Hii ajali ya kwa Mwamposa vyombo vya usalama haviwajibiki?

Hii ajali ya kwa Mwamposa vyombo vya usalama haviwajibiki?

Red Giant

JF-Expert Member
Joined
Mar 9, 2012
Posts
15,657
Reaction score
20,967
Kwanza niwape pole wahanga wote wa ajali ya jana moshi mjini. Pili niseme kuwa jukumu kubwa usalama wa eneo lile lilikuwa la Mwamposa na waandaaji wa ile shughuli. Lakini najiuliza iwapo vyombo vya usalama (hasa polisi) hawakuwa na jukumu lolote kuhakikisha lile eneo ni salama?

Mtu anapoenda kuomba kibali cha kukusanyika, kabla ya kumpa hawataki kuhakikishiwa kuwa kutakuwa na wanaosimamia usalama?.

Naomba wale waliofanya uzembe jana na kuleta maafa wawajibishwe na pia tujifunze na kuweka utaratibu ili jambo kama hili lisitokee tena.
 
Mwisho wa kibali ilikuwa saa 18:00 yeye aliendelea hadi usiku Mnene,inabidi awajibike MWAMPOSA Mwenyewe.
 
Katika nchi ya Puerto Rico mikutano ya kisiasa ya vyama vya upinzani policeccm huwa hawatoi vibali kwa kigezo kuwa hakuna usalama ila katika matamasha ya kidini huwa hakuna hata haja ya kuomba kibali![emoji12][emoji12][emoji12]
 
Mwisho wa kibali ilikuwa saa 18:00 yeye aliendelea hadi usiku Mnene,inabidi awajibike MWAMPOSA Mwenyewe.
Hapo anawajibika pakubwa sana. Lakini nature ya ajali (stampede) inaweza tokea hata mchana wa jua kali, inahitaji tu mkusanyiko. Kulikuwa na hatua za kiusalama kuzuia stampede?
 
Hapo anawajibika pakubwa sana. Lakini nature ya ajali (stampede) inaweza tokea hata mchana wa jua kali, inahitaji tu mkusanyiko. Kulikuwa na hatua za kiusalama kuzuia stampede?
Mkuu swala la usalama wa waamini 100% ilikuwa mikononi mwa MWAMPOSA,Polisi wapo pale kwa ajili ya kulinda vitendo vya kijinai visitokee/kudhibiti,Mwamposa ilitakiwa apime mwenye kitendo cha kuwaamuru kondooo(watu wengi) kukanyaga mafuta kwenye sehemu ndogo kisingeweza kuleta maafa? Polisi hawawezi kumzuia mwamposa akiwaamuru Kondoo wake wakanyage mafuta maana ni imani yao na mwamposa,polisi wangeingia kati endapo mwamposa angesema haya toa kisu mchinje mwenzako hapo ungeona polisi wanainglia kati.
 
Swali langu ni moja tu kwako mleta hoja; Upo wapi kwa sasa hivi? Ulikuwepo kwenye tukio? Umeshuhudia nini kwa hili tukio?? Usianze kulaumu na kuhukumu kitu usokijua.
Waache usalama wafanye yao ndio wapeleke kwa Pilato achambue atuletee hukumu.
 
Mwisho wa kibali ilikuwa saa 18:00 yeye aliendelea hadi usiku Mnene,inabidi awajibike MWAMPOSA Mwenyewe.

Waliompa kibali mwisho 18:00, hawakuenda kuhakikisha shughuli imekoma muda huo?
 
Kwanza niwape pole wahanga wote wa ajali ya jana moshi mjini. Pili niseme kuwa jukumu kubwa usalama wa eneo lile lilikuwa la Mwamposa na waandaaji wa ile shughuli. Lakini najiuliza iwapo vyombo vya usalama (hasa polisi) hawakuwa na jukumu lolote kuhakikisha lile eneo ni salama?

Mtu anapoenda kuomba kibali cha kukusanyika, kabla ya kumpa hawataki kuhakikishiwa kuwa kutakuwa na wanaosimamia usalama?.

Naomba wale waliofanya uzembe jana na kuleta maafa wawajibishwe na pia tujifunze na kuweka utaratibu ili jambo kama hili lisitokee tena.
Niliwahi shauri idadi ya watu nchi hii inakuwa kwa kasi, public admin inahitajika kuimarishwa, kule mbeya uwanja wa mpira ulikanyagwa na kuharibiwa na wacheza disco.

Leo watu wamekanyagwa na kufa, mwaka Jana binti alika yagwa wakigombea pesa zilizofurushwa hewani na diamond, mwaka Jana camera zilivunjwa waandishi wakigombea pesa zulizokuwa zikigawiwa na wolper.

Nilishauri mikutano ifanyike kwenye kumbi maalumu (arena) pale na viti na ulinzi wakutosha. Hata macca old ibada ya kumponda shetani imedhibitiwa watu hawafi tena
 
Waliompa kibali mwisho 18:00, hawakuenda kuhakikisha shughuli imekoma muda huo?
Two wrongs don't make a right........Kama Polisi waliopewa dhamana ya kulinda mkutano huo na kama hawajatekeleza majukumu yao nao wanaingia kwenye hiyo kesi.
 
Back
Top Bottom