Hii ndio (CV) Wasifu ya Nape Moses Nnauye

Hii ndio (CV) Wasifu ya Nape Moses Nnauye

Kumekuwepo na habari ambayo inavumishwa katika mitandao ya kijamii hasa hapa Jamiiforums kuhusu Elimu ya Katibu wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa, Itikati na Uenezi, Ndugu Nape Moses Nnauye. Taarifa hiyo kwa kiasi kikubwa inapotosha na kueleza yale ambayo si sahihi kuhusiana na CV ya Kiongozi huyo wa Chama cha Mapinduzi; Kutokana na Hilo, nimeona ni jambo la busara kuwasaidia wanajamvi kwa kuwapa CV iliyo sahihi ya Nape Moses Nnauye kama ifuatavyo;


  • Kati ya mwaka 1987-1989 alianza elimu yake ya msingi katika shule ya Msingi Mwanga-iliyopo Iramba Singida (ambapo alianza darasa la 1 mpaka 3)
  • Mwaka 1989-1993 aliendelea na kumalizia elimu ya msingi katika shule ya Bukumbi iliyopo misungwi Mwanza.(ambako alikuwa ni kati ya wanafunzi watatu “3” kati ya 120 waliochaguliwa sekondari.
  • Mwaka 1994-1995 alianza elimu ya Sekondari katika shule ya kutwa ya Ngudu Sekondari.(ambapo alisoma kidato cha kwanza mpaka cha pili)
  • Mwaka 1995-1997 aliendelea na elimu ya sekondari katika shule ya Bweni ya Sekondari Nsumba iliyopo Mwanza (ambapo aliendelea kidato cha pili mpaka cha nne)
  • Mwaka 1998-2000 alisoma elimu ya juu ya sekondari (advanced level), mchepuo wa EGM na kuhitimu Butimba TTC
  • Mwaka 2001-2002 alisoma Diploma ya sayansi ya jamii katika Chuo Cha sayansi ya Jamii-Kivukoni.
  • Mwaka 2002-2003 alisomea Diploma ya Diplomasia na uhusiano wa Kimataifa –Chuo cha Diplomasia Dar es salaam.
  • Mwaka 2005-2008 alisomea digrii ya Saikolojia, Lugha na Habari katika Chuo Kikuu cha Bangalore-India
  • Mwaka 2009-2010 alisoma digrii ya pili ya utawala (Masters in Public Administration-MPA) katika chuo cha Mzumbe.
NB: Ndugu Nape Nnauye akiwa Kivukoni aliandika “thesis” iliyohusu ; VIKWAZO VINAVYOZUIA VIJANA KUSHIRIKI KATIKA SIASA. Na pia akiwa Mzumbe University aliandika kuhusu ; SABABU ZINAZOCHANGIA USHIRIKI WA WAPIGAKURA (ni ipi sababu ya kutojitokeza wapigakura siku ya Kura)

Tunaomba jina halisi na ukoo wa baba yake pia na kabila la baba yake pls.
 
Alizaliwa mwaka gani????.

Pia mim naona hii sio CV ni Kumbukumbu zake kimasomo tu, hata hvyo hazijakamilika kwa kua hujaweka Ufaulu wa kila Ngazi ya Elimu... Halafu kwa nini sasa na sio siku kadhaa nyuma? Usitutoe kwenye Reli acha tufike Kigoma
 
Mkuu kwa matokeo hayo ni lazima aende kusoma masomo ya Advance chuo cha Ualimu kwa kuwa kule kuna walimu wengi. hivi huyo angeenda shule yenye walimu 10 unadhani wangeweza kufanya kitu?


Tuanzie hapa form 4

NAPE NNAUYE
SEX M DIV IV PTS 29 KISW D HIST D GEOG D ENGL F B/MATH F BIOL D CHEM D PHY D CIV F
-----------------------
JOHN MNYIKA
SEX M DIV I PTS 7 PHY A CHEM A BIOL A CIV A ENGL A GEOG A HIST A B/MATH A KISW A B/KNOW A
 
Nchi hii inahitaji kusoma sana hao wasomi wenyewe hawana lolote wanalolifanya
 
Mwaka 2002-2003 nilikuwa Centre for Foreign Relations & Diplomacy. Sikuwahi kumwona Nape, labda kama alisomea nyumbani.
 
Nchi hii inahitaji kusoma sana hao wasomi wenyewe hawana lolote wanalolifanya
Mbona hueleweki agwe?Kama unafikiri kusoma hakuna maana hebu jilinganishe wewe kilaza na waliohudhuria madarasa.Au kwa maneno mengine kama elimu haina maana basi jaribu ujinga.
 
Anaomba kazi? Hii CV ya nini? Hizi diploma za mwaka mmoja mmoja Duhhhh.

mmmm kumbe na wew umeziona Diploma mwaka mmoja duuuuuu:redfaces::redfaces::redfaces::redfaces::redfaces: Izo ni certificate cio diploma uyo alioandika kaamua kurefusha izo shule ili Cv ikue
 
...kuwa na baba maskini ni mipango ya Mungu ila kuwa na baba mkwe maskini ni ujinga wako mwenyewe.....
 
Shule za kuunga unga kama super glue!

Nadhani tumpongeze pia tumchukulie mfano kwa wadogo zetu ambao wanafeli au wanapata alama za chini wanakata tamaa na kuona ndio basi kumbe kuna njia kibao unatakiwa kupita mpaka kufika juu
 
Magumashi kama ilivyo Ph.D ya Nchimbi na Masters ya Lukuvi. Nchi imefika mahali watu wameanza kuinajisi elimu. Tuendako ni kubaya zaidi. Malengo ya Open University yalikuwa mazuri, bahati mbaya wanasiasa wameona ndio mahali pa kubadili titles zao. Tusubiri...
 
Back
Top Bottom