Butchery
yes, Butchery.
Ukifungua butcher angalu sehemu mbili hadi nne tofauti, na ukaweza kumanage kununua ngombe wako mwenyewe na kuchinja yafuatayo ndo mazao ya ng'ombe.
1. Ngozi, kichwa, mapembe, mkia, ulimi na miguu (vyote kwa pamoja unaweza uza kwa 30,000/= hadi 51,000/=)
2. Utapata utumbo kwa ngombe wa kawaida ni kg 8 - 15 (kila kilo ukiuzia machinjioni ili kuondoa usumbufu utauza kwa Tsh 3,000/=)
3. Maini kwa ng'ombe wa kawaida anatoa kg 2 hadi 2.5 (Pia ukiamua kuuza machinjioni utauza kwa 8,000/= kwa kila kilo)
4. Nyama nadhani unafahamu bei yake.
Kumbuka ng'ombe kwa ujumla anaweza kuleta faida kuanzia 20% - 50% ya manunuzi inategemea.
Hivyo hauwezi kukosa kuanzia 50,000- 200,000 kama faida kwa siku, kwa mwezi profit inaweza kuwa 1.5M hadi 6M inategemea.
Nimeambatanisha screen shoot ya ng'ombe niliyechinja leo.
Angalizo: Hasara ni kugusa tu na faida vilevile ni kugusa tu, kuwa makini kwa mwanzo simamia biashara mwenyewe.
Capital kwa kila butcher ni 2M(Setup, mzani digital, vifaa local, sale, na vibali).
Wasaaaalam.
Langu jina ninaitwa
Machepele.
View attachment 2832140