Hii siyo sawa kabisa, inakuwaje wezi wa kuku wanatupwa jela, wakati wezi wa mali ya umma wanaachwa huru?

Hii siyo sawa kabisa, inakuwaje wezi wa kuku wanatupwa jela, wakati wezi wa mali ya umma wanaachwa huru?

Mystery

JF-Expert Member
Joined
Mar 8, 2012
Posts
15,843
Reaction score
31,057
Tulimsikia Rais wetu, Samia Suluhu Hassan, katika hotuba yake ya majuzi, huko Katika Chuo cha Polisi
Moshi, akieleza kuwa baadhi ya maofisa wa Polisi, wanaiba mafuta ya petrol/diesel, wanayoletewa kwa matumizi ya Umma na kuyaweka kwenye daladala zao binafsi!

Rais Samia pia akaendelea kueleza kuwa taarifa anazo, hadi namba za hayo magari binafsi "yanayokunywa" hayo mafuta yetu yaliyotengwa kwa matumizi ya Umma.

Swali kubwa ninalomuuliza Rais wetu ni hili, ikiwa yeye ametuthibitishia kuwa hadi namba za hayo magari binafsi za hao makamanda anazo, je ni kwanini anashikwa na kigugumizi na hachukui hatua kwa makosa hayo ya dhahiri ya jinai?

Hivi Rais wetu anajisikiaje anapoona maelfu ya wahalifu wengine wa makosa madogo madogo, kama vile wezi wa kuku, wakitupwa magerezani kila uchao, kwenye Mahakama zetu hapa nchini, wakati hao makamanda wa Polisi akiwaachia watembee huru uraiani?

Huu ubaguzi wa wazi kabisa wa kuwafanya baadhi ya wananchi kuwa na "impunity" na kutoweza kushitakiwa na wengine wawe wanaozea jela kwa makosa madogo madogo, siyo "fair" kabisa
 
Umeongea vizuri ila, Ukijibiwa hilo swali na hili genge la majizi aka cartel of criminals) lililoko madarakani naomba uniTAG please
Lazima tuhoji, kwa kuwa tunajua kuwa hakuna mtu aliye juu ya sheria, kwa hiyo ndiyo tunauliza Hawa makamanda wa Polisi, ni kwanini hawachukuliwi hatua za kisheria??
 
Kwa Tz nikawaida mkubwa akiiba inasemwa amechukua tuu anaombwa asichukue tena lkn mdogo akiiba hapo ndoutajua tunaserikali... tunao takukuru wanaolipwa hasa lakini hakuna lamaana tunaloliona kwao zaidi ya kujisifu bar kwamba wao wanauwezo wakukamata hata polisi!!!
Tumesharudia "bongozembe" yetu ileeee yakipindi kileee
 
Hakurupuki katika kuchukua hatua siyo kama bwana yule.
 
Hivi ile report ya CAG inavyotajaga ile mipunga kuibiwa hatima yake ni nini?

Sometimes naonaga ni bora CAG aendelee na mishe nyingine maana ile report yake ni kama ratiba tu ila hamna kinachofuata baada ya hapo.
Ndiyo sababu wananchi tunaendelea kujaziwa mizigo ya tozo, kwa ajili ya kuwanufaisha baadhi tu ya maofisa wa Serikalini waendelee kutuibia!🥺
 
Dawa ya kudumu ya nchi hii ni kupata Katiba mpya ya wananchi..................

Bila hivyo wananchi wa kawaida, tutaendelea kunyanyaswa na kuumizwa na haya matozo, hadi mwisho wa Dunia!
 
Kwa Tz nikawaida mkubwa akiiba inasemwa amechukua tuu anaombwa asichukue tena lkn mdogo akiiba hapo ndoutajua tunaserikali... tunao takukuru wanaolipwa hasa lakini hakuna lamaana tunaloliona kwao zaidi ya kujisifu bar kwamba wao wanauwezo wakukamata hata polisi!!!
Tumesharudia "bongozembe" yetu ileeee yakipindi kileee
😅😅😅
 
Hivi ile report ya CAG inavyotajaga ile mipunga kuibiwa hatima yake ni nini?

Sometimes naonaga ni bora CAG aendelee na mishe nyingine maana ile report yake ni kama ratiba tu ila hamna kinachofuata baada ya hapo.
Zile ni repoti zakutupumbaza tu
 
Ni kwasabb mwenye nacho huongezewa. Mwizi wa mabilioni na mwizi wa kuku nani anacho zaidi?
 
Dawa ya kudumu ya nchi hii ni kupata Katiba mpya ya wananchi..................

Bila hivyo wananchi wa kawaida, tutaendelea kunyanyaswa na kuumizwa na haya matozo, hadi mwisho wa Dunia!
Mkuu suluhu sio katiba mpya....nadhani dawa ya kudumu ni uwajibikaji wa viongozi wetu,kila MTU kwa nafasi yake. Unaweza ukawa na katiba mpya lakini watu ni wale wale akina Mwigulu.
 
Tulimsikia Rais wetu, Samia Suluhu Hassan, katika hotuba yake ya majuzi, huko Katika Chuo cha Polisi
Moshi, akieleza kuwa baadhi ya maofisa wa Polisi, wanaiba mafuta ya petrol/diesel, wanayoletewa kwa matumizi ya Umma na kuyaweka kwenye daladala zao binafsi!

Rais Samia pia akaendelea kueleza kuwa taarifa anazo, hadi namba za hayo magari binafsi "yanayokunywa" hayo mafuta yetu yaliyotengwa kwa matumizi ya Umma.

Swali kubwa ninalomuuliza Rais wetu ni hili, ikiwa yeye ametuthibitishia kuwa hadi namba za hayo magari binafsi za hao makamanda anazo, je ni kwanini anashikwa na kigugumizi na hachukui hatua kwa makosa hayo ya dhahiri ya jinai?

Hivi Rais wetu anajisikiaje anapoona maelfu ya wahalifu wengine wa makosa madogo madogo, kama vile wezi wa kuku, wakitupwa magerezani kila uchao, kwenye Mahakama zetu hapa nchini, wakati hao makamanda wa Polisi akiwaachia watembee huru uraiani?

Huu ubaguzi wa wazi kabisa wa kuwafanya baadhi ya wananchi kuwa na "impunity" na kutoweza kushitakiwa na wengine wawe wanaozea jela kwa makosa madogo madogo, siyo "fair" kabisa
Yeye anaendelea tu alipoishia mwendazake pale alipoamua kutimua wenye vyeti feki na kuwaacha hao wezi wa wese wakitamba na vyeti feki.
 
Mkuu suluhu sio katiba mpya....nadhani dawa ya kudumu ni uwajibikaji wa viongozi wetu,kila MTU kwa nafasi yake. Unaweza ukawa na katiba mpya lakini watu ni wale wale akina Mwigulu.
Atawajibikaje wakati anajua Jaji au hakimy hana ubavu wa kumfunga wala Takukuru haina meno?
 
Back
Top Bottom