa karibia 2%!Hii ni % kubwa sana kwa uchumi wa nchi
 
ati shs trilioni 1.4 ni makusanyo ya masaa 3 ya TRA? hujui kuwa ni zaidi ya makusanyo ya mwezi mmoja ya kodi ya nchi nzima? mkuu rudi kasome ngumbaru au memkwa.
Au kama ni kwa saa ni hivi:
Fidia ya fedha za MCC ni mil. 24 kwa saa,
Lakini fedha ya ziada inayokusanywa kwa dakika 1 mil 12.7 hiyo ina maana fidia ya fedha za MCC inayohitajika kwa saa 1 inafidiwa kwa chini ya dk2, kengele wewe
 
I see katika watu waliomnukuu baba wa taifa vibaya wewe unaongoza, demokrasia aliyokuwa anaisema Nyerere yakutokuamliwa na watu wengine sio hiyo ya kuwadhulumu wananchi walichoamua au kuwa nyima haki wengine kisa hawakubaliani na CCM. Angekuwa na mawazo kama yako ktk demokrasia nadhani mpaka leo tusingekuwa na vyama vingi. Msipindishe mawazo mazuri ya Nyerere kwa kuhalalisha dhuluma zenu.Uchaguzi wa meya wajiji la dsm umechukua miezi zaidi ya mitatu ili kujaribu kupindisha haki iliyo wazi, znz demokrasia inaminywa bado unataka kuhalalisha demokrasi yako ya kipeasant kwa kumnukuu nyerere, Msipotoshe upeo mkubwa aliokuwa nao nyerere kwa mawazo yenu ya mgando kiasi hicho.
 
Ni sawa na kusema
Baada ya MCC kuchomoa trl 1.04 shirika la Kitanzania liitwalo TM limejibu kwa kuipa Tanzania sh. tr 33 karibu mara 33 ya msaada wa MCC ulioondolewa.
Ndicho kiilichotokea ndugu
 
na katika hio makusanyo ya mwezi tr. 1.3, je vipi matumizi ya mwezi ya serikali yanalipwa kutoka wapi?
 
Tuweke hivi,kwenye makadirio ya bajeti,matumizi ya kawaida ya serikali yamezidi makusanyo ya TRA.Miradi ya maendeleo itategemea misaada na mikopo!Tunashabikia nin hapa?
Bajeti trilion 29
pesa itakayokusanywa makadirio max ni trilion 17
matumizi ya kawaida ni trilion 17.8
mikopo na msaada trilion 12

hapo tunachekelea nn
 
Hatuchekelei ila ukweli usipindishwe.

Mimi pia nakubaliana na wanaosema bado tunahitaji misaada ili kufikia hatua ya kujitegemea bila kuombaomba, ila ukweli wa hesabu ndio huo
 
Sijui kwa nini Humphrey anajitia UJUHA namna hii...
Ni kwa nini ccm walikubali mchezo huu wa siasa za "demokrasia" ikiwa hawataki demokrasia ktk chaguzi zetu...?!
Ni kama vile, wao CCM ndio "alfa na omega" ktk siasa za nchi hii.... Wanatumia Mahakama watakavyo, ndio maana walitaka kutakatisha uhalifu wao wa kufuta uchaguzi wa Zanzibar, kwa kuwashawishi CUF waende Mahakamani huku wakijua walishamaliza kila kitu huko...
Kama vyombo vya kisheria kweli vipo Zanzibar, kwa nini hawachukui hatua kwa vijana wake wanaochochea ubaguzi ktk maskani ya kisonge...?!
Ya nini kutunga sheria za kudhibiti wahalifu wa mitandaoni wakati hawa walio wazi kabisa mchana kweupe wanaopita na mabango ya uchochezi wao wanasindikizwa na Polisi wasibugudhiwe....?!
MCC si kwa ajili ya nyie ccm kupata fedha tuu, ni kwa ajili pia ya kuonyesha mnawatendea WANANCHI kwa HAKI kama mlivyokubaliana na MCC...
Sasa mmeshindwa masharti, mnaanza kusema "HATUZITAKI MBICHI HIZI"....
Hii ni aibu yenu peke yenu ccm...., haituhusu sisi wananchi.., Pole pole acha porojo zako...!
 
kinachofanywa na ccm ni kualalisha wakati ukifika wa kulipa kisasi watu wasiwe na huruma na lolote litakalokuwa linafanyika yaani itakuwa kama vike mtu anavyoua nyoka. mwenye masikio na asikie
 
Habari imejaa upotoshaji sana. Nilifikiria numjibu hapa au kwingineko.

Kipande nilichonukuu kama sikosei kinaonyesha katibu msaidizi idara ya uenezi.
Kwa muda mrefu huyu bwana amejitambulisha kama mwananchi na Raia.

Hata 'alipobwanwa' hakuwahi kusema nyadhifa zake ndani ya chama.

Huyu alikuwa mjumbe wa tume ya Warioba, tunaona kwanini maoni ya tume yalishindwa kwa kuwa na ''double agent''

Hata hivyo, nimpe kionjo kidogo. Kumnukuu Mwlalimu Nyerere kibubusa ni matusi

Nyerere aliposema hayo alimaanisha demokrasia tunayoikubali wenyewe ndiyo ituongoze.Nyerere hakusema uhuni wa demokrasia ndio uongoze

Pili, anasema Marekani haijaonyesha kifungu cha katiba ya ZNZ kilichokiukwa

Huyu bwana ameshaulizwa, ni kifungu gani kilichompa Jecha mamlaka ya kufuta uchaguzi?Hakuwahi kuonuesha hata siku moja

Huyu bw hajaonyesha ni kifungu gani cha sheria kinachozungumzia uchaguzi wa marudio katika katiba ya SMZ? Hajawahi kuonyesha hata siku moja

Mwandishi anawatuhumu Marekani kuingilia mambo ya ndani.

Hatuelezi kwanini Rais JK akiwa mwenyekiti wa CCM pia alifanya safari za kwenda kusaini mikataba Washington

Hivi nani alishinikiza, sisi tuliokwenda au walioweka masharti tukayafuata?

Rais Magufuli yupo katika rekodi akisema MCC ina manufaa.

Mwandishi atueleze lini Rais alifuata kauli hiyo na kama hajafuta, mwandishi anataka kutueleza nini kuhusu serikali iliyopo madarakani?

Polepole yupo katika rekodi akisema Taifa letu linaongozwa kwa viongozi kuwa waongo. Pengine alijua siri hiyo maana yale ya sisi kuishi kama Taifa la waongo yanaonekana wazi katika bandiko lake

Hoja zake hazinisumbui, kinachonisumbua ni kuona vijana wadogo wa umri kama huu wanapoingia katika siasa za kulihadaa Taifa. Kwamba tunaishi kama Taifa la waongo, na uongo sasa ni fani. Kwamba, hatuwezi kuweka mkate mezani hadi tutunge uongo

Taifa hili lina safari ndefu, kuondoa umasikini, maradhi , ujinga na kizazi cha waongo
 
na katika hio makusanyo ya mwezi tr. 1.3, je vipi matumizi ya mwezi ya serikali yanalipwa kutoka wapi?
Statistically we do not save anything!
Mishahara tu inakula karibia nusu ya makusanyo haya,bado mgao wa ZNZ na malipo ya nishati kwa wizara za serikali na taasisi zake

Ukiweka hapo na huduma ya majeshi yetu utaona bado tunahitaji tuongeze nguvu ya kukusanya au tukope kwa "wakubwa" ambao leo tunawaita majina yasiyofaa
 
Nadhani watu wengi pamoja na wewe haujaelewa hiyo pesa ya MCC hutolewa kwa miaka 5 na sio kila mwezi. Hesabu halisi the ni takriban 1.04 Trillion na sio 1.4 mkuu. Hiyo pesa kwa mwaka 1 ni 208Bil. Ni Sawa na bil 17.3 kwa mwezi, kwa wiki ni bil 4.3. Hivyo sio pesa nyingi sana ya katisha kwa serikali kama tunavyoaminishwa. Usinielewe kuwa namaanisha hatuhitaji hiyo pesa, HAPANA. Kila shilingi ni muhimu kuipata kuliko kukosa hata kama ingekuwa mil 1 kwa mwezi maana kuna kazi itafanya. Ila nataka tu tuelewe sio pesa nyingi kiivyo.
 
Lo! Mada yako imekaa vizuri, imeeleweka na umeipangilia vema, nami nakuunga mkono 1% kwa sababu haiwezekani jasho tunalohenyekea kukusanya kwa mwezi unalidharau kwamba linaweza kukusanywa kwa masaa, hapo umeongopa au hesabu haipandi. Hata ukiwatumia Al-Shaabab, Boko Haram, Taleban, Islamic State, Al Qaida, Ant Baraka n.k huwezi kuikusanya trilioni 1.4 kwa masaa matatu, never.

Mimi binafsi kunyimwa msaada wa 1.04 trilioni hakunitishi chochote, kinachonitisha ni aina ya siasa na demokrasia tuliyoamua kufuata kuhusu Zanzibar.
 
Mkuu ume tumia neno BURE
Ktk hii dunia BURE ni ghali sanaaaa tu.Nyara za inchi ndio zimewekwa RUHANI Na hiyo BURE
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…