Heshima na hadhi ya Sheikh Ponda katika nyoyo za Waislam

Mimi ni mkristo tena mkatoliki, naamin Allah atamruzuku sheikh Ponda kwa kuipigania haki na ustawi wa uislamu, nashangaa waumin wa Bakwata wanavomponda laiti wangejua nasema laiti wangeujua ukweli wa dini yao na inavyopelekwa wasingethibutu kumdhihaki sheikh ponda mtu alieteswa, kunyanyaswa kwa kuutetea uislamu
 
Masheikh wa Bakwata hua tunawaita masheikh ubwabwa ashakhum sii matusi, wamewagawa waislamu, shirikisho la uislamu afrika mashariki ambalo linahistoria kwenye uhuru wetu pia, fedha zilizochangwa misikitini kwenye kupigania uhuru, wa nchi yetu yote yamepotea, ama hikma ya kafir ipo usoni pake na sio akilini.
 
Naomba uniulizie kwa Sheikh Ponda vipi ule utabiri wake wa Lissu kuwa rais na yeye kuwa waziri wa dini na mshauri mkuu wa Lissu umefikia wapi.
 
Nilikua nikimuona mitaani sheikh Ponda na alikua mtu mkimya lakini mkakamavu, mara nyingi akitembea kwa hatua zake za harakaharaka. Jambo moja kumuhusu ni kwamba hawezi kupita bila kusalimia watu atakao wakuta mahali, na wewe huwezi kuwa wa kwanza kumtolea salamu, ataanza yeye maana kafanya salamu kama ni ibada vile!

Mara ya kwanza nilipomsikia akiongea ilikua 1993 katika viunga vya Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu. Nilikua nimefika Mahakama ya Kisutu kugonga muhuri wa Hakimu karatasi zangu za kisheria, na kumbe siku hiyo ndio ilikua hukumu ya kina Mazinge na wenziwe katika ile kesi ya kadhia maarufu ya kuvunjwa mabucha ya nguruwe (Mbokomu Butcher) pale Manzese

Kwenye chumba cha mahakama waliruhusiwa wasikilizaji wachache tu. Mawakili wa Washtakiwa ambao walikua ni Yusuph Mchora na Nassib Mselem walimuita Sheikh Ponda ambaye alifika akiwa amechelewa na chumba kishajaa ili naye aingie

Baada ya kama saa moja na ushei hivi Ponda akatoka na kuwakusanya baadhi ya watu ambao niligundua ni Waumini wenzao pia ndugu na jamaa wa Washtakiwa na kuwaeleza kwamba pamoja na ushahidi usio na shaka kwamba hao wahadhiri kina Mazinge, marehemu Magezi na wengine kuonesha kutokuwepo kwenye hayo maeneo wakati vurugu zinatokea lakini hakimu kaamua kuwafunga miaka mitano kila mmoja! Kesi ilitolewa hukumu na marehemu Jaji Projestus Rugazia ambaye wakati huo alikua Hakimu Mkazi wa Mahakama ya Kisutu

Ponda alikua akiongea kwa kukasirika sana na baada ya pale akawaomba wale watu waondoke wakakutane na wenzao ama Msikiti wa Mtoro au Mwembechai(sikumbuki vizuri hilo) ili wajue nini cha kufanya

Walimsikiliza na wote walitii na wakaondoka pale Kisutu bila vurugu kuelekea huko walipokubaliana. Hawa jamaa baadae walikuja kutolewa kwa msamaha wa Rais wakati Mzee Ali Hassan Mwinyi anakaribia kumaliza kipindi chake cha Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Kunzia siku hiyo nimekua namuona na kumfatilia Sheikh Ponda ambapo utamkuta katika kila harakati za Waislamu. Hata mwaka 1998 kwenye vurugu za Mwembechai Sheikh Ponda alikua mbele ingawa sikumbuki kama na yeye alikamatwa. Hata huyu Rajab Katimba anayekua kwenye misafara ya Tundu Lissu ni miongoni mwa waliokua wakiratibu michango kwa ajili ya huduma za waliofungwa na walioathirika na vurugu za Mwembechai
 
Sheikh ponda anaheshimika na jamii nzima sio waislam tu kwakuwa anasimamia haki za raia na binadamu kwa ujumla sio waislam peke yao
 
Sheikh ponda anaheshimika na jamii nzima sio waislam tu kwakuwa anasimamia haki za raia na binadamu kwa ujumla sio waislam peke yao
Nakubaliana nawe mkuu Kayaman. Wilfred Rwakatare aliyewahi kua Mbunge wa Bukoba mjini wakati fulani alijikuta yupo mahabusu na wakakaa selo moja na Sheikh Ponda

Alikua curious kumfatilia kutokana na sifa zake "mbaya" alizokua akizisikia na kuaminishwa lakini anakiri mwenyewe baada ya kumfahamu kua Sheikh Ponda ni mtu mwenye maadili, tabia njema na muungwana sana sana.

Alimuelezea kama ni mtu mpenda haki, anayechanganyika na watu wa aina zote na mwenye hofu ya kweli ya Mungu. Anasema hata wakiwa wanaletewa chakula kutoka kwenye familia zao walikua wanakula pamoja bila kujali kimeletwa na mke wa Rwakatare au mke wa Sheikh Ponda. Anasema mengi juu ya Ponda ni propaganda chafu tu hasa kutoka kwa BAKWATA
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…