Hii ndio sensa ya kisasa na yenye tija kuliko zote tangu uhuru

Hii ndio sensa ya kisasa na yenye tija kuliko zote tangu uhuru

matunduizi

JF-Expert Member
Joined
Aug 20, 2018
Posts
7,968
Reaction score
19,368
Licha ya mapungufu machache, mfano karani na mwenyekiti wanazunguka bila hata reflector na kofia utadhani ni bibi na bwana wanatafuta shamba hapa Kijijini lakini hii Ni sensa super Sana.

1: Maswali yanayoulizwa yakifanikiwa Serikali itakuwa na taarifa nyeti Sana za raia wake kila Kona. Kila mwananchi, kitongoji na mkoa unakuwa wazi kwa wafanya maamuzi. Dodoso liko kisomi kiasi kwamba nikitoa taarifa sahihi, Serikali inamjua raia wake Kama Yesu anavyotujua wafuasi wake.

2: Karani amebanwa hawezi kufoji taarifa. Zilizopita niliwahi Kusoma humu jf mtu anasema yeye Baba yake alikuwa anawaletea makaratasi wanajaza wenyewe nyumbani kwao taarifa za watu bila kuwafikia.

3: Ukitaka kumuhakiki Karani Kama kafoji. Nchi naweza kuchukua sample ya watu wakati zoezi linaendelea na kutuma wapelelezi kuhakiki huku zoezi linaendelea. Kisha muhusika kuanikwa hadharani kwenye media,makarani wote wataogopa na kutii. Hivyo tutapata data swafi. Wanaweza kutengeneza hata kaigizo tu ili wawatishe wavivu.

4: Kwa watafutaji matokeo ya hii sensa Ni ya msingi Sana maana clarity ya data Ni kubwa na Ni za kutegemewa.

Ni hayo tu.

Ninaiongeza Serikali kwa hili. Binafsi nimebarikiwa Sana na huu mchakato.

Tupongeze mazuri, mabaya tukosoe kwa kutoa suluhisho (constructive criticism).
 
Mimi sio karani. Changia mada alafu hao makarani waache waendelee na wajibu wao kwa umma
Sisi huku tulipo asimia kubwa hatujafikwa na huyo karani, hili zoezi kwa upande wangu halina umuhimu
 
Back
Top Bottom