Hii ya wake wa viongozi wastaafu kuanza kulipwa ni zaidi ya too much

Chakaza

JF-Expert Member
Joined
Mar 10, 2007
Posts
40,455
Reaction score
73,145
Mbona kama vile nchi hii ina Ufa mkubwa sana wa kujali raia wake?

Yaani mwanajeshi mstaafu kapigana vita Uganda na kaponea chupuchupu mara kadhaa vitani, daktari aliyestaafu miaka ya 1990 na Mungu amempa maisha mpaka leo au Mwalimu aliyekuwa anatumika kwa moyo wote miaka hiyo bahati mbaya kwa serikali HAJAFA hadi leo anapokea kutoka HAZINA shs laki moja kama pension kila mwezi lakini eti wake wa viongozi nao wawe wanalipwa mamilioni 25% ya mishahara waliyokuwa wanalipwa waume zao?

Basi nchi hii ni tajiri sana! Lakini kwa nini haiwakumbuki basi hata hawa wazee waliolitumikia taifa kwa moyo mmoja enzi hizo.

Kumbukeni nazungumzia wastaafu walio staafu zamani 1998 kwenda nyuma kabla ya mifuko ya jamii haijaanza na wanalipwa na Hazina.
Kwanza sidhani kama wastaafu hawa wanazidi 5000 nchi nzima maana wengi wametangulia mbele ya haki waliobaki ni mateso tuu.

Mara ya mwisho kiwango hiki kupanda na kuwa laki moja ni miaka 10 iliyopita wakati wa JK. Waoneeni huruma acheni uchoyo.

 
Mtumishi wa nchi hii wewe tumika na utapambwa sana wakati unavuja jasho lkn ukisha kabidhi ofisi basi unasahaulika.

Ndiyo maana watumishi wengi sana wamekosa uzalendo na akipata nafasi ya kuiba basi anafanya kweli bil hata huruma.

Wewe ushaambiwa kuwa mtumishi kula kwa urefu wa kamba yako alafu unajfanya mzalendo ?
 
Huyu ni very selfish mom
 
Hao wake wenza kazi Yao haswa ni nini mpaka wapewe pensheni? Kutandaza miguu au kutoa gymnastic style?
Sheria hiyo isiwabague na wake/ waume wote wenye wenza walio kazini na jobless spouses wao nyumbani.
Bunge halikutumwa kwenda kutunga sheria za kibaguzi au Kwa ajili ya manufaa ya VIP pekee…
 
Tangu lini bunge hili la chama kimoja liliwahi kutunga au kupitisha sheria zenye manufaa kwa watanzania wote?
 
Ifike mahali hawa akina kikwete and the like watosheke, huyu mama hana mshipa wa aibu
 
Salma fedha mliyoiba escrow, kwenye vitalu vya gas na mafuta haiwatoshi? Hamshibi?
 
Huo ujumbe uwafikie walimu wanaoisaidia CCM kuiba kura
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…