TANZIA Helikopta yaanguka, aliyekuwa Mbunge wa Ludewa, Deo Filikunjombe na wengine wapoteza maisha!

Hii nchi pengine tumepata bahati mbaya sana! Kwa kweli tupo kwenye nchi ya aina yake "live at your own risk"

Naikumbuka ajali ya MV Skargit na MV Spice Islander! Ungekuwa makini tunaweza kuokoa watu wengi tu wakiwa hai! Nakumbuka matukio ya mafuriko! Nilichokishuhudia ni 'tweets' za watu wenye dhamana walioendelea kutoa 'updates'

Tukio la ajali ya helikopta huko Selous kando ya mto Ruaha viongozi waandamizi wa serikali wanapishana kauli kwa 'tweets'! Huyu ana-tweet hivi na yule ana-tweet vile! Wahanga wamebaki mbugani zaidi ya saa12! Tupo serious kweli?

Kama baadhi ya maelekezo yangetiliwa maana ni pengine tungesema mengine kuhusu marehemu Deo (dah inauma sana kumuita Deo marehemu)

Wapo wanasema hiyo ni mipango ya Mungu! Lakini Mungu huyuhuyu katupa uwezo wa kutumia akili na muda kupambana na majanga!
We have to act actively pale tatizo linapotokea! Tumepewa uwezo wa kutetea uhai pale tatizo linapotokea! Anapokuja kiongozi na kuanza kutoa 'tweets' za ajabu ajabu huku wahanga wakiwa kwenye sintofahamu kwa zaidi ya saa 12 hilo halikubaliki kamwe! Tunawapa dhamana muelewe kuwa mna majukumu!
 
R.I.P, pole wafiwa.

Mwigulu alikuwepo??
 
January kafanya ujinga wa kutisha. Tulithamini sana mchango wa Mh Deo kwa Taifa hili na hivyo tulihitaji kujua hali ya usalama wake. Kitoto hiki cha mzee Makamba kikawa kinafanya mzaha na upuzi ka huo bila kujali kabisa Mh Filikunjonbe hakuwa mpuuzi ka yeye au watu wenye tabia kama zake. Inasikitisha sana.
 
Duh! Ama kweli mungu hapangiwi,tumekuomba uwanusuru hawa watoto wako lakini sivyo ulivyopenda!mapenzi yako yatimizwe
 
Ukawa Sasa Njia Yetu Ni Nyeupee! Mwendo Wa Kupita Bila Kupingwa!!! Bwana Ametoa, Bwana Ametwaa. Na Pia Tunataraji Kuitwaa Ikulu Oct 25 Na Mh Ngoyai.
 
Walitakiwa wawepo wale bingwa wa matusi..

Mungu hapendi kutuchukuwa tungali na madhambi yetu anatuacha tutubu kwanza Ndg Deo kazi ameimaliza amekaza mwendo kuifikia mji wa ahadi sisi tuliobaki tukeshe tukiomba kwa vile hatuijui siku wala saa mwana wa Adamu atakapo kuja kuchukua kilicho chake.
 
It is so sad and honestly I can feel pain. In Deo Filikunjombe we remain united as a nation. It is a very big loss to this nation. He was young, committed, patriotic, reasonable guy with whom one could count on from a few remaining upright CCM members. We pray God to bless him plenty and decide his destiny according to what he did to this beloved country of ours. RIP Deo.
 
Mkuu Inaweza Ikawa Lakini Mimi Sishangai Mkapa,nape,msukuma,bulembo Wanavoongea Wanavotaka Wamejipanga Kwa Huu Mchezo,na Ndo Mana Nahisi Wakina Mnyika Wamejiweka Pembeni,hii Mechi Bado Mbichi Hii #kikwete Vs #lowassa.......!!

Huwezi kumtenganisha mwana CCM na imani za kishirikina.. Tayari wameshaanza kuamini uchawi katika haya as if akina Kombani na Kigoda hawakuwa wagonjwa..
 
ccm lazima iishiwe pumzi kwa maelezo ya makamba ambaye ndiye mshauri wa ccm juma mwapachu alikuwa na kila sababu ya kuondoka ccm!!
 
Rest In Peace wote waliokumbwa na maafa na pole kwa ndugu wote waliofikwa na mkasa huo.
 
Mwangalie huyu nae ,sasa sijui huo uchunguzi majibu yametoka saa ngapi na sijui kama yeye ndie aliyepaswa kutoa hizi taarifa ,ndio shida ya viongozi wetu kuingilia kazi za mihimili mingine bila kupima kauli zao za kisiasa zinaathiri vipi wanachi
Kuwaokoa tu mmechukua takribani masaa kumi na ushee ila majibu ya uchunguzi ushayapata the moment chopper ilipo onekana khaa mnasikitisha
 
Msiba wa pili wa wana ludewa baada ya ule wa Mtikila RIP Kamanda
 
Bora wangu hakugombea maana SI kufa huku duu,poleni wafiwa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…