poleni na majukumu wanaJF kwanza kama hapa sio jukwaa sahihi mods naomba mnisaidie, nimeona kwenye gazeti la nipashe kona ya matangazo madogo madogo kama unatafuta dawa ya kumrudisha mume,mke au mpenzi,dawa ya mvuto,kupandishwa cheo kazini na kadhalika. yale matangazo huwa ni mengi ukurasa mzima sasa nikachukua namba moja wapo nikapiga jamaa akafanikiwa kuniconvince kuna dawa atanipa ya kunifanya niheshimike kazini na niwe na mvuto bei ni 60,000 nikamwambia nina 40,000 akasema poa nyingine nitamalizia baada ya kuona matokeo. sasa masharti yake naona siyaelewi mara nikioga nayo nimpigie simu ili aniunganishe na maruhani yake mara nichukue hela nyingine niweke kwenye maji yenye hiyo dawa,etc sasa sitaki tena hii mambo JE NAWEZA KUPOTEZEA TU AU NITAPATA MADHARA? am just worried what will happen nikiendelea kufanya mambo yangu,ananipigia simu kila saa sipokei. nisaidieni mawazo wadau