Itakua ninyi ni wageni wa Sci-fi moviesJana kwenye Dstv chaneli ya Maisha Magic Bongo nilishuhudia movie inayoitwa 'hornet' nafikiri inarushwa kwa ufadhili wa Marekani, actors ni Wamarekani wenyewe ila imewekewa maneno ya Kiswahili.
Kwa wale mliowahi kuona au kufuatilia hii movie ni jambo gani hasa linaashiriwa kutokea huko mbeleni? hasa likihusisha viumbe au vyombo toka sayari za mbali na kipindi cha dhiki kuu na mateso ya namba 666 (great tribulations) yanayoongelewa kwenye Biblia hasa katika kitabu cha Daniel na Ufunuo?
Karibuni.
Hii movie inaonekana imetolewa na serikali ya marekani na katika maelezo yake ya awali inaonekana ni confidential (yaani maudhui yaliyomo kwenye hiyo movie yalikuwa yamefanywa kama jambo la siri). Humo ndani kuna matukio ya watu kuvamiwa na vyombo na viumbe kutoka sayari za juu na kupotea katika mazingira ya kutatanisha. Nikiihusianisha hii movie na maono yangu ya huko nyuma naona kuelekea mwisho wa dunia kuna viumbe kutoka sayari za juu watavamia duniani na ndo itakuwa mwanzo wa kuanza kwa machafuko na ghasia kila mahali ambazo zitakuwa nje ya uthibiti wa mifumo ya kawaida ya binadamu na inawezekana kabisa watashirikiana na waabudu shetani wa hapa duniani (illuminants and the likes). Hii pia imenifanya kujua kwamba kuna mipango timilifu ambayo inaratibiwa na ibilisi na mawakala zake kuelekea mwisho wa dunia.Itakua ninyi ni wageni wa Sci-fi movies
View attachment 1938977