Hii ya wanafunzi wa Rwanda ni fitina au vilaza

Mkuu, hao wanyarwanda wapo sahihi kabisa. Kwanini!. Tanzania ni moja ya nchi (inaweza kushika namba moja) ambayo rate ya kufeli wanafunzi wa vyuo vikuu ni kubwa sana. Nimeenda Ulaya nimeenda Marekani nimeenda Asia. Kwangu mimi sijaona wanafunzi wakifeli namna hii. Halafu cha ajabu ni kuwa ma-graduate wa vyuo vikuu vya Tanzania sio bora kama wanaohitimu Ulaya nk. Kunani? Bado elimu yetu imejikita kwenye kukariri kukariri kukariri na kukariri. Ndio maana wengi wa wanafunzi wa vyuo hawaishi kuingia na nyenzo kwenye mitihani!
 

Ujumbe umefika mkuu, ingawa wao wanadai ni vipanga
 

na hicho walichokuwa wanakiongea kwamba wao hawawezi kukremisha ila wanaelewa zaidi, ila kukrem na kuelewa kuna uhusiano mkubwa sn.
 
Ni wazi wanaweza dhani siasa zina mkono wake kutokana na hali ilivyo sasa, lakini kiuhalisia kuna mengi yanatakiwa yaangaliwe katika kufail kwao!
Wengi wameelezea utofauti wa lugha, hilo ni moja! Lingine ni system zinazotofautiana za elimu inaweza kuwa kikwazo. Tanzania tuna Advanced Sec. School baada ya O'level. Vipi kuhusu wao?? Hili linatofauti kubwa sana. Nina mfano mzuri wa vijana toka Msumbiji na DRC (wao hawana A'level). Light courses ambazo ni introductory wao wanasema kabisa zipo "above their level"!!!!
Katika lugha kuna ndugu zako Wacongo, wao wanaona bora Kiswahili kitumike kuliko English...It's funny na nashaka kama watakuwapo this AY
 
Elimu ya Udsm ngumu sana dah. Walimu wanacomplicate sana maisha.
 




Please tuache ku-associate vitukio vinavyoweza kuleta uchochezi. Sisi wabongo tunaweza kuwavumilia wenzetu, taarifa hii isije ikapokelewa na RWANDA tofauti wakaamua kulipiza visasi ovyo! Tuwe makini na posts zetu.
 
Elimu ya Udsm ngumu sana dah. Walimu wanacomplicate sana maisha.

acha uchochezi wewe. kwani umeambiwa hao wanafunzi wamesoma UDSM au Tanzania? mleta mada amesema nje ya nchi ingawa hajabainisha ni nchi gani wala chuo wanachosoma
 
hivi inakuwaje mnadisco wengine enzi zetu ata tusipofanya mtihan tunafauru
 
acha uchochezi wewe. kwani umeambiwa hao wanafunzi wamesoma UDSM au Tanzania? mleta mada amesema nje ya nchi ingawa hajabainisha ni nchi gani wala chuo wanachosoma


Ndio wanafunzi hao ni wanyarwanda ambao wanasoma pale UDSM, kila mwaka Rwanda inaleta wanafunzi wao Tanzania kama vile Tanzania inavyopeleka wanafunzi wake pale Uganda Makerere.
 

System ya elimu ni kama ya kwetu tu sema wanatumia majina tofauti, o level wanaiita junior sekondari school na a level wanaiita senior sekondari school. Kikubwa ni lugha maana ni miaka ya karibuni nafikiri kuanzia mwaka 2009 wameanza kujifunza kwa kingereza kuanzia sekondari school. Ila kama unavyojua jinsi tunavyojifunza mfano watanzania tunafundishwa kwa kingereza lakini tukiwa kwenye discussion tunaongea lugha ya kiswahili na kwao ni hivyo hivyo wanjifunza kwa kingereza wakiwa kwenye discussion zao wanadiscuss kwa kinyarwanda au kifaransa.
 
Wakuu labda na mim nitoe mchango wangu hapo juu.binafsi mim ni mmoja wa watu ambao tupo nao course moja hao warwanda...ao warwanda wanaolalamika kudsco weng wao hawajitumi na wanajitenga.yani mkipangwa kweny group moja la practical ni mzigo kwa kweli.wengi wao nadirik kusema uwezo wao ni mdogo na course wanazotaka kusoma wao kiuhalisia ni ngumu.
Kwa mfano ukienda pale coet utawakuta,wengi wao wapo civil engineering na hyo ndo course inayoongoza kwa wanafunzi kufeli...na hilo swala la kufeli sio wao tu hata sisi wazawa tunafeli vile vile..
Kiufupi ni kwmba wengi wao hawajitumi labda na lugha pia kwa mbali inachangia....
 
That is just natural akili hainunuliwi. unajua hao vijana si ajabu walikuwa na uwezo mdogo KAMA KAWAIDA YA VIONGOZI WA AFRIKA KUPENNDELEA WATOTO WAO. NAKUMBUKA KUNA MWAKA PROF. SARUNGI ALIWAHI KUKIRI KUWA ALIMPELEKA MTOTO WAKE ALIYEPATA DIV. IV F6 ULAYA MASHARIKI KUSOMEA UDAKATARI. MFANO HUU UNAWEZA KUWEPO HATA HUKO RWANDA, WATAWALA WAKAWAPELEKA WATOTO WAO BADALA YA WATOTO AMBAO NI VICHWA KTOKA FAMILIA MASKINI. HAYA YANATOKEA SANA AFRICA. KWAHIYO HIYO NI HAKI YAO KUFELI HASWABEBEKI
 
Mkuu mnafeli kwa vile hamfikii viwango kwenda Ulaya na Marekani si hoja hata sisi tumepita huko.

Ulaya na Marekani ukienda vyuo vya ovyo ovyo utapasi tu lakini unarudi mbumbumbu.

Viwango vilivyoachwa na wajerumani wakati huo FoE sasa CoeT ni vya elimu ya uhandisi vya kimataifa.

Disco zilikuwepo, zipo na zitendelea kuwepo mwanafunzi asipofikia viwango.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…