Hii hali inanipa upweke sana nimejitahidi kuikwepa lakini wapi

Hii hali inanipa upweke sana nimejitahidi kuikwepa lakini wapi

TheForgotten Genious

JF-Expert Member
Joined
Jan 18, 2014
Posts
2,087
Reaction score
3,156
Katika maisha yangu yote sijawahi kuwa na marafiki,na sipendi kabisa masuala ya marafiki,hata nikipata tatizo sina rafiki wa kumwambia mtu pekee ninayeweza kumwambia ni mama tu.

Lakini pia si mtu mwepesi wakueleza hisia ama changamoto zangu kirahisi hata kwa mama,huwa namueleza nikiona kabisa hii inaniendea kombo.

Nikikaa na kundi la vijana wenzangu huwa nakuwa msikilizaji tu tena kwa muda flani tu kisha naondoka zangu.

Napenda kujitenga sana na ninaweza kukaa Siku nzima peke yangu bila taabu yoyote ile,nikitumia muda huo kufanya kazi zangu Za kiofisi au nikifanya coding ama kufanya simulation za sakiti mbalimbali kama nipo nje ya majukumu ya kitabibu.

Nikiona mtu anaanza kunizoea huwa namkwepa haraka sana maana sipendi mazoea na watu.

Sehemu ninayoishi wapangaji wenzangu inaweza pita miezi 2 hatuja onana.

Sipendi kabisa kwenda katika matukio ya sherehe na hata ikiwa ni lazima huwa nakuwa mtu wakujitenga sana maana Mara nyingi huwa siambatani na mtu kabisa.

Sipendi kupiga piga picha hovyo kabisa. Napenda sana familia hapo ndio nadhani ni marafiki pekee naweza kudumu não japo sina família.

Japo kuna wakati huwa nakuwa mpweke mno hasa nisipokuwa na na kazi ya kufanya ,hivyo huwa najitahidi kuhakikisha nakuwa na kazi Ya kufanya kila Siku.

Mimi napambana kivyangu na mambo yangu sipendi kumshirikisha mtu kabisa ,ila huwa nakuwa na hisia yakumshirikisha mke tu lakini sina.

Ninaamini kwamba kuwa na marafiki na kujichanganya sana na watu ni njia rahisi ya mimi kujiletee matatizo.

Nafikiria kuoa ili kuepukana na hali hii nadhani itanisaidia.
 
Sijaona popote ulipojitahidi kukwepa. Bali umeamua kuipaliliza ili uzidi kuwa mpweke.

Ukitaka kuukimbia upweke basi tafuta marafiki. Jichanganye na watu, hudhuria mikusanyiko na usijione spesheli.

Vinginevyo ishi na upweke wako..
 
Hivi Mke unayetafuta utathubutu kumchakata kweli?!!
 
Issue sio kuwa karibu na watu ila mna common interest mkuu maana kuona mazungumzo yako hayafit na yako ni wazi mpo tofauti. Hivyo ni aidha utafute watu wa kariba yako au utengeneze hobby ambazo zitakupa marafiki. Kama ni mtoto wa kiume, mpira, pombe na sex zitakupa watu wengi ila kama unataka discussions za Elon Musk, hapo wabongo wengi utawakosa

Lakini usisahau hayo maisha yana upweke ila yapo peaceful sana,

ukishaanza karibisha marafiki na haupo socially active bhasi uwe na Moyo wa kupambana na dissapointments, unafki, usnitch etc

ila kama unataka watu bhasi waweke kwenye magroup tofauti tofauti kama watu wa kampani, workmates, wa kupiga nao story, watu mnaoshare interest au common vision etc

Hii itakusaidia kujua lipi utashea na kuficha kwa baadhi ya watu kutokana na uzito wao kwako kwa sababu kila info unayowapa watu ni aidha wataipuuzia au wataitumia kukuinua au kukuangusha. Kuwa makini..

Mengine ni yako mkuu maana yawezekana mzizi wa tatizo ukawa ni mzito kuliko hizi general comments tunazotoa hivyo ni wewe tu waweza kujiokoa nao kama hali yako inahusiana na past au hali yako binafsi
 
Katika maisha yangu yote sijawahi kuwa na marafiki,na sipendi kabisa masuala ya marafiki,hata nikipata tatizo sina rafiki wa kumwambia mtu pekee ninayeweza kumwambia ni mama tu.

Lakini pia si mtu mwepesi wakueleza hisia ama changamoto zangu kirahisi hata kwa mama,huwa namueleza nikiona kabisa hii inaniendea kombo.

Nikikaa na kundi la vijana wenzangu huwa nakuwa msikilizaji tu tena kwa muda flani tu kisha naondoka zangu.

Napenda kujitenga sana na ninaweza kukaa Siku nzima peke yangu bila taabu yoyote ile,nikitumia muda huo kufanya kazi zangu Za kiofisi au nikifanya coding ama kufanya simulation za sakiti mbalimbali kama nipo nje ya majukumu ya kitabibu.

Nikiona mtu anaanza kunizoea huwa namkwepa haraka sana maana sipendi mazoea na watu.

Sehemu ninayoishi wapangaji wenzangu inaweza pita miezi 2 hatuja onana.

Sipendi kabisa kwenda katika matukio ya sherehe na hata ikiwa ni lazima huwa nakuwa mtu wakujitenga sana maana Mara nyingi huwa siambatani na mtu kabisa.

Sipendi kupiga piga picha hovyo kabisa. Napenda sana familia hapo ndio nadhani ni marafiki pekee naweza kudumu não japo sina família.

Japo kuna wakati huwa nakuwa mpweke mno hasa nisipokuwa na na kazi ya kufanya ,hivyo huwa najitahidi kuhakikisha nakuwa na kazi Ya kufanya kila Siku.

Mimi napambana kivyangu na mambo yangu sipendi kumshirikisha mtu kabisa ,ila huwa nakuwa na hisia yakumshirikisha mke tu lakini sina.

Ninaamini kwamba kuwa na marafiki na kujichanganya sana na watu ni njia rahisi ya mimi kujiletee matatizo.

Nafikiria kuoa ili kuepukana na hali hii nadhani itanisaidia.
Ulishawah kujaribu Kujiunga CHAPUTA, vipi kupanda mnazi, Ebu jaribu huku mkuu
 
Rule of thumb ni kwamba, kama unajisikia vibaya kuhusu hali unayopitia, basi inakudhuru. Na kinyume chake ni kweli vile vile.

N
Rule of thumb ni kwamba, kama unajisikia vibaya kuhusu hali unayopitia, basi inakudhuru. Na kinyume chake ni kweli vile vile.

Nenda kwa psychologist
Shida siamini watu kabisa ndio maana najitenga sana,yaani hata kwenye matukio sijawahi kuambatana na mtu kabisa huwa nafikiria kwenda na wanangu bad huwa wanakuwa shule Mara nyingi maana wanasoma boarding
 
Back
Top Bottom