Hii ni mimba?

Step by step

JF-Expert Member
Joined
Apr 28, 2014
Posts
1,164
Reaction score
1,293
Jambo wadau,

mzunguko wa wife ni siku 26 mara nyingi japo kuna time zinakua 28. Mimi nimempa haki yake siku ya 12,13,14,15 yani nilikua kila asubuhi nadukua kamoja tu mpaka kesho kamoja tena kwa hizo siku 4.

Sasa leo ndo siku yake ya 26 tumepima imesoma negativ ila anasema kiuno kinamuuma je yawezekana ikawa ni mimba?

Kawaida akikaribiaga hedhi anatoka kipele usoni,matiti yanauma na kiuno lakini kwa sasa usoni yuko poa hana kipele wala matiti hayaumi ila kiuno tu ndo kinamsumbua anasema kina kaza.

Wataalam hebu nambieni kunani hapa.
 
umepga fertilization day, na pia danger days lazma iwe yenyewe io
 
shukrani wote jamani lazima nilete mrejesho hapa wa itakavyokua
 
Aende hospitali akafanye kipimo cha mimba,usije jipa matumaini sana mwishowe hamna kitu,utajiumiza!! mi pia nlikua nna mzunguko wa 28,ila zilikawia had siku ya 34!! nkawa najua mambo safi!! kukaa kidogo wageni hao wakaanza churuzika
 
pouwa ila updates ni kuwa mzunguko wake ni siku 26, leo siku ya 30 mp haijaja, dalili za hedhi zimepotea yuko normal kabisa japo joto la mwili linapanda na kuna time anapata maumivu ya mgongo kidogo. Tumepima leo siku ya 30 kimesoma negativ na yy hajawai vuka siku 28 so tumeshauriwa kuendelea kusubiri ila dalili zote za ujauzito zinaonekana
 
leo ni siku ya 31 hakuna hedhi wala dalili za hedhi mamaa yuko fiti kabisa so kashazidisha siku tano tangu alipotegemea kuona siku zake
 
CRAPSSSSSSSSSSSSSSSSSSS......jamani yaani unauliza wkt maelezo yako ndo jibu?????????????...Ngoja nipanguse mbu nakuja tena kupost
 
leo ni siku ya 31 hakuna hedhi wala dalili za hedhi mamaa yuko fiti kabisa so kashazidisha siku tano tangu alipotegemea kuona siku zake

Kama huyo mkeo hua tangia awe mkubwa hajawahi kupitisha mwezi bila kuona siku zake ni wazi asilimia mia ana ujauzito lkn kama hua miez mingine haion hio inaweza isiwe mimba,na mimba haiwezi kuonekana mapema kihivo wanasema hadi wiki ipite ndio kipimo kitaonyesha
 
Sasa mkuu unataka ushauri wa hapa uendane tofauti na vipimo ?

Cha maana ni kuendelea kupima (hakuna ushauri utakaokuwa efficient kuliko kipimo) Cha maana ili kuwa na uhakika pima wiki nzima baada ya kumiss period na pima wakati wa asubuhi
 
KanunuE kipimo cha mimba phamac.kinauzwa elf.tu

Jinsi ya kukitumia.
Huyo Mkeo akojoe katika kifaa kidogo halafu akidondoshe humo ndani kwa dakika tatu. Ikiwa kuna Mistari miwili nyekundu ina maana tiyari ana mimba.

Ikiwa ni Mstari mmoja mwekundu ina maana bado hakuna ujauzito.
 
Chukua shilingi 1000, nenda pharmacy yoyote ile/ duka la dawa. Nunua UPT, mpime ili mjue
 
kwa masikitiko makubwa kabisa mke wangu ameanza mp leo yani nimeloa hata siamini nachokiona. Mzunguko wake kila mwez ni siku 26 maajabu haya eti leo imekuja siku ya 35 kwa mara ya kwanza ktk maisha yake. Hebu nishaurini wadau nahitaji sana mtoto kuna tatzo gani hapa na kwa huu mzunguko mpya je siku za hatari zitakua lini
 
Hataareeeee


Anza kuhesabu kuanzia siku aliyoona period Mpaka zikifika siku Ishirini ndio siku ya kushika Mimba.

NB
Kwa siku zote hizo ishirini Mle vizuri na kupumzika vya kutosha .
Mwanaume hutakiwi kufanya hilo tendo kila siku kwa hiyo inatakiwa ukae siku hizi ishirini ili uwe na Nguvu.

Msiwe na papara
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…