Hii biashara ya utumwa ukiitafakari inaumiza sana: Waafrika tulifanywa kama bidhaa!

Hii biashara ya utumwa ukiitafakari inaumiza sana: Waafrika tulifanywa kama bidhaa!

mbingunikwetu

JF-Expert Member
Joined
Feb 17, 2015
Posts
13,897
Reaction score
18,477
1695154594113.png

Tunachotakiwa kukidai kwa wakoloni na wote waliojihusisha na biashara ya utumwa ni kwamba wanatakiwa kuomba radhi na wakiri kuwa, walitufanyia jambo la kinyama sana!

Cha kusikitisha ni kwamba hadi sasa hakuna aliyewahi kujitokeza kuomba radhi rasmi, japo wanakubali kuwa biashara hiyo haikustahili kuwepo.

Moja ya sababu inayowafanya wasijitokeze kuomba radhi ni hofu kuwa hatua itakayofuata ni kudaiwa fidia.

Kwa maoni yangu, ili kutunza heshima yetu, kuombwa radhi ni muhimu, lakini kudai fidia ni kama kukubali kujipiga bei tena.
 
1695154831633.png


In a joint initiative, African countries are renewing their efforts to obtain reparations from European countries for the transatlantic slave trade and other colonial-era wrongs committed centuries ago.

The slave trade — which affected millions of Africans — was the largest forced migration in history and one of the most inhumane.

Over 400 years, Africans were transported to many areas of the world, yet no reparations have as yet been paid. The process is proving much slower than many Africans expected.
 
CCM inaenfesha biashara ya utumwa mamboleo kwa kubeba washangiliaji wa mikutano yao na kuwalipa ujira mdogo sana.
 
Miaka michache sisiem itakuwa imeshawarudiha kwenye Shamba za Mikonge.
 
Marekani ukiingia kinyemela wanahesabu wewe ni mtumwa wa hiari!! Wanahesabu ni cheap ,labor imejileta!! Kazi za ovyo ndo za kwako! Ili maadam haufanyi uhalifu, hawana shida na wewe! Hatimaye wanakupa green card!! Mtumwa wa kujileta huyo, si raia lakini ni mkazi!! Hana haki zozote isipokuwa haki ya kuishi marekani!
 

World powers should consider slavery reparations – UN​

No country has adequately accounted for past atrocities and the ongoing consequences of subjugation, the global body said in a report.
The United Nations has advised countries on an array of measures, including financial compensation, for colonialism and the enslavement of people of African descent. The debt remains, despite the length of time that has passed and the difficulty of identifying perpetrators and victims, the document outlines.

Such difficulties cannot be the basis for nullifying the existence of underlying legal obligations,” UN Secretary-General Antonio Guterres said in the report released on Tuesday.
“No state has comprehensively accounted for the past and addressed its contemporary legacies” for “violently” uprooting an estimated 25 million to 30 million people from Africa, the report claims.

For decades, African and Caribbean governments and activists have called for accountability for slavery and the colonization of their countries.
 
Ni kweli biashara ya utumwa ilikuwa moja kati ya historia mbaya sana kwetu sisi waafrika, watu walichukuliwa kutoka sehemu mbalimbali za Afrika kwa nguvu na kuuzwa kama bidhaa bila ya kujali utu wao, jamii zao, familia zao na nyanja mbalimbali za maisha yao binafsi. Wazungu, Waarabu na hata Waafrika wenzetu walikuwa wakifanya biashara hii kutokana na tamaa ya pesa na utajiri.

Pamoja na ubaya wote ulioletwa na hali hii, ninaona ni hali ambayo isingeweza kuepukika katika historia ya maisha yetu binadamu, watu wenye nguvu wamekuwa wakiwatumikisha wanyonge tangu enzi na enzi, siku zote mtu mwenye nguvu atatamani kubaki na nguvu hizo na pengine kuziongeza zaidi, hii ni hali ya maisha ya ubinadamu, tumeumbiwa tamaa ya vitu vikubwa na kudharau vinyonge. Nafikiri hata kama historia ingepinduka kiasi kwamba Mwafrika angepata nguvu na teknolojia bora kuzidi ya watu wengine mambo yangekuwa hivi hivi, angetamani naye kwa njia yoyote aweze kuongeza nguvu zake na utawala kwa wale ambao angewachukulia kuwa chini yake.
Hata sasa ninaweza kusema kuwa utumwa bado unaendelea ila ni kutokana na sheria zilizopo katika zama hizi tunaona kama mambo yametulia lakini ndani kwa ndani tuna chembechembe bado za kutumikisha pale tunapopata mtu/watu ambao tunaoweza kuwafanyia hivyo kama tuna uhakika hayupo wa kutuzuia.
Nikijaribu kufikiria kwa mtu yeyote sasa hivi akipewa uwezo wa kuwa na watu wa kukufanyia kazi kiasi kwamba mali na utajiri wako unakuwa ukiongezeka na unapewa uamuzi wa kulipa mshahara mkubwa, mshahara mdogo au kutowalipa kabisa. Je wengi wetu tungechagua kipi? tungeweza kumlipa mtu kama hakuna kitu kinachotulazimisha kumlipa? kama tungepewa uamuzi wa kumpa mtu sehemu ya utajiri tulio nao au kuendelea kulimbikiza tungechagua kipi? Mwisho wa siku nionavyo mimi ni kwamba binadamu tumeumbiwa uroho na ubinafsi hasa pale tunapopata nguvu kupita watu wengine, kama hakutakuwa na kizuizi chochote cha nje basi naona watu watatumia njia zozote watakazoona zinafaa kuzidi kujinufanisha.

Nikirudi katika mada, kuhusu kuombwa radhi na heshima yetu sidhani kama itasaidia katika kufuta yaliyokwisha kutendeka na kwa namna mambo ninavyoyaona hata kama tukifanikiwa kuombwa msamaha itakuwa imefanywa kinafiki ili kuzima kelele na sio kwamba kutakuwa na majuto yoyote nyuma yake, kama ni heshima tunaitaka basi isiwe heshima ya kupewa bali iwe ni heshima tutakayoijenga sisi wenyewe bila ya kuwa watu wa kutia huruma na kusingizia shida zote tulizonazo zimetokana na utumwa (ni kweli utumwa umechangia kuturudisha nyuma lakini hatuwezi tukawa tunanyooshea vidole Wazungu/Waarabu kwa kila aina ya matatizo tuliyonayo), heshima hii kama Waafrika bado hatuna katika dunia ya sasa na sidhani kama kuombwa msamaha itaongeza heshima yoyote mbele ya macho ya waliotutawala.
 
Back
Top Bottom