kovidii
JF-Expert Member
- May 4, 2020
- 277
- 266
Nimekuwa mkulima wa miwa ya kuzalisha sukari katika Bonde la Kilombero kwa miaka kadhaa sasa ila kwa kipindi cha miaka mitatu iliyopita soko limeyumba kupita kiasi. Tatizo kubwa ni mwekezaji(kiwanda Cha sukari) kushindwa kuhimili wingi wa miwa ya wakulima wa nje (autogrowers).
Kwakuwa ni uwekezaji mkubwa na nguvu nyingi nilielekezea huko ilibidi nitafakari njia mbadala ya kuiuza miwa ile (ukizingatia mimi ni ni mkazi wa Dar, so hata usimamizi wa mauzo kule shamba unakuwa mdogo). Mwanzoni mwa mwezi March nikapata wazo la kuileta Dar kuiuza kwa wanaouza juice ya miwa. Nikaanza kufanya upembuzi wa kutafuta soko kwakuwa miwa ile iko tofauti kidogo kulinganisha na miwa iliyozoeleka kukamua juice hapa mjini.
Ilibidi nilete sample ya bidhaa yangu kwa wateja niliowakusudia, walionyesha kuikubali sababu miwa ile ina sukari zaidi ya hii waliyoizoea. Nikatafuta pia mahali pa kuweka mzigo wangu pindi nitakapoianza hiyo biashara. Baada ya kuona kila kitu kimeenda sawa wakati najiandaa kufuata mzigo ndo balaa la Corona likawa limepamba moto then kukawa na mfungo wa Ramadhan so ikabidi nitulie kidogo.
Baada ya hali kutulia na mfungo kuisha nikafanya safari. Kwa kuanzia nilipanga kuanza na angalau tani10, ili kama biashara itaenda vizuri niongeze ukubwa wa mzigo. Nilifanikiwa kukata na kupakia fuso, Jumapili tarehe 21/6 nikaingiza mzigo Dar.
Balaa lilianza kesho yake Jumatatu nilivyoanza ku-suplly mzigo kwa wateja wangu. Biashara haikuwa kama matarajio niliyokuwa nayo. Hadi leo ninandika thread hii mzigo uko zaid ya tani 7. Mbaya zaidi bidhaa hii baada ya siku 10 haifai tena kwa matumizi kwahiyo nikiangalia uchache wa mzigo ninaoupush per day naona kabisa mzigo hautakwisha na nitapata hasara.
Kinachoniumiza kichwa, matumaini yangu kama biashara ingekuwa vizuri hiyo hela ndo ingenisaidia kumsafirisha first born wangu shule this weekend. Kilichonisukuma kuandika uzi huu wakuu, ni imani yangu kwamba jukwaa hili lina aina zote za watu so kwa yeyote anayefahamu maybe mtu mwenye uzalishaji mkubwa wa Cane juice au popote kwenye kiwanda cha kutengeneza ethanol/spirit ili niiuze hii tani 7 kwa pamoja angalau niokoe gharama za msingi nilizoingia especially usafiri, labour charges etc.
Kwa yeyote mwenye kujua ufumbuzi wa hili jambo nahitaj msaada wake
Mwasiliano: 0624406434
Natanguliza shukrani!
Kwakuwa ni uwekezaji mkubwa na nguvu nyingi nilielekezea huko ilibidi nitafakari njia mbadala ya kuiuza miwa ile (ukizingatia mimi ni ni mkazi wa Dar, so hata usimamizi wa mauzo kule shamba unakuwa mdogo). Mwanzoni mwa mwezi March nikapata wazo la kuileta Dar kuiuza kwa wanaouza juice ya miwa. Nikaanza kufanya upembuzi wa kutafuta soko kwakuwa miwa ile iko tofauti kidogo kulinganisha na miwa iliyozoeleka kukamua juice hapa mjini.
Ilibidi nilete sample ya bidhaa yangu kwa wateja niliowakusudia, walionyesha kuikubali sababu miwa ile ina sukari zaidi ya hii waliyoizoea. Nikatafuta pia mahali pa kuweka mzigo wangu pindi nitakapoianza hiyo biashara. Baada ya kuona kila kitu kimeenda sawa wakati najiandaa kufuata mzigo ndo balaa la Corona likawa limepamba moto then kukawa na mfungo wa Ramadhan so ikabidi nitulie kidogo.
Baada ya hali kutulia na mfungo kuisha nikafanya safari. Kwa kuanzia nilipanga kuanza na angalau tani10, ili kama biashara itaenda vizuri niongeze ukubwa wa mzigo. Nilifanikiwa kukata na kupakia fuso, Jumapili tarehe 21/6 nikaingiza mzigo Dar.
Balaa lilianza kesho yake Jumatatu nilivyoanza ku-suplly mzigo kwa wateja wangu. Biashara haikuwa kama matarajio niliyokuwa nayo. Hadi leo ninandika thread hii mzigo uko zaid ya tani 7. Mbaya zaidi bidhaa hii baada ya siku 10 haifai tena kwa matumizi kwahiyo nikiangalia uchache wa mzigo ninaoupush per day naona kabisa mzigo hautakwisha na nitapata hasara.
Kinachoniumiza kichwa, matumaini yangu kama biashara ingekuwa vizuri hiyo hela ndo ingenisaidia kumsafirisha first born wangu shule this weekend. Kilichonisukuma kuandika uzi huu wakuu, ni imani yangu kwamba jukwaa hili lina aina zote za watu so kwa yeyote anayefahamu maybe mtu mwenye uzalishaji mkubwa wa Cane juice au popote kwenye kiwanda cha kutengeneza ethanol/spirit ili niiuze hii tani 7 kwa pamoja angalau niokoe gharama za msingi nilizoingia especially usafiri, labour charges etc.
Kwa yeyote mwenye kujua ufumbuzi wa hili jambo nahitaj msaada wake
Mwasiliano: 0624406434
Natanguliza shukrani!