Hii ndio (CV) Wasifu ya Nape Moses Nnauye

Hii ndio (CV) Wasifu ya Nape Moses Nnauye

Ushauri kwa vijana,

Hii mijadala ya elimu ya Nape na Mnyika ina mafundisho mengi sana kwa vijana kama mnataka kujifunza. Wekeni siasa pembeni na jifunzeni jinsi maisha yanavyobadilika na jinsi ambavyo kushindwa jambo moja sio mwisho wa mafanikio.

Hapa inaonyesha wazi Mnyika alikuwa na uwezo mkubwa sana shuleni na bado ana uwezo mkubwa maana hata hoja zake nyingi zina mshiko. Lakini inakuwaje kwa miaka yote hiyo kashindwa kumalizia hako kadegree ambako kwa uwezo wa Mnyika ni kadogo sana? Sidhani kama muda ndio tatizo pekee, labda hata hakuona umuhimu, kitu ambacho mimi nakielewa maana hata akina BIll Gates, Jobs hawakuona umuhimu wa kubaki vyuoni wakati tayari kichwani walikuwa na uwezo wa kufanya yale waliyotaka kufanya baada ya vyuo.

Tukija kwa Nape ni wazi uwezo wake ulikuwa mdogo, hakuwa na credits za kuingia A-level. Lakini kijana Nape hakulala chini na kuanza kulia au kulalamika, badala yake aliamua kujiendeleza kwa kuunga uunga elimu. Mwisho wa siku amesoma mpaka sasa ana masters yake kwenye Public Administration. Hili ni fundisho hata kwa vijana wote waliofeli mwaka huu, tumieni elimu hiyo ya Nape kama hamasa ya kwamba kama Nape ameweza kwanini na nyie msiweze? Bila kujali umepata sifuri au division four. Elimu ya karne ya 21 bado kijana una nafasi ya kuweza kusoma, kujiendeleza na mpaka hata kuwa profesa ukitaka. Uamuzi ni wako, kuamua kupambana au kuishia kucheka wengine. Ukipata F si unarudia?

Sisi sote tuliosoma zamani tunawajua watu wengi sana ambao form six walipata zero hata ya F zote lakini wengine sasa ni maprofesa, madaktari, wachumi nk. Kama mtu anabisha, awaangalie watu waliokuwa wanasoma PCB miaka ya 80. Utawakuta wengi pamoja na kufeli form six lakini leo wako mbali sana. Walichofanya, walijiendeleza na kufeli form six haikuwa sababu ya kuwakwamisha. Kuna jamaa mmoja juzi juzi akaniambia utani akimsema msomi mmoja maarufu wa sheria TZ kwamba alipata division zero PCB Tabora. Nilishutuka sana, sikuamini. Lakini ukweli ndio huo, kupata four au zero sio mwisho wa elimu.

Binafsi kuna vijana nimewahi kuwasaidia ambao form four walitoka na points kama hizo za Nape. Through kuwashauri na kuwasaidia, leo hii wamemaliza degree zao na wana mafanikio kwenye kazi zao.

Sawa tutumie siasa kuchekana kama kujifurahisha, lakini kwenye mioyo yetu tutambue hili ni somo tosha. Kufeli jambo mara moja sio mwisho wa dunia. Badala yake amka, jipukute na anza safari tena kwa speed hata kubwa kuliko mara ya kwanza.

Wakati wewe unacheka na kupoteza muda, wenzako wanasonga mbele.
Mawazo haya ni bora tena yenye kutaja uhalisia..,yanatoa somo na fundisho kwa walio wengi (wenye kufikiri) natamani laiti kama haya yangelieleweka katika vichwa vya wengi miongoni mwa vijana wetu.

Lakini pamoja na kuandika hapa ni vyema habari hii,.ingeanzishiwa thread yake binafsi kushauri..,kama hilo linawezekana lifanye.,tena lifanye hivi sasa. Maneno haya uliyoyaandika yanahitajika mno kwa wakati huu ambao vijana wamepata matokeo mabovu kupindukia na kuwafanya wao na jamaa zao kuwa frustrated wote wakitaka kumnyooshea kidole mwingine.,kunyoosheana vidole ambako sio suluhisho na wala hakutasaidia kitu.

Naomba nieleze mtazamo wangu kwako..,nakutazama kuwa wewe ni mtu unayestahili kuitwa great thinker tena aliyetofauti na wa kipekee humu jamvini.

Maneno mazuri ni sadaka nami nimeipokea sadaka yako, ubarikiwe...!
 
Pleaseeeee tunaomba utuambie matokeo Yale ya o level na A level, aliscore division ngapi? Kama alivyofanya mnyika.......Ndio ombi letu
 
Unashangaa hayo kuna mtu Ana Div 4 ya 31 na ni mwenyekiti wa Chama

Unamshangaa mwenye four ya 31 na kuwa mwenyekiti wa chama? Kuna huyu Rais wetu, ana Gentleman ya UDSM, mbona hushangai kuongoza maprofessor? Ndio shida ya akili ndogo kuongoza akili kubwa na ndio maana ya kuuliza "Eti nani hajui kuwa Dar hakuna maji?" Yaani anajua, halafu anauliza, sijui alikuwa anataka nini? We have lost 10 years (2005 - 2015) hakuna kitu tumefanya, hata sisi ambao hatukumpigia kura, tunamia kutokana na akili za wajinga wachache. Stupid!!!!
 
Guys miaka hiyo ambayo wengine tulisoma pande za Rocky city, Butimba TTC ilikuwa inatumika kama kituo cha kufanyia mitihani watu wa A level so its not something new kwani kuna hata close friends of mine walitumia kituo hicho kufanyia mitihani yao ya A level (kipindi hicho mama Gaudencia Kabaka - Waziri- alikuwa mkuu wa chuo). Inawezekana hata Ndg Nape naye akawa ni mmoja wa watu walio tumia kituo hicho.
 
Guys miaka hiyo ambayo wengine tulisoma pande za Rocky city, Butimba TTC ilikuwa inatumika kama kituo cha kufanyia mitihani watu wa A level so its not something new kwani kuna hata close friends of mine walitumia kituo hicho kufanyia mitihani yao ya A level (kipindi hicho mama Gaudencia Kabaka - Waziri- alikuwa mkuu wa chuo). Inawezekana hata Ndg Nape naye akawa ni mmoja wa watu walio tumia kituo hicho.

mangwela,

Wewe unaonekana huelewi kinachozungumzwa hapa.

Tuliopitia shule tunajua nini maana ya PC na SC. Private Candidate Centre haimfanyi mtu kuhitimu combination ya EGM hata siku moja. Pale unapojisajili kwa ajili ya mitihani iwe ni ya F4,F6 au QT kwenye kituo(centre)haikufanyi kuwa mwanafunzi wa kituo. Unaweza ukawa unasomea Dar na ukajisajili kufanyia Mitihani yako Butimba TTC. Itakuwa ni upuuzi kuwaambia watu kuwa umehitimu F6 Butimba TTC unless hujui unachozungumza. Nnape anajua Butimba TTC HAKUNA ELIMU YA A LEVEL(F6) inayotolewa!!!

Acha kutetea upuuzi na ujinga wa viongozi wababaishaji wa CCM kama Nnape.
 
mangwela, wewe unaonekana huelewi kinachozungumzwa hapa. Tuliopitia shule tunajua nini maana ya pc na sc. Private candidate centre haimfanyi mtu kuhitimu combination ya egm hata siku moja. Pale unapojisajili kwa ajili ya mitihani iwe ni ya f4,f6 au qt kwenye kituo(centre)haikufanyi kuwa mwanafunzi wa kituo. Unaweza ukawa unasomea dar na ukajisajili kufanyia mitihani yako butimba ttc. Itakuwa ni upuuzi kuwaambia watu kuwa umehitimu f6 butimba ttc unless hujui unachozungumza. Nnape anajua butimba ttc hakuna elimu ya a level(f6) inayotolewa!!! Acha kutetea upuuzi na ujinga wa viongozi wababaishaji wa ccm kama nnape.
mkuu uko sahihi uelewa wa watu wengine inabidi tuingie ndani ya akili zao ndio watajua nini tunaongelea hapa
 
Kumekuwepo na habari ambayo inavumishwa katika mitandao ya kijamii hasa hapa Jamiiforums kuhusu Elimu ya Katibu wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa, Itikati na Uenezi, Ndugu Nape Moses Nnauye. Taarifa hiyo kwa kiasi kikubwa inapotosha na kueleza yale ambayo si sahihi kuhusiana na CV ya Kiongozi huyo wa Chama cha Mapinduzi; Kutokana na Hilo, nimeona ni jambo la busara kuwasaidia wanajamvi kwa kuwapa CV iliyo sahihi ya Nape Moses Nnauye kama ifuatavyo;

  • Kati ya mwaka 1987-1989 alianza elimu yake ya msingi katika shule ya Msingi Mwanga-iliyopo Iramba Singida (ambapo alianza darasa la 1 mpaka 3)
  • Mwaka 1989-1993 aliendelea na kumalizia elimu ya msingi katika shule ya Bukumbi iliyopo misungwi Mwanza.(ambako alikuwa ni kati ya wanafunzi watatu “3” kati ya 120 waliochaguliwa sekondari.
  • Mwaka 1994-1995 alianza elimu ya Sekondari katika shule ya kutwa ya Ngudu Sekondari.(ambapo alisoma kidato cha kwanza mpaka cha pili)
  • Mwaka 1995-1997 aliendelea na elimu ya sekondari katika shule ya Bweni ya Sekondari Nsumba iliyopo Mwanza (ambapo aliendelea kidato cha pili mpaka cha nne)
  • Mwaka 1998-2000 alisoma elimu ya juu ya sekondari (advanced level), mchepuo wa EGM na kuhitimu Butimba TTC
  • Mwaka 2001-2002 alisoma Diploma ya sayansi ya jamii katika Chuo Cha sayansi ya Jamii-Kivukoni.
  • Mwaka 2002-2003 alisomea Diploma ya Diplomasia na uhusiano wa Kimataifa –Chuo cha Diplomasia Dar es salaam.
  • Mwaka 2005-2008 alisomea digrii ya Saikolojia, Lugha na Habari katika Chuo Kikuu cha Bangalore-India
  • Mwaka 2009-2010 alisoma digrii ya pili ya utawala (Masters in Public Administration-MPA) katika chuo cha Mzumbe
NB: Ndugu Nape Nnauye akiwa Kivukoni aliandika “thesis” iliyohusu ; VIKWAZO VINAVYOZUIA VIJANA KUSHIRIKI KATIKA SIASA. Na pia akiwa Mzumbe University aliandika kuhusu ; SABABU ZINAZOCHANGIA USHIRIKI WA WAPIGAKURA (ni ipi sababu ya kutojitokeza wapigakura siku ya Kura)

kama ni O-Level na A-Level mbona wamemaliza wengi tu?
si unaona hata matokeo ya wadogo zetu wa form 4 mwaka huu???
kusoma sio issue, the point is umetoka na divission ngapi?
una class ipi???
embu na hapa uweke kwa majigambo kama ulivyoweka hiyo CV Japo naona kama nayo ni ya kuunga na super glue.

NAWAZA TU JAMANI.
Hapo kwenye RED wadau si mnajua kwenye kuvuka hivyo vidato kuna mitihani ya michujo?
sasa hapo nahisi kuna namna ndio maana mtu mzima akahama na shule kabisa manake si unajua ile wenzio wanasonga mbele wewe unapiga mark-time?
 
ELIMU YA NAPE NNAUYE.
(nimeitoa JF)

Mwaka 1993 alifeli darasa la saba. Wakati ule jina halali la Nape akiitwa Nahum Nnauye. Waliosoma nae wanakumbuka. Bt akafanyiwa mpango na kupewa jina la Nape Mkumbo Nyagicha mtoto masikini wa Kinyiramba, aliyefaulu lakini familia yake haikuwa na uwezo wa kumsomesha.

Mwaka 1994 Nahum Nnauye akajiunga na shule ya sekondari ya kutwa Ngudu wilayani Kwimba akiwa na jina jipya la Nape. Mwaka 1995 akahamishiwa shule ya Sekondari Nsumba kwa kutumia title ya baba yake Mzee Moses Nnauye.

Mwaka 1997 akafeli form four kwa kupata division four ya point 29 akiwa na D 4, c 1 na F 5. Akareseat mara 2 bila mafanikio pale Butimba TTC ambacho ni kituo cha watahiniwa binafsi. Mwaka 1999 na mwaka 2000.

Akakata tamaa na hatimaye mwaka 2001 akaamua kwenda kusoma cheti cha Uhazili (cert of secretarial services) katika chuo cha Kivukoni. So kabla sijaendelea naomba ieleweke kuwa Nahum Moses Nnauye (Nape) hajawahi kusoma form 5 shule yoyote duniani. Kama anabisha aje hapa tumuulize maswali ya Geography 1 au Ecomics 2 uone atakavyochanganyikiwa. Kwanza hajui kama kuna paper 1 na 2 A.level, atasemaje amesoma A.level?

So akatumia cheti chake cha uhazili kuomba diploma pale chuo cha Diplomasia kurasini. akapata na akaanza kusoma. Mwaka mwaka 2002 akafeli kuendelea na 2nd year baada ya kupata suplimentary 4 ktk masomo 6 aliyokuwa akisoma. So kwa kifupi akadsco. Hivyo naomba ieleweke kuwa huyu jamaa anayejiita Nape hajawahi kutunukiwa diploma yoyote kutoka Chuo cha Diplomasia Kurasini. Kwanza asikidhalilishe chuo maana pale hakuna Diploma ya mwaka mmoja. kama anabisha aapload picha yoyote hapa alipokuwa anatunukiwa hiyo diploma.

Mwaka 2004 akatumia cheti chake cha form four kuomba degree India kwa kusaidiwa na mwandishi mmoja mashuhuri nchini kwa kuwatafutia vyuo vya nje watu waliofeli.

Na akapata kwa masharti ya kusoma miaka minne. Ikumbukwe India ni nchi yenye vyuo vya hovyo sana duniani, na ni miongoni mwa nchi ambazo hata kama una zero unaweza kusoma Bachelor bila matatizo yoyote hadi ukahitimu. Reffer kesi ya Mr.Andekisye, Lecturer aliyefukuzwa kazi Arusha University kwa kusoma elimu feki India. Andekisye aliajiriwa kama mhadhiri wa Marketing na Business Mathematics akidai ana MBA kutoka India.

Bt ilipofuatiliwa ikagundulika ni kweli ana Masters ya MBA bt hajawahi kusoma Bachelor. Alichomoka na Diploma yake ya Ualimu (Mathematics & Physics) kutoka Monduli TTC akaaply Masters India akapata akaenda kujoin. Sasa imagine mtu anatoka Diploma anakwenda Masters sembuse Nape kusoma bachelor?

Nape akapata degree yake fake ya psychology ambayo ndiyo aliyoitumia kuomba masters mzumbe. Na mzumbe hakukabidhi cheti zaidi ya kile cha degree yake ya India.
Kama anabisha aweke vyeti vyake vya o.lel na a.level hapa.

Huyo ndiye Nahum Moses Nnauye anayejiita Nape. Katibu mwenzezi wa Chama cha Mapinduzi CCM na mgombea ubunge ubungo mwaka 2010, wakati ule akijaribu kushindana na Genious John Mnyika aliyepata A 9 O.Level yeye akiwa na D 4 tu.

Achani wendawazimu wa kimawazo na fikra finyu.
Huyu jamaa amejiendeleza vema sana na anastahili pongezi nyingi sana. Kama hayuko vema kiakilia kama unvyoataka tujue asingeweza kufaulu masters pale Mzumbe.
Dr Salim Ahmed Salim na mzee Mwinyi (rais mstaafu) hawakuwahi kusoma Bachelor degree lakini ni moja wa nguli wazuri sana duniani.
Pili, si vema kabisa kuvishusha vyuo vikuu vya India, kwani kuna watu mashuhuri na wenye heshima sana nchini, akiwema Malecela waliosoma huko. Hiyo sijataja wazuoni wengine wengi Duniani. Marekani kuna vyuo bogus zaidi kuliko India.
Bila kujali mwelekeo wetu kisiasa, ni lazim tufike sehemu tufikirie kwa kutumia akili akili.
 
Elimu ya mtu utampima iQ yake.Angalia maongezi yake hotuba zake.Kuna wengine wana vyeti vizuri lakini kichwani hakuna kabisaaaaa.walikuwa wamekwenda shuleni kukremu tu.Wengine baba zao watu wakubwa na wana uwezo kusema make sure mwanangu anapata marks nzuri.Cha msingi ni utaona tu akili yake sasa hivi na utapata jibu huyu kichwani hakuna.Husiangalie vyeti kabisaaaa.Hangalia mchango wake wa kitaaluma kwa jamii.
 
Napita tu,maana umri wangu hauruhusu lkn naelekea kumzidi Nape kitaaluma.Haya jamani majadiliano mema.
 
form 6 huyo alifeli hapo ndio akaamua kwenda kusoma hiyo certificate na sio diploma! huyo kilaza nape wala hana ki2 kichwani!
 
Inaweza kuwa "private candidate" kuna center pale.

Degree za kuunga unga na kazi za kunga unga kutoka katibu muktasi mpaka katibu mwenezi subiri kesho atauuga mpaka waziri au Rais kwani hamjui tanzania yetu watu kwa kuungisha ndio viongozi wetu madokta ukishindwa wa darasani unavarisha mwenyewe kama dokta Lyatonga ? Kwani shida gani Bongo ? kuwa mjanja
 
Achani wendawazimu wa kimawazo na fikra finyu.
Huyu jamaa amejiendeleza vema sana na anastahili pongezi nyingi sana. Kama hayuko vema kiakilia kama unvyoataka tujue asingeweza kufaulu masters pale Mzumbe.
Dr Salim Ahmed Salim na mzee Mwinyi (rais mstaafu) hawakuwahi kusoma Bachelor degree lakini ni moja wa nguli wazuri sana duniani.
Pili, si vema kabisa kuvishusha vyuo vikuu vya India, kwani kuna watu mashuhuri na wenye heshima sana nchini, akiwema Malecela waliosoma huko. Hiyo sijataja wazuoni wengine wengi Duniani. Marekani kuna vyuo bogus zaidi kuliko India.
Bila kujali mwelekeo wetu kisiasa, ni lazim tufike sehemu tufikirie kwa kutumia akili akili.

Mzumbe ni chuo ambacho kinapashwa kujiangali sana na watu hawa wa kuuungaunga. Wapo wengi ambao wamepita Mzumbe na wana Masters lakini ni wahitimu wa ovyo sana . Tunao na tunawajua maana hata thesis wameandikiwa mitahani. na wengi wakishatoka mzumbe sio kwamaba wanakwenda kutumia taaluma zao hizo ila wanaingia siasa.
Fuatilia wahitimu wa Mzumbe walio kwenye siasa uone ni watu wana namna gani , Fanya utafiti mtajua nisemalo
 
DU! Fanya kama mnyika ambae amuthubutu kutaja na daraja alilopata kila level. uoga wa nini kama upo safi
 
Kumekuwepo na habari ambayo inavumishwa katika mitandao ya kijamii hasa hapa Jamiiforums kuhusu Elimu ya Katibu wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa, Itikati na Uenezi, Ndugu Nape Moses Nnauye. Taarifa hiyo kwa kiasi kikubwa inapotosha na kueleza yale ambayo si sahihi kuhusiana na CV ya Kiongozi huyo wa Chama cha Mapinduzi; Kutokana na Hilo, nimeona ni jambo la busara kuwasaidia wanajamvi kwa kuwapa CV iliyo sahihi ya Nape Moses Nnauye kama ifuatavyo;

  • Kati ya mwaka 1987-1989 alianza elimu yake ya msingi katika shule ya Msingi Mwanga-iliyopo Iramba Singida (ambapo alianza darasa la 1 mpaka 3)
  • Mwaka 1989-1993 aliendelea na kumalizia elimu ya msingi katika shule ya Bukumbi iliyopo misungwi Mwanza.(ambako alikuwa ni kati ya wanafunzi watatu “3” kati ya 120 waliochaguliwa sekondari.
  • Mwaka 1994-1995 alianza elimu ya Sekondari katika shule ya kutwa ya Ngudu Sekondari.(ambapo alisoma kidato cha kwanza mpaka cha pili)
  • Mwaka 1995-1997 aliendelea na elimu ya sekondari katika shule ya Bweni ya Sekondari Nsumba iliyopo Mwanza (ambapo aliendelea kidato cha pili mpaka cha nne)
  • Mwaka 1998-2000 alisoma elimu ya juu ya sekondari (advanced level), mchepuo wa EGM na kuhitimu Butimba TTC
  • Mwaka 2001-2002 alisoma Diploma ya sayansi ya jamii katika Chuo Cha sayansi ya Jamii-Kivukoni.
  • Mwaka 2002-2003 alisomea Diploma ya Diplomasia na uhusiano wa Kimataifa –Chuo cha Diplomasia Dar es salaam.
  • Mwaka 2005-2008 alisomea digrii ya Saikolojia, Lugha na Habari katika Chuo Kikuu cha Bangalore-India
  • Mwaka 2009-2010 alisoma digrii ya pili ya utawala (Masters in Public Administration-MPA) katika chuo cha Mzumbe
NB: Ndugu Nape Nnauye akiwa Kivukoni aliandika “thesis” iliyohusu ; VIKWAZO VINAVYOZUIA VIJANA KUSHIRIKI KATIKA SIASA. Na pia akiwa Mzumbe University aliandika kuhusu ; SABABU ZINAZOCHANGIA USHIRIKI WA WAPIGAKURA (ni ipi sababu ya kutojitokeza wapigakura siku ya Kura)
Hata mimi niliye feri mwaka huu najua tu jamaa na e aliferi form 4
 
Yani Nape alipiga Yai kwenye Civics? sasa CCM walimpaje itikadi na uenezi mtu asiyejua hata uraia?:shut-mouth:
 
Kumekuwepo na habari ambayo inavumishwa katika mitandao ya kijamii hasa hapa Jamiiforums kuhusu Elimu ya Katibu wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa, Itikati na Uenezi, Ndugu Nape Moses Nnauye. Taarifa hiyo kwa kiasi kikubwa inapotosha na kueleza yale ambayo si sahihi kuhusiana na CV ya Kiongozi huyo wa Chama cha Mapinduzi; Kutokana na Hilo, nimeona ni jambo la busara kuwasaidia wanajamvi kwa kuwapa CV iliyo sahihi ya Nape Moses Nnauye kama ifuatavyo;

  • Kati ya mwaka 1987-1989 alianza elimu yake ya msingi katika shule ya Msingi Mwanga-iliyopo Iramba Singida (ambapo alianza darasa la 1 mpaka 3)
  • Mwaka 1989-1993 aliendelea na kumalizia elimu ya msingi katika shule ya Bukumbi iliyopo misungwi Mwanza.(ambako alikuwa ni kati ya wanafunzi watatu “3” kati ya 120 waliochaguliwa sekondari.
  • Mwaka 1994-1995 alianza elimu ya Sekondari katika shule ya kutwa ya Ngudu Sekondari.(ambapo alisoma kidato cha kwanza mpaka cha pili)
  • Mwaka 1995-1997 aliendelea na elimu ya sekondari katika shule ya Bweni ya Sekondari Nsumba iliyopo Mwanza (ambapo aliendelea kidato cha pili mpaka cha nne)
  • Mwaka 1998-2000 alisoma elimu ya juu ya sekondari (advanced level), mchepuo wa EGM na kuhitimu Butimba TTC
  • Mwaka 2001-2002 alisoma Diploma ya sayansi ya jamii katika Chuo Cha sayansi ya Jamii-Kivukoni.
  • Mwaka 2002-2003 alisomea Diploma ya Diplomasia na uhusiano wa Kimataifa –Chuo cha Diplomasia Dar es salaam.
  • Mwaka 2005-2008 alisomea digrii ya Saikolojia, Lugha na Habari katika Chuo Kikuu cha Bangalore-India
  • Mwaka 2009-2010 alisoma digrii ya pili ya utawala (Masters in Public Administration-MPA) katika chuo cha Mzumbe
NB: Ndugu Nape Nnauye akiwa Kivukoni aliandika “thesis” iliyohusu ; VIKWAZO VINAVYOZUIA VIJANA KUSHIRIKI KATIKA SIASA. Na pia akiwa Mzumbe University aliandika kuhusu ; SABABU ZINAZOCHANGIA USHIRIKI WA WAPIGAKURA (ni ipi sababu ya kutojitokeza wapigakura siku ya Kura)

:israel:Mbona wewe Tandaleone PS wa Nape hauko makini? kwanini usiweke alifaulu kwa kiwango gani O-Level na A-Level? inaonekana wewe ni mpambe tu haujui kitu
 
Back
Top Bottom