Hiddink ateuliwa meneja mpya Chelsea

Hiddink ateuliwa meneja mpya Chelsea

RUCCI

JF-Expert Member
Joined
Oct 6, 2011
Posts
1,701
Reaction score
1,714
attachment.php


Aliyekuwa meneja wa timu ya taifa ya Uholanzi Guus Hiddink ameteuliwa kuwa kaimu meneja wa Chelsea hadi mwisho wa msimu.

Ameteuliwa baada ya Jose Mourinho kufutwa Alhamisi.

Hiddink, aliwahi kunoa Chelsea wakati mmoja, alipowasaidia kushinda Kombe la FA mwaka 2009, lakini bado hajatia saini mkataba.

The Blues wamo nambari 16 ligini kwa sasa baada ya kushindwa mechi tisa kati ya 16 walizocheza msimu huu Ligi Kuu Uingereza.

Hiddink alishinda mataji sita ya ligi ya Uholanzi na Kombe la Ulaya akiwa meneja wa PSV Eindhoven ya Uholanzi katika vipindi viwili.

Pia aliongoza timu za taifa za Korea Kusini, Australia na Urusi kabla ya kujiunga na Chelsea mara ya kwanza kujaza pengo lililoachwa na Luiz Felipe Scolari Februari 2009.

Alijiuzulu wadhifa wake kama mkufunzi wa timu ya Taifa ya Uholanzi mwezi Juni, baada ya kutofanya vyema katika juhudi za kuwasaidia kufuzu kwa Euro 2016.

Mwishowe Uholanzi hawakufuzu kwa michuano hiyo.

Chanzo: BBC Swahili
 

Attachments

  • 151219081747_guus_hiddink_file_512x288_pa_nocredit.jpg
    151219081747_guus_hiddink_file_512x288_pa_nocredit.jpg
    18 KB · Views: 651
Back
Top Bottom