Ukiichunguza misema/methali za kiswahili kila moja ina nyingine ambayo ni oppositi yake kwa mfano mvumilivu hula mbivu opposite yake ni ngoja huumiza matumbo, polepole ndio mwendo opposite yake ni chelewa chelewa utakuta mwana si wako, mbio za sakafuni huishia ukingoni opposite yake ni mgagaa na upwa hali wali mkavu...
Kwahiyo unaangalia tu mazingira gani unahitaji methali gani na kuitumia. Kama ina tija au lah inategemea na jinsi mtumiaji atakavyokuwa makini kwenye kuchagua mazingira muafaka...
na hao tuliowapa dhamana ya kuongoza upatikanaji wa maendeleo hayo kwa haraka wenyewe wanaharakisha kujipatia maendeleo yao tena kwa harakaharaka na kutumia shortcut (ufisadi)..isingekuwa hii harakaharaka yao ya kutaka maendeleo yao binafsi kwa haraka pengine tungekuwa tupo mbali sana kimaendeleo..Mkuu, nchi ipo nyuma sana kiuchumi, kwa nini tusifanye haraka kuiendeleza?
Asante mkuu kwa mchango wako. Nchi yetu ina wanafalsafa wengi kama ZeMarcopolo na wengineo, nafikiri ifike mahali tu tuwe na misemo ambayo itakuwa ni positive zaidi yenye kuhamasisha kuleta maendeleo ya Taifa letu changa lenye zaidi ya miaka arobaini.