SoC02 Heri kubaki na afya njema kuliko kutafuta matibabu bora

SoC02 Heri kubaki na afya njema kuliko kutafuta matibabu bora

Stories of Change - 2022 Competition

zephania5

JF-Expert Member
Joined
Aug 18, 2022
Posts
232
Reaction score
807

Awali ya yote, nipende kumshukuru Mungu mwenyezi atupae uhai na uzima bure, pamoja na afya kwa wana jamii forum wote. Afya njema iko juu ya mali na utajiri. Afya bora ni zaidi ya umaridadi au umashuhuri, na tena afya ni zaidi ya kutokuwa na ugonjwa. Zipo tafsiri mbalimbali juu ya afya ikiwemo ile ya shirika la afya duniani(WHO) ya mwaka 1948 inayosema '' Afya ni hali ya ustawi wa kimwili, kiakili, kijamii na sio tu hali ya kutokuwa na ugonjwa au udhaifu wa kimwili na kiakili''. Afya ni zaidi ya kutokuwa na ulemavu. Afya njema humweka mtu mbali na magonjwa au maambukizi, pamoja na athari zinazoletwa na magonjwa. '' Nilipokuwa kijana mimi na afya tulitafuta pesa, na sasa nimezeeka, mimi na pesa tunaitafuta afya'' Aliwahi kusema mzee mmoja. Ni kweli kuwa umaskini kwa kiasi.
kikubwa humweka mtu katika athari ya kuwa afya mbaya, lakini pia tusisahau kuwa, magonjwa humaliza pesa. Watu wengi huithamini afya na kuitilia maanani pale ugonjwa unapokuja. Afya njema huleta furaha, lakini magonjwa huleta karaha. Ni heri kubaki na afya njema, kuliko kutafuta matibabu bora.

Karne ya 21 na fya
infectious-disease-researcher-lab-test-petri-microscope.jpg
Professor Karl Kuchler is new Chief Editor of Infectious Diseases specialty in Frontiers in Microbiology - Science & research news | Frontiers Tafiti nyingi leo zinafanyika kutokana uwepo wa magonjwa mbalimbali miongoni mwa binadamu, pamoja na uwezekano wa mlipuko wa magonjwa mapya katika miongo ya hivi karibuni. Dawa nyingi zinatengenezwa kutokana na wimbi la uwepo wa magonjwa. Madaktari na wataalamu mbalimbali wa afya wanaongezeka, kutokana na ongezeko la wagonjwa , maana mgonjwa mara nyingi ndiye anayemwona daktari.

Kila kitu tunachokifanya kina athari juu ya afya zetu, ikiwa ni athari ya moja kwa
moja au isiyo ya moja kwa moja. Kila kitu tunachokula kina athari ndani ya miili
yetu, mara nyingi afya zetu zinaathiriwa na chaguzi za kila siku yaani ule nini, unywe nini ama ufanye nini! Kwa miaka ya hivi karibu katika zilizoendelea pamoja na nchi zinazoendelea mazingira yanayotuzunguka yamegeuka kuwa adui kwa afya ya binadamu. Julai 18 2022, homa ya mgunda(Leptospirosis) ikathibitishwa rasmi kimaabara hapa nchini Tanzania, chini ya wizara ya Afya.

Chanzo hasa ikiwa ni mwingiliano wa maji pamoja na mkojo, kinyesi kutoka kwa wanyama wa kufugwa na wanyama pori. Usalama juu ya afya ya binadamu umekuwa ni mdogo sana, maana hata binadamu wanaomzunguka nao kwa kiasi kikubwa husababisha magonjwa na kudhoofisha afya pia. Magonjwa kama kifua kikuu(TB), pumu na homa ya ini( Hepatitis B) ni moja ya magonjwa yanayoweza kuambukizwa kwa kasi kutoka mtu mmoja kwenda kwa mtu.

Mwingine kupitia njia ya hewa pamoja na kugusana. Magonjwa mengi yanayohusiana na mfumo wa upumuaji kama saratani ya mapafu, yanachangiwa pia na wimbi la ongezeko la ongezeko la vyombo vya usafiri kama.

Magari, pikipiki, na treni au magari moshi vinavyotoa hewa chafu na kuharibu anga hewa. Ongezeko la viwanda na maendeleo ya sayansi na teknolojia, yamekuwa na manufaa kwa maisha ya kila siku kwa mwanadamu, lakini kwa upande mwingine yamekuwa na madhara makubwa katika uchafuzi wa vyanzo vya maji, uchafuzi wa ardhi, uchafuzi wa angahewa pamoja uharibifu wa mimea, na hivyo kuhatarisha afya
ya binadamu kwa namna moja au nyingine.

Inawezekanaje kuwa mwenye afya njema?
black_man_worried_shutterstock_15297313-615x345-1.jpg
Huu ndiyo Ugonjwa Utokanao na Msongo wa Mawazo Katika karne hii, inaonekana kana kwamba ni rahisi kupata magonjwa au maambukizi kuliko kuendelelea kubaki mwenye afya njema, maana hata madaktari na wataalamu wengine wa afya huugua pia. Maambukizi na vifo vingi hutokea pia hospitali, na kwenye vituo mbalimbali vya afya.

Kwa kiasi kikubwa afya ya mwanadamu
huatambatana na dhana ya kwamba: nini anapaswa kufanya na nini hapaswi kufanya ili aendelee kuwa mwenye afya njema, pia ni nini anapaswa kula au kunywa, na ni nini hatakiwi kula au kunywa ili awe salama katika afya yake. Yapo mambo kadha wa kadha yanayoweza kumsaidia binadamu kuepuka kutembelea vituo vya afya, au
kumuona daktari mara kwa mara, maana kinga ni bora kuliko tiba.

1.Chakula bora chenye afya njema.
HealthyFood_248929619.png


Eating healthy during a pandemic

Si kila kinachoingia tumboni kinafaa kwa matumizi ya chakula, na kukidhi mahitaji ya mwili wa mwanadamu. Mfano, takwimu zinaonesha kuwa kiwango kikubwa cha matumizi ya soda huchangia 22% ya ugonjwa wa kisukari. Chakula bora ni kile kinachodumisha afya ya mwili na kumkinga dhidi ya magonjwa. Chakula kinatakiwa
kitumiwe katika kiwango sahihi, kulingana na uhitaji wa mtu( kazi, umri, hali ya hewa, uzito, muda, hali ya kiafya ya mtu kwa ujumla). Waeskimo wanaopatikana Alaska hutumia samaki katika kipindi kirefu cha maisha yao, lakini mara nyingi hukumbwa na madhara yanayotokana na ukosefu wa matunda pamoja na mboga mboga. Kufikia mwaka 2013 taarifa kutoka katika shirika la chakula duniani yaani FAO, ilionekana kuwa takribani asilimia 70 ya magonjwa yanayotokea katika miongo.
kadhaa ya hivi karibuni, yametokana hasa na matumizi ya wanyama kama sehemu ya mlo, pamoja na mwingiliano wa magonjwa ya binadamu pamoja na magonjwa ya wanyama.

Matumizi ya vyakula vilivyosindikwa viwandani hasa vile vyenye sukari nyingi, rangi, mafuta mengi, pamoja na kemikali mbalimbali kwa ajili ya kuongeza ladha au kuvihifadhi vidumu kwa muda mrefu, vinapendwa sana na wengi na vinazidi
kuongezeka siku kwa siku, na hivyo inaonekana ni vigumu kuepuka matumizi yake, lakini si rafiki kwa afya.

Ukweli usiopingika ni kuwa, vyakula vinavyotokana na nafaka halisi, jamii ya mikunde, matunda, na mboga za majani ni vyakula bora miongoni mwa makundi mbalimbali ya vyakula, sababu zifuatazo:

a. Huwa na virutubisho vyote vinavyopatikana kwenye vyakula vingine kama nyama.

b. Huwa na sifa ya uponyaji, kwa kuwa vina antioksidanti au viondoa sumu kwa baadhi ya vitamini pamoja na madini.

c. Ni vyakula ambavyo havina madhara vikitumiwa katika ubora wake. Lakini zaidi ni kwamba hupatikana kwa urahisi.

Kwa miaka miaka mingi vyakula hivi vimechukuliwa kama vyakula vya watu duni, lakini badala yake vimekuwa na manufaa mengi, ambayo hudhibiti gharama kwa ajili ya matibabu yanayotokana na athari za upungufu wa vyakula hivi.

Kwa karne nyingi zilizopita chakula kama kabeji imekuwa ikitumika kama kinga dhidi ya saratani, ikiwemo pamoja na uvimbe wa saratani. Wagiriki waliipenda pamoja watu walioishi zama za utawala wa warumi kama akina Hipokreti, Galemi pamoja na Diopokrati.

waliithamini kwa kuwa iliwasaidia warumi kukaa kipindi kirefu bila ya kutumia dawa.
Ikiwa unapenda vyakula vitamu kama peremende, chokoleti, sukari, keki pamoja na soda ambavyo vingekuletea madhara mbalimbali kama ongezeko la uzito, ongezeko la sukari mwilini, shinikizo la juu la damu, matatizo ya kusahau, wasiwasi pamoja na msongo wa mawazo, badala yake unaweza kutumia vyakula kama asali mbichi, ndizi, viazi vitamu, mchanganyiko wa juisi mbali mbali kutoka kwenye matunda na mboga za majani kama brokoli, spinachi, karoti, nanasi, tikitimaji, zabibu, embe, tende, miwa, humpa mtu ladha maridhawa pamoja na afya mathubuti.

Tunda aina ya tofaa(Apple) hujulikana kama malkia wa matunda kwa kuwa ni tunda tamu na lenye faida nyingi ndani ya mwili kama vile, kudhibiti tatizo la kukosa choo, shinikizo la juu la damu, saratani ya utumbo mpana, sukari yake pia huwafaa hata wenye tatizo la kisukari.

1. Mazoezi na shughuli za mwili
Exercise-for-different-age.jpg
https://1stnews.com/exercise-for-different-age/
Gari huwa haliwekewi mafuta ili liendele tu kukaa kituoni, bali limpeleke
anaeliendelesha pale anapohitaji kufika. Vile vile mwili wa binadamu hauwezi tu
kulishwa chakula na kukaa bila ya kufanya chochote, badala yake chakula hicho kinaweza kugeuka sumu, hasa kisipotumiwa pasipo utaratibu maalumu. Kukaa siku saba bila ya kufanya mazoezi huufanya mwili kuwa dhaifu.

Tafiti zinaonyesha kuwa, mlo kamili pamoja na mazoezi hupunguza uwezekano wa kupata saratani kwa 30%. Asilimia kubwa ya vijana kwa wazee hawajihusishi na shughuli za mazoezi badala yake muda mwingi hutumika kwenye runinga, mitandao ya kijamii pamoja na kazi za kukaa kama zile za maofisini. Mazoezi humkinga mtu na uzito kupita kiasi, matatizo ya moyo, huboresha mfumo wa uzazi pamoja na kuweka vichocheo vya mwili yaani homoni katika uwiano mzuri, mazoezi huboresha mzunguko wa usingizi, mazoezi huongeza homoni za furaha kama vile dopamaini na noradrenalini, zinazosaidia kuondokana na msongo wa mawazo, wasiwasi pamoja na sononeko.

3. Mahusiano mazuri ya jamii.
shutterstock_1038614926_web.jpg
4 Benefits of Healthy Relationships - Acenda Afya ya akili pamoja na mtindo wa maisha huathiriwa sana na mahusiano baina ya mtu na jamii anayoishi. Mahusiano mazuri humwepusha mtu dhidi ya msongo wa mawazo na chaguzi mbaya za maisha. Taarifa kutoka shirika la afya duniani(WHO), kufikia Januari 2017, takribani watu milioni 350 duniani walikuwa wameathiriwa na msongo wa mawazo. Msongo wa mawazo mara nyingi hutokana na hali tofauti tofauti
za kimaisha kama uchumi na mahusiano. Hali hii husababisha kinga za mwili kushuka, kukosa hamu ya kula, kukosa usingizi, upungufu wa nguvu za kiume, kutojihusisha na shughuli za mwili pamoja na mazoezi, na hivyo kumfanya mtu kupata magonjwa na maambukizi kwa urahisi.
4. Kiasi
Kila kitu kinatakiwa kifanyike au kutumiwa kwa kiasi hata kama ni kizuri ndani ya mwili, mwili ulitengenezwa.

kwa mifumo inayofanya kazi kwa utaratibu maalumu, mahitaji ya mwili yanapopungua au kuzidi, mwili huwa haufanyi kazi kama inavyotakiwa, mazoezi yafanyike kwa kiasi kulingana na mahitaji au hali ya mtu, kadhalika vilevile kwa chakula, hewa safi, muda wa kulala, muda wa kufanya kazi, muda wa kupumzika, vyote vinatakiwa vizingatiwe katika utaratibu wake.

Vile vile zipo njia zingine kadha wa kadha, zitakazoweza kusaidia kupunguza idadi ya wagonjwa pamoja na maambukizi ya magonjwa katika karne yetu, kama vile kudumisha usafi na utunzaji wa mazingira, kuwa na sera nzuri kuhusu afya na inayotekelezwa na watu wote, elimu ya afya kwa jamii kusisitizwa kupitia vyombo vya habari kama vile runinga, redio, magazeti, majarida pamoja na mitandao ya kijamii, matumizi ya maji safi na salama, kujihusisha na shughuli za ibada kama vile kuimba na kuabudu. Kutembelea vituo vya afya kwa ajili ya kupima maendeleo ya afya ya mwili kama vile shinikizo la damu, kiwango cha sukari mwilini, kiwango cha oksijeni mwilini, pamoja uwezekano wa maambukizi ya magonjwa yanayoweza kutokana na virusi, bakteria pamoja na fangasi, kwa ajili ya kuchukua tahadhari, ushauri nasaha. Salia na afya njema.
 

Attachments

  • images(20).jpeg
    images(20).jpeg
    8.7 KB · Views: 48
  • IMG-20220712-WA0003.jpg
    IMG-20220712-WA0003.jpg
    19.2 KB · Views: 43
  • Exercise-for-different-age.jpg
    Exercise-for-different-age.jpg
    24.5 KB · Views: 51
Upvote 225
Hivi wewe mureta mada kuna mambo hayaepukiki bana weeee!! kabisaa na hakuna asiye penda afya bora kila mutu anataka lkn je utakwepa ajali weye na gari unaendesha kila siku kwani waliopata wapenda??
Afya bora ni zaidi ya kutokuwa na ulemavu, na ulemavu si ugonjwa, japo unaweza kusababisha mtu kupata magonjwa mengine kama msongo wa mawazo na mengineyo. Na hapa yamezungumziwa magonjwa hasa yanayotokana na mtindo wa maisha
 
utayaacha?!! dawa za Hospital x-ray zenu hizo, ni makemikali matupu tena bora utumie dawa za DR mwaka! Pc kompyuta mapakato unayotumia mwanga wake ni hatari kwa korodani zako unalijua hiloo!

Moshi unaovuta ukiwa barabarani waweza kukupa utasa na kuzaa vitoto vichaa unajua ivo,...majii ya baridi unayotumia yananyonya spinal cord fluids...y
Kinga ni bora kuliko tiba, hapa tunaangalia zaidi jinsi ya kupunguza risk ama athari, sababu huwezi kuwa salama kwa 100%. Magonjwa mengine ni ya kurithi, umasikini wa kukosa huduma bora na za msingi, kama mlo kamili, maji safi na salama vile vile hupelekea magonjwa. Kuwa na ufahamu na elimu itasaidia kuepuka magonjwa ambayo si ya lazima, sababu hata madaktari huugua. Lakini kuwa na ufahamu kunapunguza athari za kupata magonjwa
 
Kinga ni bora kuliko tiba, hapa tunaangalia zaidi jinsi ya kupunguza risk ama athari, sababu huwezi kuwa salama kwa 100%. Magonjwa mengine ni ya kurithi, umasikini wa kukosa huduma bora na za msingi, kama mlo kamili, maji safi na salama vile vile hupelekea magonjwa. Kuwa na ufahamu na elimu itasaidia kuepuka magonjwa ambayo si ya lazima, sababu hata madaktari huugua. Lakini kuwa na ufahamu kunapunguza athari za kupata magonjwa
Chifu umemjibu kisomi sana.

Shukrani Kaka kwa ujumbe safi sana.
 
Nachagua wapi lini nini cha kujifunza!
Ni heri kuuliza mahali ambapo haukuelewa ama ulipata utata. Tatizo wengi tunasoma ili tupate cha kujibu na si kuelewa zaidi
 
Ni heri kuuliza mahali ambapo haukuelewa ama ulipata utata. Tatizo wengi tunasoma ili tupate cha kujibu na si kuelewa zaidi
Ni Makosa ya kiutendaji kumuuliza kipofu njia!
 
kuhusu makala ya afya yangepewa nafasi yake yakipekee kwasasbu ni kitu ambacho kila mtu anahitaji kimsaidie kwenye shughuli zake bila afya akuna kitu unaweza fanya kivyovyote vile asante sana kaka
 
kuhusu makala ya afya yangepewa nafasi yake yakipekee kwasasbu ni kitu ambacho kila mtu anahitaji kimsaidie kwenye shughuli zake bila afya akuna kitu unaweza fanya kivyovyote vile asante sana kaka
Ni kweli kabisa. Maana mara nyingi binadamu anapoamka huwaza juu ya hali yake ya kimaisha siku hiyo itakwendaje(fedha, ndoa na mengineyo), huku akiweka kando juu ya suala la afya siku hiyo litakwendaje. Bila afya hakuna shughuli za maendeleo zitakazosonga mbele, hakuna furaha katika ndoa ama mahusiano, bila afya hakuna ufaulu katika masomo. Ahsante pia kwa maoni yako.
 
View attachment 2343272
Awali ya yote, nipende kumshukuru Mungu mwenyezi atupae uhai na uzima bure, pamoja na afya kwa wana jamii forum wote. Afya njema iko juu ya mali na utajiri. Afya bora ni zaidi ya umaridadi au umashuhuri, na tena afya ni zaidi ya kutokuwa na ugonjwa. Zipo tafsiri mbalimbali juu ya afya ikiwemo ile ya shirika la afya duniani(WHO) ya mwaka 1948 inayosema '' Afya ni hali ya ustawi wa kimwili, kiakili, kijamii na sio tu hali ya kutokuwa na ugonjwa au udhaifu wa kimwili na kiakili''. Afya ni zaidi ya kutokuwa na ulemavu. Afya njema humweka mtu mbali na magonjwa au maambukizi, pamoja na athari zinazoletwa na magonjwa. '' Nilipokuwa kijana mimi na afya tulitafuta pesa, na sasa nimezeeka, mimi na pesa tunaitafuta afya'' Aliwahi kusema mzee mmoja. Ni kweli kuwa umaskini kwa kiasi.
kikubwa humweka mtu katika athari ya kuwa afya mbaya, lakini pia tusisahau kuwa, magonjwa humaliza pesa. Watu wengi huithamini afya na kuitilia maanani pale ugonjwa unapokuja. Afya njema huleta furaha, lakini magonjwa huleta karaha. Ni heri kubaki na afya njema, kuliko kutafuta matibabu bora.

Karne ya 21 na fya View attachment 2343283Professor Karl Kuchler is new Chief Editor of Infectious Diseases specialty in Frontiers in Microbiology - Science & research news | Frontiers Tafiti nyingi leo zinafanyika kutokana uwepo wa magonjwa mbalimbali miongoni mwa binadamu, pamoja na uwezekano wa mlipuko wa magonjwa mapya katika miongo ya hivi karibuni. Dawa nyingi zinatengenezwa kutokana na wimbi la uwepo wa magonjwa. Madaktari na wataalamu mbalimbali wa afya wanaongezeka, kutokana na ongezeko la wagonjwa , maana mgonjwa mara nyingi ndiye anayemwona daktari.

Kila kitu tunachokifanya kina athari juu ya afya zetu, ikiwa ni athari ya moja kwa
moja au isiyo ya moja kwa moja. Kila kitu tunachokula kina athari ndani ya miili
yetu, mara nyingi afya zetu zinaathiriwa na chaguzi za kila siku yaani ule nini, unywe nini ama ufanye nini! Kwa miaka ya hivi karibu katika zilizoendelea pamoja na nchi zinazoendelea mazingira yanayotuzunguka yamegeuka kuwa adui kwa afya ya binadamu. Julai 18 2022, homa ya mgunda(Leptospirosis) ikathibitishwa rasmi kimaabara hapa nchini Tanzania, chini ya wizara ya Afya.

Chanzo hasa ikiwa ni mwingiliano wa maji pamoja na mkojo, kinyesi kutoka kwa wanyama wa kufugwa na wanyama pori. Usalama juu ya afya ya binadamu umekuwa ni mdogo sana, maana hata binadamu wanaomzunguka nao kwa kiasi kikubwa husababisha magonjwa na kudhoofisha afya pia. Magonjwa kama kifua kikuu(TB), pumu na homa ya ini( Hepatitis B) ni moja ya magonjwa yanayoweza kuambukizwa kwa kasi kutoka mtu mmoja kwenda kwa mtu.

Mwingine kupitia njia ya hewa pamoja na kugusana. Magonjwa mengi yanayohusiana na mfumo wa upumuaji kama saratani ya mapafu, yanachangiwa pia na wimbi la ongezeko la ongezeko la vyombo vya usafiri kama.

Magari, pikipiki, na treni au magari moshi vinavyotoa hewa chafu na kuharibu anga hewa. Ongezeko la viwanda na maendeleo ya sayansi na teknolojia, yamekuwa na manufaa kwa maisha ya kila siku kwa mwanadamu, lakini kwa upande mwingine yamekuwa na madhara makubwa katika uchafuzi wa vyanzo vya maji, uchafuzi wa ardhi, uchafuzi wa angahewa pamoja uharibifu wa mimea, na hivyo kuhatarisha afya
ya binadamu kwa namna moja au nyingine.

Inawezekanaje kuwa mwenye afya njema?
View attachment 2343151Huu ndiyo Ugonjwa Utokanao na Msongo wa Mawazo Katika karne hii, inaonekana kana kwamba ni rahisi kupata magonjwa au maambukizi kuliko kuendelelea kubaki mwenye afya njema, maana hata madaktari na wataalamu wengine wa afya huugua pia. Maambukizi na vifo vingi hutokea pia hospitali, na kwenye vituo mbalimbali vya afya.

Kwa kiasi kikubwa afya ya mwanadamu
huatambatana na dhana ya kwamba: nini anapaswa kufanya na nini hapaswi kufanya ili aendelee kuwa mwenye afya njema, pia ni nini anapaswa kula au kunywa, na ni nini hatakiwi kula au kunywa ili awe salama katika afya yake. Yapo mambo kadha wa kadha yanayoweza kumsaidia binadamu kuepuka kutembelea vituo vya afya, au
kumuona daktari mara kwa mara, maana kinga ni bora kuliko tiba.

1.Chakula bora chenye afya njema.
View attachment 2343140

Eating healthy during a pandemic

Si kila kinachoingia tumboni kinafaa kwa matumizi ya chakula, na kukidhi mahitaji ya mwili wa mwanadamu. Mfano, takwimu zinaonesha kuwa kiwango kikubwa cha matumizi ya soda huchangia 22% ya ugonjwa wa kisukari. Chakula bora ni kile kinachodumisha afya ya mwili na kumkinga dhidi ya magonjwa. Chakula kinatakiwa
kitumiwe katika kiwango sahihi, kulingana na uhitaji wa mtu( kazi, umri, hali ya hewa, uzito, muda, hali ya kiafya ya mtu kwa ujumla). Waeskimo wanaopatikana Alaska hutumia samaki katika kipindi kirefu cha maisha yao, lakini mara nyingi hukumbwa na madhara yanayotokana na ukosefu wa matunda pamoja na mboga mboga. Kufikia mwaka 2013 taarifa kutoka katika shirika la chakula duniani yaani FAO, ilionekana kuwa takribani asilimia 70 ya magonjwa yanayotokea katika miongo.
kadhaa ya hivi karibuni, yametokana hasa na matumizi ya wanyama kama sehemu ya mlo, pamoja na mwingiliano wa magonjwa ya binadamu pamoja na magonjwa ya wanyama.

Matumizi ya vyakula vilivyosindikwa viwandani hasa vile vyenye sukari nyingi, rangi, mafuta mengi, pamoja na kemikali mbalimbali kwa ajili ya kuongeza ladha au kuvihifadhi vidumu kwa muda mrefu, vinapendwa sana na wengi na vinazidi
kuongezeka siku kwa siku, na hivyo inaonekana ni vigumu kuepuka matumizi yake, lakini si rafiki kwa afya.

Ukweli usiopingika ni kuwa, vyakula vinavyotokana na nafaka halisi, jamii ya mikunde, matunda, na mboga za majani ni vyakula bora miongoni mwa makundi mbalimbali ya vyakula, sababu zifuatazo:

a. Huwa na virutubisho vyote vinavyopatikana kwenye vyakula vingine kama nyama.

b. Huwa na sifa ya uponyaji, kwa kuwa vina antioksidanti au viondoa sumu kwa baadhi ya vitamini pamoja na madini.

c. Ni vyakula ambavyo havina madhara vikitumiwa katika ubora wake. Lakini zaidi ni kwamba hupatikana kwa urahisi.

Kwa miaka miaka mingi vyakula hivi vimechukuliwa kama vyakula vya watu duni, lakini badala yake vimekuwa na manufaa mengi, ambayo hudhibiti gharama kwa ajili ya matibabu yanayotokana na athari za upungufu wa vyakula hivi.

Kwa karne nyingi zilizopita chakula kama kabeji imekuwa ikitumika kama kinga dhidi ya saratani, ikiwemo pamoja na uvimbe wa saratani. Wagiriki waliipenda pamoja watu walioishi zama za utawala wa warumi kama akina Hipokreti, Galemi pamoja na Diopokrati.

waliithamini kwa kuwa iliwasaidia warumi kukaa kipindi kirefu bila ya kutumia dawa.
Ikiwa unapenda vyakula vitamu kama peremende, chokoleti, sukari, keki pamoja na soda ambavyo vingekuletea madhara mbalimbali kama ongezeko la uzito, ongezeko la sukari mwilini, shinikizo la juu la damu, matatizo ya kusahau, wasiwasi pamoja na msongo wa mawazo, badala yake unaweza kutumia vyakula kama asali mbichi, ndizi, viazi vitamu, mchanganyiko wa juisi mbali mbali kutoka kwenye matunda na mboga za majani kama brokoli, spinachi, karoti, nanasi, tikitimaji, zabibu, embe, tende, miwa, humpa mtu ladha maridhawa pamoja na afya mathubuti.

Tunda aina ya tofaa(Apple) hujulikana kama malkia wa matunda kwa kuwa ni tunda tamu na lenye faida nyingi ndani ya mwili kama vile, kudhibiti tatizo la kukosa choo, shinikizo la juu la damu, saratani ya utumbo mpana, sukari yake pia huwafaa hata wenye tatizo la kisukari.

1. Mazoezi na shughuli za mwili View attachment 2343110 https://1stnews.com/exercise-for-different-age/
Gari huwa haliwekewi mafuta ili liendele tu kukaa kituoni, bali limpeleke
anaeliendelesha pale anapohitaji kufika. Vile vile mwili wa binadamu hauwezi tu
kulishwa chakula na kukaa bila ya kufanya chochote, badala yake chakula hicho kinaweza kugeuka sumu, hasa kisipotumiwa pasipo utaratibu maalumu. Kukaa siku saba bila ya kufanya mazoezi huufanya mwili kuwa dhaifu.

Tafiti zinaonyesha kuwa, mlo kamili pamoja na mazoezi hupunguza uwezekano wa kupata saratani kwa 30%. Asilimia kubwa ya vijana kwa wazee hawajihusishi na shughuli za mazoezi badala yake muda mwingi hutumika kwenye runinga, mitandao ya kijamii pamoja na kazi za kukaa kama zile za maofisini. Mazoezi humkinga mtu na uzito kupita kiasi, matatizo ya moyo, huboresha mfumo wa uzazi pamoja na kuweka vichocheo vya mwili yaani homoni katika uwiano mzuri, mazoezi huboresha mzunguko wa usingizi, mazoezi huongeza homoni za furaha kama vile dopamaini na noradrenalini, zinazosaidia kuondokana na msongo wa mawazo, wasiwasi pamoja na sononeko.

3. Mahusiano mazuri ya jamii.
View attachment 23431234 Benefits of Healthy Relationships - Acenda Afya ya akili pamoja na mtindo wa maisha huathiriwa sana na mahusiano baina ya mtu na jamii anayoishi. Mahusiano mazuri humwepusha mtu dhidi ya msongo wa mawazo na chaguzi mbaya za maisha. Taarifa kutoka shirika la afya duniani(WHO), kufikia Januari 2017, takribani watu milioni 350 duniani walikuwa wameathiriwa na msongo wa mawazo. Msongo wa mawazo mara nyingi hutokana na hali tofauti tofauti
za kimaisha kama uchumi na mahusiano. Hali hii husababisha kinga za mwili kushuka, kukosa hamu ya kula, kukosa usingizi, upungufu wa nguvu za kiume, kutojihusisha na shughuli za mwili pamoja na mazoezi, na hivyo kumfanya mtu kupata magonjwa na maambukizi kwa urahisi.
4. Kiasi
Kila kitu kinatakiwa kifanyike au kutumiwa kwa kiasi hata kama ni kizuri ndani ya mwili, mwili ulitengenezwa.

kwa mifumo inayofanya kazi kwa utaratibu maalumu, mahitaji ya mwili yanapopungua au kuzidi, mwili huwa haufanyi kazi kama inavyotakiwa, mazoezi yafanyike kwa kiasi kulingana na mahitaji au hali ya mtu, kadhalika vilevile kwa chakula, hewa safi, muda wa kulala, muda wa kufanya kazi, muda wa kupumzika, vyote vinatakiwa vizingatiwe katika utaratibu wake.

Vile vile zipo njia zingine kadha wa kadha, zitakazoweza kusaidia kupunguza idadi ya wagonjwa pamoja na maambukizi ya magonjwa katika karne yetu, kama vile kudumisha usafi na utunzaji wa mazingira, kuwa na sera nzuri kuhusu afya na inayotekelezwa na watu wote, elimu ya afya kwa jamii kusisitizwa kupitia vyombo vya habari kama vile runinga, redio, magazeti, majarida pamoja na mitandao ya kijamii, matumizi ya maji safi na salama, kujihusisha na shughuli za ibada kama vile kuimba na kuabudu. Kutembelea vituo vya afya kwa ajili ya kupima maendeleo ya afya ya mwili kama vile shinikizo la damu, kiwango cha sukari mwilini, kiwango cha oksijeni mwilini, pamoja uwezekano wa maambukizi ya magonjwa yanayoweza kutokana na virusi, bakteria pamoja na fangasi, kwa ajili ya kuchukua tahadhari, ushauri nasaha. Salia na afya njema.
nzuri hii nayo kaka asante sana kakanaomba kukufahamu maana unaandika sana
 
Back
Top Bottom