HESLB mkimaliza kuwaumbua wadaiwa sugu Jumatato ijayo, muwaumbue pia na wale wanaofanya tatizo la ajira kuongezeka nchini

HESLB mkimaliza kuwaumbua wadaiwa sugu Jumatato ijayo, muwaumbue pia na wale wanaofanya tatizo la ajira kuongezeka nchini

CELLULAIRE

Member
Joined
Mar 16, 2016
Posts
76
Reaction score
97
Nichukue fursa hii adhimu kabisa kuwapongezeni watu wazima ambao ni Watendaji wa Bodi ya Mikopo nchini ( HESLB ) kwa kuweza kupoteza muda wenu mwingi, kujadiliana, kuchanganya fikra zenu hadi baadae mkaja na maamuzi ambayo Kwenu mmeona yana Tija ya kuwaumbua wadaiwa sugu wa mikopo na kuweka picha zao siku ya Jumatano ijayo.

Ombi langu kuu kwenu ni moja tu nalo ni kwamba nawaombeni mkishamaliza kuwaambua hao wadaiwa sugu kama akili zenu zilivyowatumeni na mlivyoshauriana basi kwa moyo huo huo pia kesho yake mtuwekee pia na wale Watanzania wachache au hata ikiwezekana mmoja wao ambaye ndiyo Kisababishi kikuu cha Wasomi ambao ni wadaiwa Sugu hao Kutokupata Kazi au kutokuwa na Uwezo wa Kujipatia Vipato kama ilivyokuwa zamani ili nao waweze Kuwalipeni hayo Madeni yenu.

Imenifikirisha mno kama watendaji wasomi wazima wa Bodi ( HESLB ) tena mlienda shuleni kabisa huku wengi wenu mkiwa na Elimu za Bachelors, Masters na PhD's mlikaa kitako kabisa katika vikao vyenu na akili zenu zikawatumeni mje na mkakati huu. Nawaza hivi hiyo Taasisi yenu ingekuwa inakaliwa na watendaji ambao hawana elimu hizo kama zenu hali ingekuwaje au na wao Maamuzi yao yangekuwaje?
 
Tatizo ni kwamba huu mkopo hauna lengo la kumsaidia mwanafunzi, bali una lengo la kumyonya mwanafunzi baada ya kumaliza chuo. Inawezekanaje hela unayompa mwanafunzi anapoingia mwaka mwingine we ushaanza kumpiga riba kabla hata hajamaliza masomo yake ? Ni bora wangefanya hivi, mwanafunzi pindi amalizapo masomo yake wachukue jumla ya hela waliyompa kisha waweke riba ya kurudisha hiyo hela kuliko ilivyo sasa.
 
Wangeweka grace period ili mkopaji arejeshe fedha walau mwaka mmoja baada ya kumaliza masomo yake ama yule atakaye weza arejeshe hata kabl ya muda huo kutegemea na uwezo na upatikanaji wa fedha. Lakini pia, mfumo wa urejeshaji unaruhusu kufanya marekebisho ya mahesabu kwa kupunguza deni ili mkopaji arejeshe fedha kwa mkupuo?
 
Ngosha kwisha habari yake,ametumia ma TRILIONI kununua midege,SGR na StiGiLoz zinapumulia mashine hela imekata,sasa kapiga PINI fedha NSSF kimya kimya watu wasilipwe hela ili mradi achukue fedha akakamilishe miradi yake HEW(white elephant project),anawakaba HESLB wakusanya madeni ayachukue akatapakanye kwenye miradi hewa.

Awamu ya 4 tunaaminishwa kwamba ilikuwa na ufisadi wa kutisha,wafanyakazi hewa,rushwa na bla bla kibao lakini ndio ilikuwa bora kuliko awamu hii ya MATAGA praise team,awamu ya 4,NSSF ilikuwa hela inatoka ndani ya wiki 3 tu,safari za wafanyakazi kama zote,wafanyakazi hewa walikuwa wanalipwa,vyeti feki walikuwa wanalipwa na serikali ilikuwa inajiendesha safi tu,huyu ngosha anatuambia anakusanya mara mbili ya kikwete lakini fedha za kurun miradi hana.....FUTUHIIII NDIO NI FUTUHI.
 
Ngosha kwisha habari yake,ametumia ma TRILIONI kununua midege,SGR na StiGiLoz zinapumulia mashine hela imekata,sasa kapiga PINI fedha NSSF kimya kimya watu wasilipwe hela ili mradi achukue fedha akakamilishe miradi yake HEW(white elephant project),anawakaba HESLB wakusanya madeni ayachukue akatapakanye kwenye miradi hewa.

Awamu ya 4 tunaaminishwa kwamba ilikuwa na ufisadi wa kutisha,wafanyakazi hewa,rushwa na bla bla kibao lakini ndio ilikuwa bora kuliko awamu hii ya MATAGA praise team,awamu ya 4,NSSF ilikuwa hela inatoka ndani ya wiki 3 tu,safari za wafanyakazi kama zote,wafanyakazi hewa walikuwa wanalipwa,vyeti feki walikuwa wanalipwa na serikali ilikuwa inajiendesha safi tu,huyu ngosha anatuambia anakusanya mara mbili ya kikwete lakini fedha za kurun miradi hana.....FUTUHIIII NDIO NI FUTUHI.
ili la NSSF ni tatzo kubwa sana,, hawa wazee ni wengi na wanateseka,,, miezi sita inapita mstaafu hajapewa hela zake,,, tunapoelekea ni kubaya sana zaid ya tulipotoka,,,
 
ili la NSSF ni tatzo kubwa sana,, hawa wazee ni wengi na wanateseka,,, miezi sita inapita mstaafu hajapewa hela zake,,, tunapoelekea ni kubaya sana zaid ya tulipotoka,,,

Miezi 6 michache hivyo mkuu?

Kuna watu wamekaa tangu 2018 January na documents zote zimekamilika kila kitu lkn mpk leo hawajapewa hela zao,wengine wamepewa mafao yao robo robo bado wanawadai na siku hizi wanaanza tabia ya kukulipa pensheni yako ya kila mwezi kabla ya mafao yako ili uitumie kusogeza siku mpk utakapolipwa hayo mafao yako baada ya hio miaka wanayotaka wao.

Inshort jamaa ni wanyama sana,jamaa hua anakaa mbele ya tv anasema nchi hii ni tajiri sana ina mahela mengi huku wastaafu na familia zao wanamcheki tu wanabadilisha channel/radio huku wakisitika tu.
 
Watuumbue tu wanadhani tunaogopa ,Kuna kipindi Fulani majina yetu kama laki 1 yaliwekwa mtandaoni na mikwara kibao kwa hiyo Hawa jipya hao waweke tu hizo picha ,binafsi nahisi deni langu lishafika milioni 20 manake kila mwezi wanaongeza penalty
 
Miezi 6 michache hivyo mkuu?

Kuna watu wamekaa tangu 2018 January na documents zote zimekamilika kila kitu lkn mpk leo hawajapewa hela zao,wengine wamepewa mafao yao robo robo bado wanawadai na siku hizi wanaanza tabia ya kukulipa pensheni yako ya kila mwezi kabla ya mafao yako ili uitumie kusogeza siku mpk utakapolipwa hayo mafao yako baada ya hio miaka wanayotaka wao.

Inshort jamaa ni wanyama sana,jamaa hua anakaa mbele ya tv anasema nchi hii ni tajiri sana ina mahela mengi huku wastaafu na familia zao wanamcheki tu wanabadilisha channel/radio huku wakisitika tu.
wako wazee hata izo za mwezi hawajaanza kupewa,,, yani unakuta mzee alikuwa anafanya kazi wizarani lakini kastaafu kakaa mwaka mzima hajaona mafao kiasi cha kwamba hadi ile akiba aliyokuwa nayo imeisha anaanza kukopa mtaani,,, mzee kaitumikia serikali miaka 30 na zaidi alaf hapewi haki yake hii si ni balaa
 
wako wazee hata izo za mwezi hawajaanza kupewa,,, yani unakuta mzee alikuwa anafanya kazi wizarani lakini kastaafu kakaa mwaka mzima hajaona mafao kiasi cha kwamba hadi ile akiba aliyokuwa nayo imeisha anaanza kukopa mtaani,,, mzee kaitumikia serikali miaka 30 na zaidi alaf hapewi haki yake hii si ni balaa

Na yule bwana hua anasimama hadharani huku akisema kwa kujiamini kabisa eti tuna hela za nyingi na ni matajiri sana na J2 anaenda kabisa kanisani wkt wako wanatutesa wastaafu huku mtaani.

Wastaafu wamekua omba omba tu,hakuna heshima ya kuitwa mstaafu wa serikali,ni upuuzi mtupu.
 
Katika sheria za kinyonyaji huyu ngosha ameipitisha ni hii ya bodi ya mikopo.
Jamaa kadhamiria kabisa kiwafanya wote waliosomeshwa na hiyo bodi kuwa watumwa milele ilhali yeye na viriba na wenzie walisomeshwa na serikali bure kabisa, hajaona haitoshi hawa wa mikopo wakomeshwe.
Mkopo wanaotoa HESLB kwa wazazi wanaojiweza better wasomeshe watoto wao kupitia mikopo ya bank inalipika...
Sheria nyingine ya kinyonyaji ni ya mifuko ya jamii, ngosha jitafakari sana unayoyatenda kwa taifa hili.
Vijana na wazee mtakaoendelea kuchagua viongozi walioshindwa kuweka mpango mkakati wa kurekebisha sheria ya bodi ya mikopo na ile ya mifuko ya jamii mnaendelea kuchangia ufukara kwenye familia na koo zenu.
 
Back
Top Bottom