Hii ni kawaida ama nina shida gani mimi?

Hii ni kawaida ama nina shida gani mimi?

KIJANA HONGERA SANA KWA KIPAJI CHAKO ULICHONACHO NAONA KAMA UNANIFAA SANA KWENYE SHUGHULI ZANGU ZA UJENZI WA TAIFA.Tafadhali naomba tuwasiliane kwenye barua pepe ifuatayo: Ombeni.charles@gmail.com

Mkuu kazi za zako kujenga taifa? Kazi gani mkuu? Niweke wazi kwanza kabla hatujaenda next step.
Kama vp ni PM.
 
nlikuwa na rafiki yangu alikuwa na hali km yako. yeye aliambiwa ana jini mahaba,yule jini ndo anakuwa hapendi kumuona anakasirika ndo mana analipiza kisasi lkn yule dada akaombewa duwa saivi ameanza kupona
 
Mmm pole sana nenda kaombewe upone bwana kukoseana ni part ya maisha hali yako itawagharimu wengu haswa sisi tusiokujua.
 
Watangazie chuki mafisadi woote, ili tuweze kuthibitisha.
 
Hebu wakasirikie wale wawekezaji katika madini waliowadanganya au kutoa rushwa taifa likaingia katika mikataba ya kipumbavu ili waturudishie haki yetu.
 
Nilisoma thread ya memba flani ambaye alipata ndoto kwamba kuna ndege itapata ajali na nikasoma nyingine kuhusu ndugu aliyekua anakabwa sana usiku. Thread hizo ndizo hasa zilizonisukuma na mimi nitoe hili ambalo nimekua linanisumbua maishani mwangu, japo sijawahi mwambia mtu.
Nikikosana ama kukorofishana na mtu halafu nikimchukia ama kumkasirikia huyo mtu basi huwa huyo mtu anapatwa na balaa flani au anaandamwa na mikosi.
Mtu wa kwanza kuligundua hili jambo hili alikua mama yangu mzazi, nikiwa mdogo sana nilisikia siku moja mama akimuhadithia shogake (jirani yetu) lakini sikutilia maanani ila nilivyokua mkubwa ndiyo nilielewa.
Baadhi ya matukio ninayoyakumbuka ni
1. Nikiwa shule ya msingi, kuna mwanamama alikua anauza mafenesi akanidhulumu hela yangu, nikakasirika sana na nikalia sana. Kuanzia hapo huyo mama alikua kila fenesi analoleta limeharibika hadi akaacha hiyo biashara.
2. Nikiwa advance, kuna jamaa tulipigana na nikamwambia utaona, baada ya wiki jamaa akakamatwa mtaani akawa suspended na hakurudi tena shule.
3. Nikiwa chuo kuna dada mmoja alikua girlfriend wangu na tukaachana, alinitukana sana na nikamchunia. Yule dada aliandamwa na sup hadi akaja kuniomba msamaha
4. Nikiwa chuo kuna jamaa mmoja tulikosana naye, baada ya wiki kama moja hivi alidisco.
5.kuna mwalimu alinipiga sana nikiwa shule ya msingi, nilimchukia na nikajisemea rohoni natamani afe, baada ya miezi kama mitatu yule mwalimu aliugua akafa.
6. Ni juzo tu kuna jamaa mmoja alinidhulumu hela flani, nimeshtuka kukutana na huyu bwana wiki iliyopita akiwa chizi.
Matukio kama haya ni mengi sana hadi inafika kipindi mtu akinikasirisha namuomba Mungu asije akapatwa na makubwa.
Nisaidieni wakuu, hii hali kweli ni ya kawaida, binafsi sidhani kama ni coincidence kwa haya yanayotokea!!.

Dah nakutamania kama nini jembe hehehe. Itabidi uwe my best friend ntakuwa na'divert vibifu vyangu na wajingawajinga kwako ukiwalipukia tu kitukitu(mi ntakuwa roho kwatuu)
Ehehehehehe
 
pole, maombi husaidia kweli.

Kuna mdada alimwambia mtu 'you will pay for this somedays'
baada ya siku 3, mtoto ya yule kaka akaanguka shule ghafla.

Yule kaka akarudi kwa yule dada kulalamika, yule dada alijisikia vibaya mno.
Na wala hakufanya lolote, aliropoka kwa hasira tu.
 
This thread proves that most Tanzanians are superstitious. Guys guys guys how on earth can you believe that this is true? Eti nikasema natamani afe then akafa. Oh Please give me a break!!!
 
Some stories are best kept secret even if possible. Mfano nkipishana na mtu anatembea bila KICHWA barabarani siwezi nkaja mwaga hapa ukweli huo maana hauaminiki. I'm sorry to say this but story yako haiaminiki hata iweje.
 
Some stories are best kept secret even if possible. Mfano nkipishana na mtu anatembea bila KICHWA barabarani siwezi nkaja mwaga hapa ukweli huo maana hauaminiki. I'm sorry to say this but story yako haiaminiki hata iweje.

Kama humuamini mtukane sasa uone kama hajakunuizia ukuni ukahamia kichwani kama pembe ya kifaru
 
Naomb mchukie ******, ahanguke leo leo,ntashukuru kwa msaada wako mkuu.
 
Naomb mchukie m.k.w.r.e, ahanguke leo leo,ntashukuru kwa msaada wako mkuu.
 
Omg! Mi naogopa hata kuchangia nisije nikakukasirisha nikapata mikosi.
 
Some stories are best kept secret even if possible. Mfano nkipishana na mtu anatembea bila KICHWA barabarani siwezi nkaja mwaga hapa ukweli huo maana hauaminiki. I'm sorry to say this but story yako haiaminiki hata iweje.

tembea uone.
 
nenda ukafanyiwe maombi yatakusaidia.
 
Sio aombe Mungu apewe siri ya matumizi ya nguvu hizo , BALI AOMBEWE ATOKWE NA HAYO MAPEPO YANAYOMTESA< HUYO MWISHO WAKE NI MCHAWI WA KUTISHA

MUNGU AMPONYE NA KUMUWEKA HURU
 
Usinielewe vibaya mkuu, nataka kabla sijakushauri nikashauriane na maza-ako, maana napa ipresheni kuwa anajua A-Z ya shida yako. Mkuu ukinichukia n'takomaje mimi!

Hahahahhahahhahaaaaaaaaaaa................lol. Nimechekaje?
 
Sio aombe Mungu apewe siri ya matumizi ya nguvu hizo , BALI AOMBEWE ATOKWE NA HAYO MAPEPO YANAYOMTESA< HUYO MWISHO WAKE NI MCHAWI WA KUTISHA

MUNGU AMPONYE NA KUMUWEKA HURU

Aaah asiombewe kwanza awachukie CCM wote wageuke misukule,hapo ndio ntaamini na kusuuzika mtima.
 
Back
Top Bottom