harder king
JF-Expert Member
- Jan 21, 2017
- 3,970
- 6,907
Mkuu kama alikuomba kwa ajili ya kupikia Sawa ila kama ukupewa sababu ya kuombwa unga na wewe ukatoa bila kumuliza anakoupeleka mm sijaona kosa maana ata mm natumiaga kung'arisha viatu na vinang'aa vizuri tu.Issue sio unga ishu ni chakula. Hata kama ingekuwa punje moja ya haragwe
Push to Start
Ila baada ya kugundua kwamba unga uliompa aliutumia kwa kusafishia viatu muda huo huo kama ungemwambia huyo jirani yako kwa upole tu kwamba hukujua kama unga alioomba ulikuwa ni wa kusafishia viatu na ukamsikia jibu lake usingeteseka kiasi hiki. Maana kwa jinsi unavyoonekana baada ya kuamua kuanzisha uzi huu hapa leo utateseka sana siku nzima kwa sababu utalazimika kuwa unauchungulia kila mara kuona wadau wanasemaje kuhusu hii hoja yako. Sasa hayo si mateso jamani wakati ungeweza kuyaepuka kwa kutumia hiyo njia mbadala na pia kwa kuzingatia kwamba ulikuwa umetoka kanisani?Nimeumia sana mkuu
Push to Start
Vizuri boss. Mm nimepanga
Sasa mkuu unga kibakuli unakuuma namna hyo kweli hii ngoma nzito[emoji16][emoji16][emoji16]
Sent using Jamii Forums mobile app
Jamaa angekuwa wa ajabu kama angedanganya matumizi ya huo unga. Lakini hawakuwa na makubaliano yoyote ya matumizi.Mkuu kama alikuomba kwa ajili ya kupikia Sawa ila kama ukupewa sababu ya kuombwa unga na wewe ukatoa bila kumuliza anakoupeleka mm sijaona kosa maana ata mm natumiaga kung'arisha viatu na vinang'aa vizuri tu.
Sent using Jamii Forums mobile app
Aisee,we ni mwandishi mzuri sana,pole lakin
Ukimaliza kufua viatu kabla ya kuvianika unapaka unga kwa juu, ndipo unaanika, hii inasaidia kuzuia viatu kuwa na ramani au kufubaa vikikauka,,Huo unga unasafishaje viatu? Sijawahi kuona au kusikia hii kitu.
Mkuu una uvumilivu wa kiwango cha Lissu mi ningemzingua
Na hii haijalishi kama rangi ya viatu ni kahawia, nyeusi, blue n.k. utatumia tu huo unga ambao wenyewe kwa rangi ni mweupe?Ukimaliza kufua viatu kabla ya kuvianika unapaka unga kwa juu, ndipo unaanika, hii inasaidia kuzuia viatu kuwa na ramani au kufubaa vikikauka,,
Habari za Jpili wana Jukwaa
Nimerudi nyumbani after church nikawa nafanya mambo wawili matatu kwa ajili ya mchana huu.
Mara jirani akagonga mlango, nikafungua.
Tukasalimiana vizuri. Alikuwa na kibakuli mkononi. Akaniomba kama nina Unga ugali nimsaidie kidogo kwenye bakuli lakke nikamjibu ninao. Akauliza ni Dona au sembe?
Nikamjibu ni Sembe. Akasema ndo mzuri. Basi nikamchotea nikampa. Baada ya muda nikaona ule unga wangu anautumia kufulia viatu vyake.
Mimi nilijua labda kakwama unga wakati anapika ugani kumbe ni unga wa Kung’arishia viatu??
Nimeumia japo ni jambo dogo. Maisha haya ni magumu sana. Tuwe na Discpline na vyakula.
Jpili njema
Push to Start