DOKEZO Hii sio haki, Haiwezekeni eneo langu ligundulike kuwa na madini halafu serikali inipangie bei ya kuuza eneo langu na inakuwa ni Amri sio ombi

DOKEZO Hii sio haki, Haiwezekeni eneo langu ligundulike kuwa na madini halafu serikali inipangie bei ya kuuza eneo langu na inakuwa ni Amri sio ombi

Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'

Nikifa MkeWangu Asiolewe

JF-Expert Member
Joined
Feb 26, 2024
Posts
6,944
Reaction score
14,351
Nchi hii imebarikiwa sana na huu ndo ukweli halisi, Si mbunga za wanyama, ardhi zenye rutuba, mito, mistu maziwa, Bahari na madini vyote hivi vinapatikana Tanzania achilia mbali ambavyo sijataja kama ges na makaa ya mawe na vingine vingi.

Wakuu kuna vitu serikali inawafanyia wananchi wake unabaki na maswali mengi sana yasiyo kuwa na majibu.
Inawezekana vipi shamba langu limegundulika kuwa lina madini kama dhahabu, shaba, chuma na ulanga bei ipangwe na serikali kuwa hawa wenye mashamba tutawapa kila heka m5(mfano) bila kuwahusisha wananchi wenyewe?

Waziri wa Ardhi na waziri wa nishati na madini hii ni sawa kweli? Ukweli hii sheria haifai kama ipo iondolewe mnaibia wananchi.Kuna mahari fulani wananchi walinunuliwa mashamba yao kwa m3 kila heka na kupanua eneo la mwekezaji mkubwa wa madini jina X.Imagine eneo lako lina dhahabu halafu ulipwe m3!!? Hivi viongozi mnao fanya haya aibu huwa mnaziacha wapi?

Heka ya miguu 70 urefu 70 mapana yenye dhahabu mnakubaliana kabisa watu wapewe m3? hata kama sijui sheria lakini hili sio sawa kabisa.Tundu Lissu na uhakika hawezi kukubali hili lifanyike.

Napendekeza kila wenye mashamba/maeneo yao iwapo litagundurika lina madina/ges pamoja na kwamba watapewa hiyo hela bado wanapaswa wawe na share mle wapate % hata kama nikidogo wapewe maisha yao yote hadi pale mgodi utakapoacha uzarishaji wake.

Hata kama mnajua kwa sasa hatuna uwezo wa kuchimba madini ni sawa kizazi kinachokuja kitaweza kuchimba na hili sio la kupinga kushindwa kwetu kusitufanye vitukuu vyetu waje waishi maisha ya ufukara zaidi.

Naomba sana tendeni haki hii ya kluwatumia olice kufukuza watu na kupisha mwekezaji ikome bali mazungumzo yafanyike na watu waridhie na sio ubabe.
 
Madini sio mali yetu sisi ni wasimamizi tu madini yote duniani bila kujali yapo nchi gani ni ya familia ya Debeers na kina Dupont family wao ndio uamua soko la madini.
 
Inasikitisha sana

20250131_160335.jpg
 
Nchi hii imebarikiwa sana na huu ndo ukweli halisi,Si mbunga za wanyama,ardhi zenye rutuba,mito,mistu maziwa,Bahari na madini vyote hivi vinapatikana Tanzania achilia mbali ambavyo sijataja kama ges na makaa ya mawe na vingine vingi.

Wakuu kuna vitu serkali inawafanyia wananchi wake unabaki na maswali mengi sana yasiyo kuwa na majibu.
Inawezekana vipi shamba langu limegundurika kuwa lina madini kama dhahabu,shaba,chuma na ulanga bei ipangwe na serikali kuwa hawa wenye mashamba tutawapa kila heka m5(mfano) bila kuwa husisha wananchi wenyewe?

Waziri wa Ardhi na waziri wa nishati na madini hii ni sawa kweli? Ukweli hii sheria haifai kama ipo iondolewe mnaibia wananchi.Kuna mahari fulani wananchi walinunuliwa mashamba yao kwa m3 kila heka na kupanua eneo la mwekezaji mkubwa wa madini jina X.Imagine eneo lako lina dhahabu halafu ulipwe m3!!? Hivi viongozi mnao fanya haya aibu huwa mnaziacha wapi?

Heka ya miguu 70 urefu 70 mapana yenye dhahabu mnakubaliana kabisa watu wapewe m3? hata kama sijui sheria lakini hili sio sawa kabisa.Tundu lisu na uhakika hawezi kukubali hili lifanyike.

Napendekeza kila wenye mashamba/maeneo yao iwapo litagundurika lina madina/ges pamoja na kwamba watapewa hiyo hela bado wanapaswa wawe na share mle wapate % hata kama nikidogo wapewe maisha yao yote hadi pale mgodi utakapoacha uzarishaji wake.

Hata kama mnajua kwa sasa hatuna uwezo wa kuchimba madini ni sawa kizazi kinachokuja kitaweza kuchimba na hili sio la kupinga kushindwa kwetu kusitufanye vitukuu vyetu waje waishi maisha ya ufukara zaidi.

Naomba sana tendeni haki hii ya kluwatumia olice kufukuza watu na kupisha mwekezaji ikome bali mazungumzo yafanyike na watu waridhie na sio ubabe.
Ni Mahenge?
 
Kuna jama yeye alikuwa na shamba kubwa tu ila ni mchanga tupu akawa anauza kwa watu wa ujenzi watu wakamchoma serikalini
Lile shamba limevhukuliwa na serikal now hana kitu mfumo mbovu
 
Back
Top Bottom