Hii picha nimeipenda sbb inanikumbusha mbali

Hii picha nimeipenda sbb inanikumbusha mbali

cheusimangala

JF-Expert Member
Joined
Feb 27, 2010
Posts
2,585
Reaction score
498
enzihizo.jpg



Weee sema chochote upendacho kuhusu hii picha lkn mie imenikumbusha mbali sana back to 80's wakati niko mtoto, hasa wakati wa xmas mama yetu alikuwa ananunua kitambaa cha aina moja wote kuanzia dada zangu hadi mimi tunashonewa kitambaa hicho hicho hadi mshono mmoja.

Viatu mnanunuliwa vikubwa kidogo eti ili ukuwe navyo mbele unajazia na karatasi ili vitoshe.
mkishakula pilau na double cola mnapewa hela muende mjini mkatembee,basi nilikuwa najiona nimependezaa,usoni mmepakwa mafuta ya rays mnang'aa kama kioo.

Mkienda kutembea mjini mtu unatembea kama kiwete maana viatu vinaumiza..aah nafurahi kuwa mtu mzima maana leo hii nisivyopenda nguo za kushona.leo nikiamua kuvaa leging na skin jeans hakuna wakunichagulia.

Utu uzima raha jamani.
 
mshukuru pia mama yako kwa kukupeleka shule!!

Picha safi sana hii love ya mama bana....anamtanguliza mtoto mbele,
wamjini wanawaacha watoto nyuma!!
 
Nimekubali mama kumbe kwa umri tunakaribiana, nilifikiri we wa juzi tu!
 
Ila raba mtoni zimekukaa mama! Na huo mguu, acha tu!
 
Those days were days bana, sikukuu ilikuwa kweli sikukuu sare nyumba nzima, jioni mnaenda kutembea somewhere. kwa jirani km wana nguo mpya nyie hamna daaaaaaaaaaaaah sikukuu inakuwa mbaya mnooooo
 
Such a lovely pic !!! with green n enrich soil !!! It's remind me a lots on those days !! thanx cheusi !
 
Those days were days bana, sikukuu ilikuwa kweli sikukuu sare nyumba nzima, jioni mnaenda kutembea somewhere. kwa jirani km wana nguo mpya nyie hamna daaaaaaaaaaaaah sikukuu inakuwa mbaya mnooooo

hahaa we acha tu xmas moja fundi alifanikiwa kushona nguo za ndugu zangu wote lkn yangu akachelewa hivyo nikaambiwa nitaivaa tar 26 instead kwa hiyo nivae ya xmas iliyopita!nililia siku hiyo yaani!hahaa kazi kwelikweli!
 
wa mjini malezi ya bata .... anajua kutotoa tu wala hajui kulea kijijini malezi ya kuku... wa huku mjini ukiwauliza anakwambia bwana eee nilikuwa kwenye starehe zangu ndio ukapatikakana wewe wala sikupanga
 
eheeeee umenikumbusha mabli mno... enzi hizo kipindi cha x mas na mwaka mpya nikiona maza karudi na box tu basi na jua ndani kuna MOKA na sis nae ana SKUNA zake... pia najua kuna mashati ya ndege na suruali za mchelemchele na zina mikanda ya kama mpira ina pad ya treni.... hahhhhhhh tumetoka mbaliiiii..... siku hiyo unatembea kama unanyata... hukai ovyo na wala hushiki chochote ovyo..... ila mkirudi tu nguo unaishia kuziona kwenye kabati mpaka upatikane mtoko... baada ya sikukuu kama mbili tatu ndio zinakuja mpya zingine..
 
People...kuna kitu hapa....Jana mwanaJF fulani alitoa picha fulani ya members wawili wakiwa wadogo, na walikuwa eneo hilihili...Je hamuongezi 1 na 1 mkapata 8?

kijijini1.jpg



linganisha na hii hapa chini!

enzihizo.jpg
 
Cheusimangala umetoa wapi picha yangu lakini???🙂😀
Mod naomba uitoe kwenye web yako nisijepata matatizo ya kifamilia
 
Cheusimangala umetoa wapi picha yangu lakini???🙂😀
Mod naomba uitoe kwenye web yako nisijepata matatizo ya kifamilia
jamani fl1 si uliniruhusu mwenyewe niichukue kwenye ile albam yako!lol
 
People...kuna kitu hapa....Jana mwanaJF fulani alitoa picha fulani ya members wawili wakiwa wadogo, na walikuwa eneo hilihili...Je hamuongezi 1 na 1 mkapata 8?

nasikia eti hao mabrazamen hapo juu ni chrispin na kaizer enzi zao zakutesa!
 
eheeeee umenikumbusha mabli mno... enzi hizo kipindi cha x mas na mwaka mpya nikiona maza karudi na box tu basi na jua ndani kuna MOKA na sis nae ana SKUNA zake... pia najua kuna mashati ya ndege na suruali za mchelemchele na zina mikanda ya kama mpira ina pad ya treni.... hahhhhhhh tumetoka mbaliiiii..... siku hiyo unatembea kama unanyata... hukai ovyo na wala hushiki chochote ovyo..... ila mkirudi tu nguo unaishia kuziona kwenye kabati mpaka upatikane mtoko... baada ya sikukuu kama mbili tatu ndio zinakuja mpya zingine..

umenichekesha!unakumbuka mashati ya ujiuji?kazi kweli.
 
Back
Top Bottom