Inakubidi kujimudu kutoogopa.. Fat Joe hakuogopa alivyosikia Big Punisher kafa.. uzito unasemekana huambatana na BP ila yeye haamini katika hilo.. nakushauri Mtafute Mmasai au Mkuria Original akusaidie kuandaa menyu ya Asili ya Mashujaa[Nyama ya Mbuzi inachanganywa na mizizi asilia ya kitabibu,au Ghichuri ya Mbuzi aliefugwa Porini anakula mimea tu!] haina uhusiano wowote na mizimu wala ushirikina,hofu inayosabisha una panic itaisha.
Hofu inayokusibu ndio inafanya Moyo wako unakimbia muda wote wakati hakuna shari yaani ni kwamba unakuwa kichwani kwako umejenga taswira fulani kabla ya kutokea jambo halisi.Mfano rafiki kipenzi anaumwa, unaenda kumcheki hospitali ukitumaini ni mzima lakini unapofika katika korido ya wodi unakutana nesi anayemwuuguza anasukuma kitanda cha matairi kilichobeba mwili wa mtu,moyo utakimbia sana japo haujafahamu kama ni rafiki yako au ni mgonjwa mwingine.
Hofu inaweza kuwa inakusibu sababu ya:
1.Madeni
2.Vifo ulivyoshuhudia au unavyohisi vitatokea
3.Mtihani au Kesi
4.Kukosa Tumaini Kukatishwa tamaa na wanafamilia
5.Kutengwa
6.Kuwindwa na Nguvu za Giza
7.Chuki za wafitini na Kutishwa n.k
Wadau waje wakupe mbinu za kuondoa Hofu;
1.Kushiriki Michezo
2.Kutokukaa na wanafiki
3.Kupata Hewa safi na Chakula kisicho na Caffeine nk
4.Kusali [Sala yenye lengo la kujipa Moyo na Mori
5.Kusikiliza nyimbo za kishujaa (Kamwe usisikilize nyimbo za Maombolezo au Mapambio ya ufufuko mpaka utapokuwa umepona)
.............Ngoja wadau waje