Hii hali tunaweza kuielezea vipi?

Hii hali tunaweza kuielezea vipi?

Etugrul Bey

JF-Expert Member
Joined
Aug 6, 2020
Posts
6,514
Reaction score
15,247
Habari zenu members.

Kuna hali Fulani ambayo ipo,kwamba waeza kutana na mtu lkn bila sababu yoyote ukajikuta unamkubali,mnaenda Sawa na mnajikuta kana kwamba mmefahamiana siku nyingi,mkikutana mnasalimiana vizuri na mnaweza tengeneza connection kirahisi Tu.

Lakini kinyume chake kuna mtu unakutana nae,Bila sababu yoyote ya msingi unajikuta Tu yaani haumkubali hata kidogo,hata kuzoeana tabu,unajiuliza hata hajakufanyia kitu chochote kibaya lakini yani inatokea Tu.

Niliwahi sikia kuwa Kwa nadharia ya kidini kuwa,zile roho ambazo baada ya kuumbwa zliikiwa pamoja au majirani huwa huku duniani zikikutana huwa zinaenda Sawa Kwa maana zilikuwa na back ground moja na zile ambazo haziivi hazikuwahi kuwa pamoja Kwa maani zilikuwa mbali mbali.

Bila Shaka hata wewe msomaji ushawahi msikia mtu anasema,mi Fulani simpendi hata kidogo,ingawa hajawahi kumfanyia chochote kibaya,ebu tupanuane mawazo hapa.

Ni hayo tu.
 
Unaonekana una uchawa. Sasa kuna watu ukijipendekeza mnaelewana ila kuna watu wakigundua wewe ni chawa wanakupotezea. NI HAYO TU.
 
Nahisi roho yangu ilikuwa ya jasusi muuaji kabla kuja kwangu maana kila ninaekutana nae namchukia hapo hapo.
 
Back
Top Bottom