Hii imekaaje wapendwa

Yaani hiyo ni mfano mbaya kwa jamii, maza house alipaswa kutoa onyo kali ili iwe fundisho kwa watu wenye tabia kama hiyo na hao wahusika ili wasirudie tena huo ufenenge wao. Ucheka na nyani utavuna mabua. NDOA NA IHESHIMIWE

Sawabho, Sio kuvuna mabua tu, UTALALA NJAA
 
Hahahaaa imekaa vyema susy ukimkuta mwenye mali mwenye hasira anaondoka na sikio lako moja. Ni mchezo hatari sana huu

Uhakikishe unavaa bukta ndani, maana timbwili hilo!
 
nilikuwa naziona sana pale mabibo hostel......!

jamaa anakaa na mwanamke semester moja,semester inayofuata the same woman anakuwa na rafiki wa jamaa....

halafu THEY LIVE HAPPILY THREE OF THEM!....

hasa hasa wale jamaa wa MUHIMBILI WALE.....
 
Dena asante kwa majibu....

Na nafikiri ni kweli huyo mwenye mume aliyefanyiwa bday, alikuwa hajui kama ex-wa mumewe ndo kaandaa hiyo sherehe; otherwise inakuwa ngumu kuamini kabisa, unakubali kabisa mume wako aaandaliwe sherehe..eti na ex-wake???!!! Hapana, hiyo inakataa kuingia akilini...

Kwangu mimi naiona haijakaa vizuri,...tena mume wa mwaandaa sherehe hayupo, hapo kuna utata!!! Kuna dalili za kukumbushia enzi zao....!!!!
 
nilikuwa naziona sana pale mabibo hostel......!

jamaa anakaa na mwanamke semester moja,semester inayofuata the same woman anakuwa na rafiki wa jamaa....

halafu THEY LIVE HAPPILY THREE OF THEM!....

hasa hasa wale jamaa wa MUHIMBILI WALE.....

Ila ngumu mtumishi hii kuishi hivyo hapana aiseee
 
Hiyo red nimekusoma na ni ukweli kabisa eti wengine husema kwani tuliachana kwa ugomvi mara visingizio kibao ila lakini tukikutana kusalimiana ruksa eti DC au nayo noma??

Kukuna ni jambo jingine kwani hiyo ni chance event (kama hakuna mawasiliano ya awali). Yaani ni probability kwamba mnaweza kukutana au la ambayo si kubwa sana. Ila kama mnakaa mnapanga kukutana na kufanyiana parties hayo ndiyo yanaleta mashaka.

Kusalimiana ni uungwana na hakuna dhambi hapo. Ila mkianza kutekenyana kwenye viganja ndipo tunawatilia mashaka kwama mnajizuga na kujidanganywa badala ya kuwadanya wenzi wenu na umma wote!
 

Maty wangu,

Upo wewe? Mwenzio nimelisusa hilo jina la babu...Sitaki mimi, nisijekuonekana na mimi ni mlozi kama huyo babu wa Loliondo.
:focus:

Maty, Maty.....Unataka niamini kwamba wanawake hawajui maana ya kuachana?
 
Duh, hii kali.. lakini imeonyesha uungwana kwa watu walioachana kistaarabu bila kutupiana mayai mabovu.. changamoto ni kwa huyo mke wake, awe serious ataibiwa!
True, awe makini. Baba alimuagaje mama?????
 
huyo ni mwizi wa mapenzi kama wezi wengine tuliowazoea hakua la zaidi hapo anajipanga kufisadi ndoa ya mtu

Naku-support ndugu yangu!
Binafsi sioni mantiki ya mtu uliyeachana nae miaka kumi iliyopita ana familia yake na wewe una familia yako eti leo unamfanyia sherehe ya siku yake ya kuzaliwa?unataka kuonyesha nini?kuna vitu vingapi ambavyo ni vya muhimu kwako na familia yako kwa sasa ambavyo ungefanya?aah hapo naona uzushi tu hakuna lolote na wala si bure!!
 
Pia tukumbuke pamoja na kugombana kama wapenzi maisha bado yanaendelea, ipo siku mtakutana. Hakuna haja ya kuwekeana visasi mpaka mnavuana na c***i mlizopeana zawadi wakati mkiwa kwenye good terms


Na kumfanyia sherehe kabisaa
Hiyo kwangu ngumu.
Tukikutana kwanza sina story nyingi nae, just salaam na mawili matatu kila mtu anashika 50 zake.
 
Jamani haya mambo ya besidei ni kama utamaduni wa magharibi msimlaumu sana mke aliyesahau pengina katika kukua kwake hakuwa anaona hivyo vitu wala kujua umuhimu wake,sasa sio rahisi leo tu kaolewa aanze tu ghafla ku care kuhusu besidei.
 
 
Maty wangu,

Upo wewe? Mwenzio nimelisusa hilo jina la babu...Sitaki mimi, nisijekuonekana na mimi ni mlozi kama huyo babu wa Loliondo.
:focus:

Maty, Maty.....Unataka niamini kwamba wanawake hawajui maana ya kuachana?

babu bora umetambua kwamba babu wa loliondo ni mlozi asee wewe unastahili sana, wanawake tunajua maana ya kuachana ila wababa wasumbufu sana tena sana unakuta hata alikuacha mwenyewe lakini baada ya muda eti................ ee mwenyezi mungu tujalie neema
 
Mkwewe hana tizo. Kwanza ile si birth day kama wengi wetu tujidanganyavyo. Mara nyingi huwa ni Birth Date. Alafu haina uhusiano na ndoa. La msingi huyo mme anaonekana wazi kuwa bado anaendelea kumega kwa EX wake
 

Maty...Maty...Hebu basi acha kuniongezea huzuni mwenzio!

Kwa hiyo wakisumbua sana mnawakubali waendelee kuwachakachua? Hivi kwani hamjui kuwa wanaume wanapenda kuonja onja? Hamkuelezwa hivyo na bibi zenu?

Mwanamume wa kweli angefurahi kuwa na wake kama 5 hivi.. Mmoja anaishi kwenye wallet, mwingine anakwenda kumwona siku hiyo (date) na watatu wanakuwa kwenyereserve list huko home. Aki-miss date anaanza na yule wa kwenye wallet...Ikishindikana anaangalia reserve list.

Ningewambia shauri yenu..ila nawaonea huruma. Wengine ni wadogo zangu, wajukuu, shemeji, wanangu, mama ana shangazi zangu!
 


Hiyo kweli wanaume ndo zao hizo tena akishaonja anaanza madharau kama alikuwa anakupigia simu ujue kazi imehamia kwako halow darling mbona kimya utasikia "Kazi nyingi sana" Hebu nipigie baadae kidogo niko kwenye kikao wakati mwanzoni alikuwa anapiga sijui vikao havikuwepo ha ha ha ha wanaume bana nawapenda kweli kwa mambo yenu
 
hii ya kuwa marafiki na ex mwenzenu ilinishinda kabisa, ni drama tu mda wowote mnamegana, hasa kama uliachwa bado unapenda ni ngumu kushinda majaribu

sitaki kusikia habari ya ex kwenye mahusiano yangu kabisa, huyo mama anaibiwa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…