Hayo mapato yanatoka wapi kama sio kwa shughuli za watu?
Huko kwenu sijui ila huku Njombe tunalima chai,miti na Mazao yake,matunda mbalimbali hasa parachichi,Mazao ya nafaka kama viazi,na sasa Vanilla.
Ndani ya miaka 3 , Njombe itakuwa inaongoza Tzn kwa kilimo cha Vanilla maana kinalimwa kitaalamu kwenye greenhouses.
Kuhusu Migodi kwenye hiyo Halmashauri ni tatizo ambalo liko mikoa mingine hasa kanda ya ziwa , mapato mengi kutoka kampuni za Madini ambapo zina watu wachache Sana tofauti mikoa ya Nyanda za Juu Kusini ambako shughuli ni zile zinamnufaisha mtu moja kwa moja.