Hii ndio maana halisi ya neno ndoa halali

Hii ndio maana halisi ya neno ndoa halali

Mwamuzi wa Tanzania

JF-Expert Member
Joined
Apr 7, 2020
Posts
15,486
Reaction score
45,256
Nimewasikia wengi wakilitumia neno ndoa halali. Wakisema ni mume wangu halili, wengine wakisema mke wangu halali. Wengine wakisema kuwa wamefunga ndoa halali n.k.

Je, mume anaporudi nyumbani asubuhi bila kusema alikuwa wapi hiyo tutaendelea kuiita ndoa halali? Mke na mume kila mmoja hajui kipato cha mwenzie hiyo tutaendelea kuiita ndoa halali? Wanandoa wanapigana mpaka wanatoana meno na ngeu, je, hiyo tutaendelea kuiita ndoa halali?. Wanandoa wanashindana kuchepuka kwa kukomoana, je hiyo tutaendelea kuiita ndoa halali?

Jibu ni HAPANA.
Je, vijana wawili waliovutana wakaamua kuishi pamoja kama mke na mume pasi na ugomvi, visasi huku wakiepuka michepuko hiyo tuiite ndoa haramu kwakuwa Mchungaji hajaifungisha? Wapenzi wawili waliovutana wakaishi na kuzaa watoto kwa furaha hiyo tuiite ndoa haramu kwakuwa sheikh hajaifungisha?

HAPANA.
Ukweli ni kwamba sheikh au Mchungaji hawezi kuifanya ndoa iwe halali au haramu. Bali wanandoa wenyewe ndio wanaweza kuifanya ndoa yao iwe halali au haramu.

SWALI: Je, ndoa yako ni halali au haramu?
 
Nimewasikia wengi wakilitumia neno ndoa halali . Wakisema ni mume wangu halili, wengine wakisema mke wangu halali. Wengine wakisema kuwa wamefunga ndoa halali n.k.
Je, mume anaporudi nyumbani asubuhi bila kusema alikuwa wapi hiyo tutaendelea kuiita ndoa halali?
Halali sana, uharamu uko kidogo kwa sababu ya michepuko michache
 
Nimewasikia wengi wakilitumia neno ndoa halali. Wakisema ni mume wangu halili, wengine wakisema mke wangu halali. Wengine wakisema kuwa wamefunga ndoa halali n.k.
Umeanzisha thd ukaweka maelezo yako,kisha ukaweka swali halafu wewe mwenyewe ukaja na conclusion zako tayari kwa mtazamo wako tu na sio kwa kutumia vifungu vya dini yeyote,dini ambazo ndio msingi wa kuhalalisha ndoa,

So,hapa hata ukijibiwa swali lako huwezi kukubaliana na majibu coz umesha weka unachokiamini wewe na kukipigilia msumari tayari!
 
Ndoa ya kwanza: Ilikuwa Halali sababu tulifungia kanisani na harusi kubwa sana....ila uharamu wake ni kwamba mwanamke alikengeuka baada ya kuwa na uwezo kupata ugali na connections za wakubwa mjini hivyo dharau ,kiburi vikazidi nikampiga chini ....tunaendelea kulea watoto

Mahusiano ya pili:Haramu sababu sijafungishwa ndoa rasmi lakini ni Halali sababu tumeshibana sana , nina piece of mind,no stress na tumeishi pamoja miaka 2 sasa ,adabu na heshima mbele
 
Hiko ni kivumishi tu cha kuwarusha roho mashosti! Ati wangu wa halali 😅😅😅 wakati jamaa tunamjua zipo mbovu kishenzi!
Hizi ndoa hatari.
Kuna jamaa jirani yetu kazichapa na mke wake mpaka kakimbia na boxer tu baada ya kumshushia wife wake kichapo na wife wake kutaka kumchoma kisu.
 
Back
Top Bottom