Hii ndiyo historia ya mbio za marathon

Hii ndiyo historia ya mbio za marathon

Kanungila Karim

JF-Expert Member
Joined
Apr 29, 2016
Posts
20,743
Reaction score
25,564
Image may contain: 5 people, outdoor




WATU WENGI TUMEZOEA KUANGALIA MASHINDANO YA MBIO ZA MARATHON KATIKA MICHEZO YA OLIMPIKI AU KWENGINEKO LAKINI HATUJAPATA KUFAHAMU NINI CHANZO AU HISTORIA YA MBIO HIZI.

SASA UNGANA NAMI ILI KUJUA HISTORIA YAKE.

Hebu fatilia kisa hiki👇🏿

Mnamo miaka ya 490 BC, Dola ya Uajemi (Persian empire) ikiwa chini ya mfalme Darius ilikuwa inavamia mji wa Anthens ambao ndio makao makuu ya Ugiriki

Uvamizi huo ulikuja kama shambulio la kutaka kulipa kisasi kwa anthens kufuatia kitendo chao cha kuwasaidia watu wa mji wa Ionia waliokuwa wanataka kupindua utawala wa Darius(mfalme wa Persia) katika mapambano yaliyofanyika katika mji wa Iade (battle of lade) mnamo 493BC

Ingawa Persia waliweza kushinda vita hiyo dhidi ya watu wa Ionia , Mfalme Darius wa Persia aliapa kuwaadhibu miji ya Anthens na Aretria kwa kitendo chao cha kuisaidia Ionia.

Hivyo basi, mwaka 490BC, mfalme Darius alipeleka majeshi yakiongozwa na kamanda Datis, kwenda kuvamia, kuangamiza na kuteka miji ya anthens na eretria, na hatimaye kuitawala ugiriki yote.

Persian ilivamia miji ya Aegean, kupitia Cyclade na kufanikiwa kuiteka eretrea, na kuendelea kuukaribia mji wa Anthen.

Lakini walipofika mji wa Marathon, majeshi ya Anthens wakawa tayari wamefika eneo hilo. Na ndipo mapigano yalifanyika katika mji huo wa Marathon

Anthens walimtuma mtu mmoja aitwaye Philippides kwenda mji wa Spartan ili kuwaomba msaada wa kuongezewa nguvu dhidi ya Persian.

Philippides akakimbia mojakwa moja hadi mji wa Spartans, lakini siku ile akakuta watu wa mji huo (spartan) wapo katika sherehe za kuabudu, hivyo hawakuweza kuja kuwasaidia anthens kwenye vita.

Vita iliendelea na hatimaye anthens wakaweza kushinda vita dhidi ya Persian empire.
Philippides kama ilivyo kawaida yake, alivoona Anthens wameshinda vita akajawa na furaha kubwa, akakimbia bila kupumzika kutoka mji wa Marathon ambapo vita vilifanyika hadi mji wa anthens kwenda kutoa ripoti ya ushindi.

Alipofika ofisini aliingia kwa pupa pasipo kubisha hodi.
kulikuwa na viongozi kadhaa ofisini humo.

Phillipides akatamka maneno haya "WE HAVE WON" (tumeshinda) na akakata roho papo hapo.

......

Hivyo basi, haya mashindano ya mbio za marathon , yalianzishwa kama kumbukumbu ya shujaa Phillippides ambaye alikimbia kutoka mji wa marathon hadi anthens.

.....
Mbio za kwanza za marathon zilifanyika mnamo mwaka 1896 kwenye michezo ya kwanza ya Olimpiki mpya. -kama mtakuwa mnakumbuka vizuri nilitoa historia ya michezo ya olimpiki kwamba ilikuwa na awàmu mbili (Ancients Olimpic 776 BC na modern olimpik 1896.)

Mbio hizi za marathon, zina umbali wa kilometa 40.2km
Baada ya kufanyika marekebisho kutoka 40km.- Na huu umbali ni makadirio ya umbali kutoka mji wa marathon hadi Anthen.

Mwisho.
 
Image may contain: 5 people, outdoor




WATU WENGI TUMEZOEA KUANGALIA MASHINDANO YA MBIO ZA MARATHON KATIKA MICHEZO YA OLIMPIKI AU KWENGINEKO LAKINI HATUJAPATA KUFAHAMU NINI CHANZO AU HISTORIA YA MBIO HIZI.

SASA UNGANA NAMI ILI KUJUA HISTORIA YAKE.

Hebu fatilia kisa hiki👇🏿

Mnamo miaka ya 490 BC, Dola ya Uajemi (Persian empire) ikiwa chini ya mfalme Darius ilikuwa inavamia mji wa Anthens ambao ndio makao makuu ya Ugiriki

Uvamizi huo ulikuja kama shambulio la kutaka kulipa kisasi kwa anthens kufuatia kitendo chao cha kuwasaidia watu wa mji wa Ionia waliokuwa wanataka kupindua utawala wa Darius(mfalme wa Persia) katika mapambano yaliyofanyika katika mji wa Iade (battle of lade) mnamo 493BC

Ingawa Persia waliweza kushinda vita hiyo dhidi ya watu wa Ionia , Mfalme Darius wa Persia aliapa kuwaadhibu miji ya Anthens na Aretria kwa kitendo chao cha kuisaidia Ionia.

Hivyo basi, mwaka 490BC, mfalme Darius alipeleka majeshi yakiongozwa na kamanda Datis, kwenda kuvamia, kuangamiza na kuteka miji ya anthens na eretria, na hatimaye kuitawala ugiriki yote.

Persian ilivamia miji ya Aegean, kupitia Cyclade na kufanikiwa kuiteka eretrea, na kuendelea kuukaribia mji wa Anthen.

Lakini walipofika mji wa Marathon, majeshi ya Anthens wakawa tayari wamefika eneo hilo. Na ndipo mapigano yalifanyika katika mji huo wa Marathon

Anthens walimtuma mtu mmoja aitwaye Philippides kwenda mji wa Spartan ili kuwaomba msaada wa kuongezewa nguvu dhidi ya Persian.

Philippides akakimbia mojakwa moja hadi mji wa Spartans, lakini siku ile akakuta watu wa mji huo (spartan) wapo katika sherehe za kuabudu, hivyo hawakuweza kuja kuwasaidia anthens kwenye vita.

Vita iliendelea na hatimaye anthens wakaweza kushinda vita dhidi ya Persian empire.
Philippides kama ilivyo kawaida yake, alivoona Anthens wameshinda vita akajawa na furaha kubwa, akakimbia bila kupumzika kutoka mji wa Marathon ambapo vita vilifanyika hadi mji wa anthens kwenda kutoa ripoti ya ushindi.

Alipofika ofisini aliingia kwa pupa pasipo kubisha hodi.
kulikuwa na viongozi kadhaa ofisini humo.

Phillipides akatamka maneno haya "WE HAVE WON" (tumeshinda) na akakata roho papo hapo.

......

Hivyo basi, haya mashindano ya mbio za marathon , yalianzishwa kama kumbukumbu ya shujaa Phillippides ambaye alikimbia kutoka mji wa marathon hadi anthens.

.....
Mbio za kwanza za marathon zilifanyika mnamo mwaka 1896 kwenye michezo ya kwanza ya Olimpiki mpya. -kama mtakuwa mnakumbuka vizuri nilitoa historia ya michezo ya olimpiki kwamba ilikuwa na awàmu mbili (Ancients Olimpic 776 BC na modern olimpik 1896.)

Mbio hizi za marathon, zina umbali wa kilometa 40.2km
Baada ya kufanyika marekebisho kutoka 40km.- Na huu umbali ni makadirio ya umbali kutoka mji wa marathon hadi Anthen.

Mwisho.
Historia nzuri sana.Be blessed
 
Mm mwenyewe ni mpenzi wa huu mchezo, hasa huwa nashiriki Kilimanjaro half Marathon 21.1km.
Nilikuwa sijui historia yake, ubarikiwe mkuu
 
Back
Top Bottom