Uchaguzi 2020 Hii ndo sababu CCM wanakwepa kuzungumzia Dhahabu kwenye kampeni zao

Uchaguzi 2020 Hii ndo sababu CCM wanakwepa kuzungumzia Dhahabu kwenye kampeni zao

Missile of the Nation

JF-Expert Member
Joined
May 24, 2018
Posts
15,101
Reaction score
56,054
Baada ya kuingia madarakani serikali ya awamu ya tano mwaka 2017 ililitangazia Taifa na dunia azma yake ya kurekebisha sekta ya madini nchini hususan dhahabu.

Ikaunda tume Mbili za Osoro na Mruma, zikaja na matokeo ya kitafiti na maazimio yaliyotikisa nchi.
Miongoni mwa matokeo hayo ni amoja na:

(1) kwa miaka yote ambayo Acacia amefanya kazi nchini wameunder declare madini wanayo chukua (yaani walikuwa wakichukua madini mengi kuliko wanayotuambia)

(2)Ukiachilia mbali dhahabu kwenye makinikia, walikuwa wakituibia madini mengine kama vile nickel, cobalt na rare earth metals

(3) Kwamba makadirio ya wizi huo ni takriban dola za kinarekani bilion 190, ambayo ni kama shilingi za Kitanzania zaidi ya Trilion 420 na ushehe

Serikali mwaka 2017 ikatunga sheria na ikaweka vitu vifuatavyo:

1. Makinikia yatakuwa hayasafirishwi nje ya nchi, makampuni yatatakiwa kuchenjulia hapahapa

2 Mikataba yote ya madini lazima ipitishwe bungeni

3. Kesi zinazohusu madini yetu lazima ziamuliwe kwenye mahakama za Ndani

Licha ya uwepo wa sheria hiyo ambayo profesa Kabudi alijitapa nayo sana lakini serikali yenyewe ikaivunjilia mbali kwenye makubaliano yake na Barrick kwa mfano:

(1) Barick wakaruhusiwa kuwa wanachukua makinikia na kuyapeleka nje

(2)Mkataba wa Barick na serikali haukuelekwa bungeni

(3) Mkataba wa Barick na serikali unawaruhusu kufungua kesi za migogoro nje ya Tanzania

Katika muktadha huo inashangaza kidogo

1. Kwanza unafahamu hawa watu wamekuibia zaidi ya Trilion 420, kwa nini ukubali settlement ya dola milion 300 tu, ambayo ni sawa na shilingi bilion 690 (0.69 Trillion), ambayo ni pesa mbuzi kulinganisha na Trillion 420?

2. Kama hawa unajua kuwa ni wezi na ushahidi unao, kwa nini uendelee kufanya nao kazi in the first place kwa nini tusidai matrillion yetu kwanza halafu tutafute watu honest tufanye nao biashara?

3. Kwa nii uvunje sheria zako mwenyewe ulizojiwekea ukiamini hizo ndo zitakazolinda utajiri wako?

Kutokana na maswali haya magumu si ajabu kuona CCM wanakwepa sana kuzungumzia ishu ya madini maana inawavua nguo

Kwa uchambuzi zaidi wa hili suala, angalia mahojiano haya, wameyaelezea vizuri sana hayo:


 
Amini nakwambia, hakuna mtu tapeli kama Jiwe. Huyu mzee tukimwondoa hapo October ndo tutajua mengi. Ingawa Tundu Lissu kasema hatolipa kisasi na atamtunza vizuri Kama Raisi mstaafu ila amini nakwambia machafu yake yakija kuwekwa wazi watu wanaweza andamana kutaka aondolewe kinga ili ashtakiwe ! The guy is simply so evil
 
Jiwe ni muongo sana, anaendesha nchi kiujanjaujanja na fiksi nyingi mno

Sikutegemea kuona Jiwe anampitisha Deo Mwanyika mtu aliyefunguliwa mashitaka ya uhujumu uchumi, tena aliyekiri mahakamani kuhujumu uchumi katika madai kwamba anashirikiana na Wezi wa ACACIA kutuibia, kuwa mgombea ubunge kwa tiketi ya CCM huko Njombe Mjini

Bahati nzuri wananchi wameshamstukia kuwa ni msanii
 
Mijamaa isiyojulikana almanusra ituondolee kichwa chetu adimu Tundu Lissu kisa kukurupuka kwao na kujidai mizaleeeendo, kumbe haijui A wala B yoyote ya madini, ni mikurupuko mwanzo mwisho!

Baada ya kukuru kakara zao mwishowe ikaishia kuyalamba miguu mabeberu yaleyale waliyoyatukana kuwa eti ni majizi. Hakuna cha kuchenjua Makinikia nchini wala baba yake Matrilion yenye thamani inayolingana na Noah kwa kila mtanzania!.

Kamba tupu!
 
Hotuba kampeni akiwa Mara JPM alieleza mafanikio na kufafanua manufaa $300M , ni aibu nayo tunalipwa kwa mafunga ya nyanya,ukiachilia $100M, nyingine kwa miaka kadhaa tena walipaji wamechagua maeneo mfano kusupport tume ya madini $5, sehemu ya barabara zenye maslahi kwao.... ni kama walituzidi hoja.Hotuba report ,kauli za mkuu akihutubia taifa as uf taifa linaingia vitani!! ( Ilituharibia sana uwekezaji FDI) Busara ingetumika mapatano na wadau hiyo $300 ni pato la mwezi pekee Barrick multiplier effect, kinyume chake tumepoteza ajira na maisha maelfu , kutishia wawekezaji,tumepoteza mapato, kudorola uchumi wazabuni na viwanda .
 
Jiwe ni muongo sana, anaendesha nchi kiujanjaujanja na fiksi nyingi mno

Sikutegemea kuona Jiwe anampitisha Deo Mwanyika mtu aliyefunguliwa mashitaka ya uhujumu uchumi, tena aliyekiri mahakamani kuhujumu uchumi katika madai kwamba anashirikiana na Wezi wa ACACIA kutuibia, kuwa mgombea ubunge kwa tiketi ya CCM huko Njombe Mjini

Bahati nzuri wananchi wameshamstukia kuwa ni msanii
Hizi short cuts za Magufuli zitamgharimu sana.
 
Wazee wa MIGA kazini...
emoji3.png

Viva JPM
 
Hizi short cuts za Magufuli zitamgharimu sana.

Hazimgharimu yeye, yeye anajua katiba inamlinda kwa madudu yote anayofanya akiwa ofisini, anajua ana majeshi, NEC, Polisi usalama wa Taifa etc

Bali maamuzi yake yanatugharimu sisi wananchi na vizazi vyetu, sisi ndo tutalipa gharama za maamuzi yake yaliyojaa ego badala ya fikra sahihi
 
Ukistaajabu ya Sheria za madini,utamshangaa JK aliyekuwa Rais Sasa mke na mtoto ni wabunge wa CCM. Ukiwa unastaajabu ya JK utamshangaa Mwinyi mtoto wake anagombea Urais Zanzibar na watoto wengine wa kwake wanagombea ubunge Zanzibar. Ukiwa unastaajabu mzee mwinyi ,utakutana na mtoto Lowasa waziri mkuu Mstaafu, Fred Lowasa anagombea ubunge monduli. Ukiwa unastaajabu Mzee Lowasa, utakutana na mtoto wa waziri mkuu Mstaafu mzee Pinda anagombea ubunge kupitia ccm.watanzania bila kujali itikafi zetu mnajifunza nini?
 
Ukistaajabu ya Sheria za madini,utamshangaa JK aliyekuwa Rais Sasa mke na mtoto ni wabunge wa CCM. Ukiwa unastaajabu ya JK utamshangaa Mwinyi mtoto wake anagombea Urais Zanzibar na watoto wengine wa kwake wanagombea ubunge Zanzibar. Ukiwa unastaajabu mzee mwinyi ,utakutana na mtoto Lowasa waziri mkuu Mstaafu, Fred Lowasa anagombea ubunge monduli. Ukiwa unastaajabu Mzee Lowasa, utakutana na mtoto wa waziri mkuu Mstaafu mzee Pinda anagombea ubunge kupitia ccm.watanzania bila kujali itikafi zetu mnajifunza nini?
CCM ni genge la wanyonyaji wa kisiasa
 
Back
Top Bottom