Ni haki yao kutukanwa kwa ujinga wao hvy usiwatetee.angalia sababu su vigezo vya kukosa mkopo walivyovitoa.mf. Wanasema kama ulisoma privet basi unauwezo wa kujilipia, kwanza kwanini hawakusema mapema ili mtu huyu ajue na asijisumbue kuomba mkopo na kupoteza muda na pesa? Et wenye dip wanaweza kujisomesha kwanza kwa mshahara upi? Na je wanajua wategemezi walionao wanaowategemea? Et wamepembua kwa vigezo hvy.vipi yatima wamekosa na waliambatanisha na vyeti vya vifo vya wazazi wao na bado wakakosa na wasio yatima wakapata tena kwa asilimia mia? Hivi kwanini wasingetoa mkopo kwa wastani wa asilimia kadhaa mf. Hamsini kwa kila aliyeomba kuliko kumrundikia mtu mmoja asilimia zote mia? Kwa msingi huo kwanini wasitukanwe?watasababisha vurugu za bure kabisa kwa ubabaishaji wao. Wamekula sh. Elfu thelathin hawajatosheka wameleta mradu mwingine wenye manufaa kwao et kukata rufaa ulipie tena huku ulishapoteza elfu thelathini na bado wakadharau viambatanisho vyako. Mimi namuomba mh. Rais j. K. Aingilie kati kutunusuru na hii kadhia ya ubabaishaji wa watendaji wa bodi hii.maombi yangu kwa mh. Rais j.k ni mosi, vunja uongozi wa bodi kwani umeshindwa kazi. Pili, naomba uagize kila aliyekosa mkopo apewe asilimia hamsini ya gharama za masomo kulingana na gharama za chuo alichoomba muombaji. Naimani serikali yako sikivu italishughurikia haraka iwezekanavyo. Nawasilisha kwako mh. Rais dr. J.k.