Pre GE2025 Hii kali: Rais Samia awaagiza JUMIKITA 'kuchuja' maudhui ya mtandaoni tena katika Kongamano la Sekta ya Habari!

Pre GE2025 Hii kali: Rais Samia awaagiza JUMIKITA 'kuchuja' maudhui ya mtandaoni tena katika Kongamano la Sekta ya Habari!

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)

Cute Wife

JF-Expert Member
Joined
Nov 17, 2023
Posts
1,906
Reaction score
5,000
Jumikita kwa wale msiyojua kirefu chake ni Jumuiya ya Wanahabari wa Mitandao ya Kijamii, wanawakilisha wanahabari wote wa mtandaoni nchini. Rais Samia anawasifia na kuwaambia mwende mkachuje yanayosemwa mtandaoni watu waseime wanayoyataka na nyie mnakenua na kuinama kuonesha mnashukuru na kupokea maagizo!

Mnajielewa kweli nyie? Yaani watu wanapigania uhuru wa vyombo vya habari halafu nyie mnakuwa sehemu ya kukwamisha juhudi hizi kwa kuungana na Raisi!

Eti chujeni wasiende kusema wanayotaka! Kutwa kuchwa ni uozo kila sehemu, serikali inanuka wizi na ubadhirifu, halafu unataka watu wote wawe kama hao nyuki wako akina Lucas Mwashambwa kusifia ovyo kama vile hawana vichwa!

Jumikita hamsathili kuwepo, nyinyi ndio mtakuwa wa kwanza kukandia wenzenu wanaotoa taarifa kwa maslahi ya umma. Ni kweli sasa hivi mazingira yamebadilika, kidogo ukatili umepungua, lakini uminywaji wa haki uko pale pale.

Rais Samia ungekuwa na mshauri mzuri hata mmoja leo ilikuwa ni nafasi nzuri ya kumaliza utata kuhusu suala la X na kuonesha kweli unaunga mkono suala la uhuru wa vyombo vya habari.

Akaitaja JF na Tanzania Leaks ili tu afikishe maagizo yake vizuri ya vyombo vya mtandaoni kufanyiwa censorship!

Hapa mama (kama anavyokuita Lucas Mwashambwa) unazidi kuchemka, unazidi kuharibu, mama ametukwamisha!



"Kwanza nawashukuru (JUMIKITA) kwa kazi nzuri mnayoifanya lakini mnawajibu wa kujichuja huko kuhakikisha.... Uhuru wa mawazo upo, mtu anaongea anayotaka lakini nyinyi mliofanya jumuiya kuangalia mawasilianano huko (chini) muweze kuchuja sasa na kuwaelewesha wale wengine wanaoandika wanavyotaka. Tutumie vyombo vyetu

"Kujenga nchi yetu na si kuboa. Watu wakisoma nje tunajibomoa wenyewe na sifa yetu Tanazania wanayoijua hawatuelewi. Unajua mimi nikienda nje na kufika kwenye mkutano na kukutana na wenzangu unasingia “Hongera sana Samia..” unajiuliza mh hongera za nini? Mngekuja huku kwetu mkasikia wanayosema? Lakini kumbe nje wanayaona na wanayapongeza sana, lakini njoo Tanzania!

"Kwahiyo JUMIKITA wanangu mkafanye kazi nzuri. Nawashukuru sana kwamba Makongamano haya yanawapa fursa ya kujitathmini je tunafanya vyema? Tumefika wapi? Tunakwendaje? Kwahiyo na katika vikundi vyenu vidogo vidogo hivyo hebu kakaeni kwenyewe na mjifanyie tathmini na kuona je kazi yetu inaleta matokeo Chanya au hasi. Hasi hayaachi kuwepi lakini yanaathiri kiasi gani katika nchi yetu? Nendeni mkafanye hiyo kazi lakini nawashukuru kwa kazi mnayoifanya ya kusambaza habari."
- Rais Samia
 
Mheshimiwa Rais wetu mpendwa na Jemedari wetu kipenzi cha watanzania Daktari Samia Suluhu Hasssan,yupo sahihi kabisa maana kuna watu unakuta anaandika habari ya kizushi na uongo pasipo kuweka ushahidi wa aina yoyote ile,wala nyaraka ya aina yoyote ile kuthibitisha madai yake.sasa hii kiuandishi haikubaliki maana inakuwa inamchafua mtu au taasisi au serikali bila ushahidi wowote ule.

Wengine unakuta wanaandika tu na kuleta taharuki kwa watu kwa sababu ya chuki tu binafsi .kwa hiyo ni kweli ni lazima sisi watumiaji wa mitandao tuhakikishe habari zetu zinakuwa na uthibitisho badala ya kuchafuana na kuleta habari za uongo na uzushi tu zisizo na ukweli wa aina yoyote ile.
 
Maneno na mawazo ya Rais Samia yana lingana na yale ninayo yasema hapa JF mara kwa mara. Kwamba, 'hatuwezi kujenga kwa kujibomoa n.k'

Naamini ile barua yangu imefika pahala panapo stahili.

Najua fika siko peke yangu, ila nataka kuamini nimechangia katika mtazamo wa Rais wetu.

Kiunagaubaga nilsema hivi...Najinukuu

"The Media Services Act, 2016 and the Electronic and Postal Communications(Online Content) Regulations, 2020 imetoa framework ambazo hatua zinaweza kuchukuliwa dhidi ya matamshi ya chuki na maudhui ambayo yanaweza kuchochea machafuko ya Umma.

Sheria hizi ni muhimu katika kuchangia Ustawi wa Jamii na Taifa letu kwa Ujumla.

Kwa taarifa zaidi soma:

Barua ya Wazi kwa Dkt. Dorothy Gwajima na Nape Nnauye

 
Kama kungekuwa na uwezekano 2025 tukafanya mabadiliko walao nuru ingetuzukia.
 
Mheshimiwa Rais wetu mpendwa na Jemedari wetu kipenzi cha watanzania Daktari Samia Suluhu Hasssan,yupo sahihi kabisa maana kuna watu unakuta anaandika habari ya kizushi na uongo pasipo kuweka ushahidi wa aina yoyote ile,wala nyaraka ya aina yoyote ile kuthibitisha madai yake.sasa hii kiuandishi haikubaliki maana inakuwa inamchafua mtu au taasisi au serikali bila ushahidi wowote ule.

Wengine unakuta wanaandika tu na kuleta taharuki kwa watu kwa sababu ya chuki tu binafsi .kwa hiyo ni kweli ni lazima sisi watumiaji wa mitandao tuhakikishe habari zetu zinakuwa na uthibitisho badala ya kuchafuana na kuleta habari za uongo na uzushi tu zisizo na ukweli wa aina yoyote ile.
CC: ChoiceVariable The Sunk Cost Fallacy 2 The Sunk Cost Fallacy benzemah Erythrocyte Sexless gearbox deblabant G4N CHADEMA and company
, Ladies and Gentlemen.

Naogopa kujaza server za JF.

Mnahusishwa.
 
CC: ChoiceVariable The Sunk Cost Fallacy 2 The Sunk Cost Fallacy benzemah Erythrocyte Sexless gearbox deblabant G4N CHADEMA and company
, Ladies and Gentlemen.

Naogopa kujaza server za JF.

Mnahusishwa.
Kwahiyo kuna Samia wawili. Yupo Samia wa majukwaani ambaye anasisitiza uhuru wa habar., Halafu yupo Samia wa nafsini ambaye hataki uhuru wa habari na anaiagiza jumikata kuchuja habari!


Na huyu Samia wa nafsini ndiye mwenye nguvu zaidi kuliko Samia wa majukwaani
 
..anayebomoa ni Mama Abduli na Ccm yake, sio waandishi wa habari, au wananchi wa kawaida.

..vilevile maisha ni magumu kwa wananchi wa kawaida. Vijana wetu hawana ajira. Sijui ni kwanini Mama Abduli anaamini anastahili kupongezwa, au kusifiwa.
 
Kwahiyo kuna Samia wawili. Yupo Samia wa majukwaani ambaye anasisitiza uhuru wa habar., Halafu yupo Samia wa nafsini ambaye hataki uhuru wa habari na anaiagiza jumikata kuchuja habari!


Na huyu Samia wa nafsini ndiye mwenye nguvu zaidi kuliko Samia wa majukwaani
Kikuu ni kwamba mmehusishwa.

Mchujo unakuja.

Haya.
 
Back
Top Bottom