Hesabu za matipper ya Mchanga

Hesabu za matipper ya Mchanga

Either that au uwe mtu wa kushinda kwenye ma gereji uswahilini na maduka ya wauza spea used ambazo hata huelewi unauziwa kitu gani. Huko Tabata kwanza gari yako ndogo uliyoenda nayo inaweza kubaki huko huko na yenyewe, kuna hii njia ya kuingilia Tabata kwenye ma spea kutokea Kigogo nilishanusurika kupinduka na SUV, it is so effed up utadhani unaenda maficho ya ISIS. And then mafundi wanadanganya initial estimates za matengenezo, au hajui undani wa tatizo mpaka akishafungua machuma ndio ndio anakwambia kuna hiki na kile na hiki na kile, inabidi u come up na hela ambayo hukuijua toka mwanzo. Kwa kweli biashara za kusimamia mafundi gereji hazina mpango aisee.... kwa hiyo watu wana resort kwenye kuamini watu, kama ulivyosema, which I don't believe in anymore, utafanyaje biashara kwa hesabu za kupewa facts and figures na mtu baki/mwajiriwa? Kuna dereva ashanambia gari imepasuka engine block njiani Mkata, how? The angels know. Na kwamba amefanya kila awezalo akisaidiana na madereva wenzake kuivuta gari kurudi karibu na mji bila ku incur costs za kupeleka spea/mafundi wa kushusha engine maporini huko au kulivuta at a fee, sasa hujui umshukuru ama umfukuze, sina muda kwa kweli wa kwenda Mkata kuhakikisha engine block limepasuka au amefanya change quarter. No way, not again na hizi biashara za kuaminiana.
NAKUBALIANA ASILIMIA 100 what a hell uache shughuli zoote pengine ndio zilizoleta lori uende kushinda garage na kunafundi alishusha difu kesho yake nikaambiwa kaenda kutengeneza lori Mikumi langu kaliacha.

Watanganyika.
Ukisoma changamoto zangu hapo juu wala usingezungumzia hesabu ya hiyo hela maana kwanza hutaipata madalali nao wanamgao, bila wao kazi haifanyiki na hata hivyo unaweza kwenda kijiweni usiuze huo mchanga. Huko machimboni nako polisi wanachangisha malori bila hivyo hamchoti, pia kuna watu wa rasilimali wana mgao bila kuwasahau kuna mchango sijui wa kijiji yaani ukija kutoa gharama ya mafuta, tingo na dereva ya siku kinachobaki ndio usave in short ni peanut.

Mi napenda challenge lkn za lori kwa kweli ni nyingi mno huwezi kulinganisha na gari zingine ulizotaka kulinganisha. Lori lina kwama porini ambako litakuwa limeharibika pengine na mzigo au limezama. Daladala au taxi hupita kwenye lami lkn siyo malori. Even though kununua lori mtu akuamini umfuatie lori UK hata kwa 50m tu its impractical.
 
NAKUBALIANA ASILIMIA 100 what a hell uache shughuli zoote pengine ndio zilizoleta lori uende kushinda garage na kunafundi alishusha difu kesho yake nikaambiwa kaenda kutengeneza lori Mikumi langu kaliacha.

Watanganyika.
Ukisoma changamoto zangu hapo juu wala usingezungumzia hesabu ya hiyo hela maana kwanza hutaipata madalali nao wanamgao, bila wao kazi haifanyiki na hata hivyo unaweza kwenda kijiweni usiuze huo mchanga. Huko machimboni nako polisi wanachangisha malori bila hivyo hamchoti, pia kuna watu wa rasilimali wana mgao bila kuwasahau kuna mchango sijui wa kijiji yaani ukija kutoa gharama ya mafuta, tingo na dereva ya siku kinachobaki ndio usave in short ni peanut.

Mi napenda challenge lkn za lori kwa kweli ni nyingi mno huwezi kulinganisha na gari zingine ulizotaka kulinganisha. Lori lina kwama porini ambako litakuwa limeharibika pengine na mzigo au limezama. Daladala au taxi hupita kwenye lami lkn siyo malori. Even though kununua lori mtu akuamini umfuatie lori UK hata kwa 50m tu its impractical.

Mkuu kama umetazama kwa karibu nilichosema mimi, hapa inategemeana sana na business plan yako. Kama unafanya biashara hii part time na wewe upo office basi kizaza chako. Kaka mimi mwenywe napiga kilungu bila uwoga, hivyo dereva atanisaidia ijumaa na jumamosi.

Kama gari ni lazamani lazima upate Repair and Maintenance cost. Hilo lipo popote, kuna changamoto kwenye hii biashara lakini cash flow yake inatia moyo. Kuliko hesabu za tax au bajaji. Nilichosema mimi ni kwamba kuwasaidia wajasilimali humu kuangalia kama wanaweza wanunue gari nje ya Tanzania. Offer niliyotoa ni sababu nimeishi hizo nchi kwa miaka 10+ najua mchakato mzima wa magari.
 
hii 120m labda kama unataka kulinunua dar. Nusu ya hiyo bei unapata uk 32 tons scania 8x4 towel.

nikweli mkuu tena yukei bei nzuri ila ukitaka usijute pitsha bandari ya mombasa utafaidi sana
nilienda kuchukua mende yaa kakayangusikupata uhuni kama unaoendelea pale bandarisalama
 
Pia gari lenye matumizi zaidi consumption(fuel) ni hayo ya tani 32 kwani mashine zake ni kubwa
 
mkuu daaa kwenye pesa inabidi kupunguza tu risk , kama unaweza weka tracking system akheri uweke tu
 
Hizo gari kutoka uk Mtanganyika ni model gani?tractor unit?tipper 4x8 which ndo nzuri kuhimili road zetu?
 
Last edited by a moderator:
Inategemea na Maeneo ambayo gari itafanyia kazi.

Kwa Dar maeneo ya kazi ni Mbagala, Gongolamboto, kigamboni na Bunju.

Kwa Bunju ton 4 ni 60,000/70,000. Tone 16 ni 120,000/150,000 na Tone 32 ni 250,000 hadi 300,000.

Tone saba kwa huku zimepotea kabisa. Zimebaki Iveco Cargo chache ambazo zinashindwa kuhumili mikikimikiki ya kazi za mjini.

Usisahau kuna watu wa Tanroads wanapima mizani barabarani. Ukikamatwa fine zao minimum 2mil maxmum 6mil.

Ni Pm kwa zaidi.

Pia huku Mbezi ya kimara fuso za tani 4 zipo kibao na hesabu zake ni 85,000/= hadi 100,000/= kwa siku. Ninasema hivyo kwa uhakika coz hata mimi nipo kwenye hii biashara long time
 
Angalizo tuu wadau sina shaka na mahesabu za magari haswa malori aina ya tipper,tatizo kubwa la biashara hii ni maintanance cost ziko juu sanaa,unaweza pokea hesabu ya miezi mitatu kwa faida lakini mwezi wa nne ikala yote na kukopaaa juu,achilia mbali spare fekii na tabia za madereva wetuu.Udalali pia unachukua sehemu kubwa ya faidaa...au ucheleweshwaji wa malipo..mimi ushauri wangu kama huna mizigo yako mwenyewe by 70% then itakuchukua muda sana kupata matarajio unayo yataka bila kusahau capital intensive ya malori iko juu saanaaa..
 
Angalizo tuu wadau sina shaka na mahesabu za magari haswa malori aina ya tipper,tatizo kubwa la biashara hii ni maintanance cost ziko juu sanaa,unaweza pokea hesabu ya miezi mitatu kwa faida lakini mwezi wa nne ikala yote na kukopaaa juu,achilia mbali spare fekii na tabia za madereva wetuu.Udalali pia unachukua sehemu kubwa ya faidaa...au ucheleweshwaji wa malipo..mimi ushauri wangu kama huna mizigo yako mwenyewe by 70% then itakuchukua muda sana kupata matarajio unayo yataka bila kusahau capital intensive ya malori iko juu saanaaa..

Mkuu sasa toa ushauri watu waweke wapi pesa? Maana umetupa analysis ya gharama.
 
Mtanganyika nimekupa hint hapoo ya 70%utilization by ur own usage,ifanyie kazi na utaona mabadiliko makubwa sanaaa,transpoters wana mitaji mikubwa lakini hawajitambui
 
Last edited by a moderator:
120, chukua eicher zako 2 walahi nakwambia ukisimamia mwenyewe, kwa mwaka 1 tuu capital yako yote inarudi, unaanza kula faida. Nshasimamia sana hizo business nkaona wahindi wanavyotajirika
 
Mkuu sasa toa ushauri watu waweke wapi pesa? Maana umetupa analysis ya gharama.

Use 70/20 percent rule....kama ujuavyo transport inatuexpose kwenye biashara nyingi sana kazi ipoo kuzifanyia fursaa..tunabebeshwaa mizigo mingi sasa why ubebee muda wotee ifanyie kazi value chain ya transport
 
Kwa yeyote anayehitaji Tipper Scania, Tractor Unit, Canter 7 tons, Gari dogo toka UK tuwasiliane nitampatia msaada wa kutosha kwenda kukagua ba process zote za kusafirisha. Kampuni yetu iko hapa UK ( Lets Impo and Expo Ltd) Karibuni no zetu ni +44 7424 138508. Gharama zetu ni nafuu !!
 
Use 70/20 percent rule....kama ujuavyo transport inatuexpose kwenye biashara nyingi sana kazi ipoo kuzifanyia fursaa..tunabebeshwaa mizigo mingi sasa why ubebee muda wotee ifanyie kazi value chain ya transport

Mkuu kwa mji kama Dar es Salaam ambao 80% ya watu wamepanga, na mji unategemea kuongeza watu mpaka 10 million by 2025, maana yake real estate business sio tuu ina boom lakini will continue to soar kwa double digit. Cha muhimu ni jinsi gani you and I will capitalize na kutap that growth. Sababu pesa zetu za mitaji bado sio solid, ndio maana diversification mwanzoni inakuwa impossible, sasa changamoto zote tumezisikia, lakini hakuna doubt kwamba biashara ya Tipper ni sawa na mabasi mwaka 1990 it was hot commodity na watu wengi wametoka. The question is how utaitumia hii business kufund growth.
 
Back
Top Bottom