Hili ni tatizo kaka,angekuwa kajifungua salama tungesema jitahidi kulea...ila kikawaida si vizuri mtu aliyejifungulia kisu kuwahi kubeba mimba ,unatakiwa ukae miaka miwili ili layer za ngozi ziwe zimepona.Japo kuna wifi yangu aliwahi kuzaa baada ya mwaka kwa njia ya C japo alikuwa hafanyi kazi yeyote mpaka siku ya kujifungua.Nenda hospitali pia ili akapimwe ni jinsi gani hilo kovu linaendelea huko ndani lisije likaleta tatizo,pia ni vizuri kutumia njia za kuzuia mimba mama akiwa katika hali ya kunyonyesha.