Hiki kinywaji kimeniponza

ween

JF-Expert Member
Joined
Jul 20, 2016
Posts
414
Reaction score
129
Wakuu, kwa mara ya kwaza leo Nimekunywa kinywaji cha baridi Azma energy, Kwakweli Nimependa radha yake na nimeinjoy.... Cha ajabu baada ya kama Dk 20 hiv hari yangu imebadirika miguu haina nguvu hari kadhalika moyo hauko poa nahic kero mpaka hpo sijaelewa nifanye nn? Ushauri plz
 
Wewe hata kahawa nyingi haikufai
 
Hicho kitakuwa namba 2ya kile kilichoua wale pale kimara
 
Isome chupa ya hicho kinywaji sehemu yenye maandishi mekundu ndo utaelewa angalia ucjelala jumla mkuu!
 
Hizo unakunywa ukitoka kufanya mazoezi...

Ukinywa alafu ukae tu, zinakulaza...

Cc: mahondaw
 
Mkuu kama una matatizo ya moyo au shinikizo la damu hulusiwi kabisa kutumia vinywaji vyenye caffein nyng kama energy drink..

Umekosa nguvu kwasababu hiyo caffein imeshusha blood pressure kwenye mwili wako na reaction yake ndo unakuta unaishiwa nguvu na kujisikia mchovu sana..
So dont dont try that again
 
mkuu energy drink sio nzuri hasa ile ya azam kwa watu wenye pressure ndogo. mimi jana nilichelewa kuamka pia nikawa na safari ya mjini. nikaona haia haja ya kunywa chai maana joto kali, nikanunua energy ya azam nikanywa fasta fasta ili nirefresh mwili. weeee kufika maeneo ya tazara nikaanza kukosa nguvu kwenye siti ya gari niliyokaa. hapo hapo mapigo ya moyo yakawa chini sana na jasho linanitoka usipime. nikavumilia kidogo mpaka kufika kariakoo hali ikawa nzuri nikaenda mgahawani nikala ila bado sikula sana kutokana na reaction ya ile energy drink. kwa ushauri wangu bora mtu unywe ukiwa umeshafanya kazi angalau nzito kidogo
 
kula like mkuu maelezo yako mazuri sana
 
We hujala.alafu unaenda kupalamia vinywaji hovyo hovyo unategemea nin?
 





MUHIMU KWA MUSTAKABALI WA AFYA YAKO SOMA !!!

Azam company ni kampuni inayolisha Watanzania na nchi nyingi kusini mwa jangwa la Sahara. Mzee wetu huyu amekuwa msaada mkubwa kwa Watanzania na nchi jirani zinazotuzunguka kupitia huduma mbali mbali anazotoa kuanzia usafiri wa majini, vyakula hata vinywaji. Sitasita kumpongeza mzee wetu kwa huduma zako na Mungu atakulipa kwa hili.

Kilichonifanya nikujadili hapa mzee ni hiki kinywaji chako kipya , Watanzania wamekipokea na wanakitumia sana kifupi kinauzika huu ndio ukweli . Na mimi kama miongoni mwa wateja wake nikajaribu kukionja kutaka kujua kina ladha gani kinywaji hiki ?? Kinywaji hiki kinaitwa .Baada ya kufungua na kuonja kwa mara ya

kwanza kilinishinda kurudia fundo la pili nikajua labda huenda ni gesi ngoja nikiache kwa muda kidogo, lakini hata baada ya kukirudia tena bado kilinishinda.

Nikajikuta navutiwa kusoma kimeungwa kwa kutumia viungio gani(ingredients) hiki nilichokiona ndicho

kilichonifanya niandike haya , malengo sio kuharibu biashara yako la ni kuwajuza Watanzania ambao wengi wetu lugha iliyotumika hapa ni changamoto kuijua , lakini pia wengi wetu huwa hatuna utamaduni wa kusoma hivi vibandiko kabla ya kutumia .NI NINI NILICHOKIONA NA KIKANISTUA?? HIKI HAPA !!

1.INGREDIENTS(VIUNGIO)

Water sugar, Carbondioxide,Citric acid,(E330), Taurine, Acidity Regulator Sodiumcitrates E331,Colour plain , Caramel E150a, Inositol,Preservative Potassium Sorbate E 202,Flavouring,Niacin,Pantothenic Acid, Vitamin B6, B12

Baada ya kuandikwa hivi viungia ukiangalia katika chupa hii kilichofatiwa ni muda wa matumizi na mahali kinapozalishwa. Lakini bado sikupata mantiki kwanini kimekuwa kikali mno kwanini!!!!
GHAFRA katika kudadisi zaidi ndipo chini ya maandishi hayo nikakuta maandishi mengine mapya tena yamewekwa juu ya wino#MWEKUNDU# kuashiria TAHADHALI bila kuandikwa neno lenyewe la TAHADHALI

Maandishi haya yameandikwa katika lugha ya KINGEREZA yanasomeka hivi:

"High caffeine content(31.5mg/m100)Taurine(0.03%).Do not Drink More than 2battles per Day, Not suitable for persons Sensitive to Caffeine, Children, Pregnant, Breast feeding women and Avoiding Drinking before sleeping"
TAFSIRI; HAYA KWA!! WASIOJUWA

Ina kiasi kikubwa cha CAFFEINE, Usinywe zaidi ya chupa 2 kwa siku, Haifai kwa watu wenye matatizo na

CAFFEINE, haifai kwa watoto, wajawazito, wana mama wanaonyonyesha na mwisho Usitumie muda mfupi kabla ya kwenda kulala kinywaji hiki.

Kwanini usinywe muda mfupi kabla ujakwenda kulala ?
Kiwango cha 31.5mg/ml100 za caffeine ni nyingi kwa matumizi ya kawaida hivyo kuna hatari ya blood pressure kushuka na ukiwa usingizini na hatimaye ukapoteza maisha hivyo ni hatari kunywa wakati unakwenda kulala, inaathiri ubongo pia. kwa watoto na hata watu wazima. kwa wajawazito, kwa wanaonyonyesha

Sasa Mzee wangu Bakhressa ni watanzania wangapi wanatumia kinywaji hiki pasipo kujua? kuna wajawazito watoto, wazee wote wanakibugia tu hawajui kinachoendelea katika kinywaji hiki mzee.

Hakuna kinywaji ambacho ni CARBONATED kisichokuwa na CAFFEINE hii inajulikana lakini mzee HIKI

KIWANGOCHA (31.5mg/100m) ULICHOWEKA HUMU NI KIKUBWA MNO Sina hakika lakini inawezekana

KIKAPITA hata kiwango cha kwenye HEINKEN . CAFFEINE DRINK Kuna baadhi ya nchi kama UFARANSA,

MAREKANI, HISPANIA, UINGEREZA WAMEPIGA MARUFUKU
Kutokana na athari zake hasa KATIKA UBONGO.

Hakuna shaka Mzee baada ya muda mfupi wa matumizi ya kinywaji hiki WATANZANIA WENGI HASA kina mama na watoto na hata wanaume watapata matatizo haya , MFUMO WA UBONGO kuathirika hili halina shaka ,

VIDONDA vya tumbo, kwa wana mama wajawazito wanaobugia pia watazaa watoto wenye matatizo hasa AKILI kutokana na Ubongo kuathiliwa, wanaonyonyesha pia, MZEE kama ujumbe huu utakufikia naomba TUONDOLEE

JANGA ILI Maana haya matatizo tuliyonayo YANATUSHINDA .

Watanzania wengi wataumia SIKU CHACHE ZIJAZO na hazipo mbali.

[HASHTAG]#Caffeine[/HASHTAG] ni nini?

Caffeine
Drug

Caffeine is a central nervous system stimulant of the methylxanthine class of psychoactive drugs. It is the world's most widely consumed psychoactive drug, but unlike many other psychoactive substances,
 
Asante mzizi mkav
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…