Hii ndio Siri ya mafanikio isiyosemwa sana Yanga

Hii ndio Siri ya mafanikio isiyosemwa sana Yanga

Sawa, naungana na wewe kwenye hizi pongezi. Ni kweli kabisa chini ya uongozi wake, Yanga imepata mafanikio makubwa ndani ya uwanja. Mfano kuchukua ubingwa wa Ligi kuu kwa mara 2 mfululizo, kucheza fainali kombe la Shirikisho Afrika kwa mara ya kwanza kabisa katika historia, nk.

Ila mwisho wa siku nafikiri haya mafanikio ya timu nayo yaendane pia na uwekezaji wa miundombinu kwenye klabu.

Yanga ina miaka zaidi ya 80 tangu ilipoanzishwa! Lakini mpaka leo hii, timu haina hata uwanja tu wa kufanyia mazoezi. Kuna ule mradi wa Kigamboni! Sijui mpaka leo umeishia wapi!!

Mashabiki na wanachama wa Yanga tunatakiwa tuwaambie ukweli viongozi wetu. Mafanikio ya uwanjani pekee hayatoshi. Tunataka pia kuona timu inawekeza kwenye miundombinu.

Yanga hii ya sasa inayoimbwa kila kona ya nchi, ilishakuwepo enzi za Abbas Gulamali, na pia Yusuph Manji! Ila kwa nyakati zote hizo, iliishia tu kupata umaarufu wa uwanjani! Huku timu ikiendelea kujivunia jengo pekee la pale mitaa ya Twiga na Jangani!! Nje ya hapo, Yanga haina kitu kingine cha kujivunia!

Ni wakati muafaka huu kwa rais wa Yanga kuurejesha ule mradi wa Kigamboni kwenye utekelezaji. Na siyo kufurahia tu mafanikio ya uwanjani.
Boli kwanza hayo mengine baadae.

Sent from my SM-A515F using JamiiForums mobile app
 
Mwamba anaupiga mwingi mpaka unamwagika,natamani hapo baadae Inshaallah aje kuwa Rais wa TFF (Ila baada ya kuipa Yanga[emoji172][emoji169][emoji123] Makombe 10+ ya ligi,na walau makombe ma 3+ ya CAF)
Uongozi Bora,Mabadiliko ya Kimuundo na Kiutendaji,Uwazi,Ushirikishwaji,Usasa (mbinu za kuongoza futbori la kileo),Kiu ya Mafanikio aliyonayo Eng. Hersi,Upendo kwa wachezaji na viongozi wenzie,Hamasa na Motisha kwa wachezaji ni baadhi kati ya mengi yanayomsaidia Eng. Hersi kupata mafanikio akiwa Young Africans.
Vilabu na viongozi wa timu zngne Bongo,Afrika Mashariki na Kati ipo tuition kubwa wanapaswa wajifunze kwa huyu Mwamba,tumpe maua yake kabla hajanyakuliwa na chama na serikali (kiddin[emoji3])
Kongole kwa Muwekezaji GSM,Kongole kwako Eng.,hata wasipokuimba leo watakuimba kesho kama mfalme wa transformation
Ndo maana kawa Mwenyekiti wa ACA.
 
View attachment 2809487
Ni Engineer HERSI SAID,
Raisi wa Klabu ya Yanga.

Mwalimu Nyerere aliwahi kusema kuwa Ili [Nchi] iendelee inahitaji vitu vinne, WATU, ARDHI, SIASA SAFI na UONGOZI BORA.
Katika vyote hivyo Cha muhimu zaidi ni Uongozi Bora.

Yanga chini Mheshimiwa Raisi HERSI wamelithibitisha hili.
HERSI Huwa hatamkwi Sana,.Lakini ndiye msingi mkubwa wa maendeleo ya Klabu ya Yanga.

Mpeni maua yakeeeee!

Engineer HERSI, you are My Icon, Endelea kuupiga mwingi.
He is trying let us give him a hand
 
Back
Top Bottom