Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 33,771
- 41,027
SICHO HICHO
Hiki kilichoko sicho, hiki sicho kilichoko,
Ndicho hiki hichohicho, ndicho hiki hakiko,
Hiki ni kile si hicho, kile kisichokuwako
Hakuna cha mgao, kilichoko ni historia;
Ya mgao!
Aliyesema hakiko, kwamba hakitakuwapo,
Yeye mwenyewe hayuko, alichosema hakipo,
Huyu bwana yuko yuko, kama popo mwenye pepo,
Hakuna cha mgao, kilichoko ni historia;
Ya mgao!
Wanachogawa hakipo, kwani kisingekuwepo,
Ugawe vipi hakipo, hakipo huko mlipo,
Kama wafuata upepo, ndugu zangu mpo mpo,
Hakuna cha mgao, kilichoko ni historia;
Ya Mgao!
Cha nini hki cha nani, kwanini tena ni nini?
Tutamuuliza nani, kinaendelea nini?
Tunakuwa kama nyani, kujenga nyumba mtini!
Hakuna cha mgao, kilichoko ni historia;
Ya Mgao!
Tukubalini watani, janja ya jiwe ya nini?
Hili jambo siyo geni, linarudia kwa nini?
Ahadi zao jamani, twaamini kama dini!
Hakuna cha mgao, kilichoko ni historia;
Ya Mgao!
Na. M. M. Mwanakijiji (Sauti ya Kijiji)
Hiki kilichoko sicho, hiki sicho kilichoko,
Ndicho hiki hichohicho, ndicho hiki hakiko,
Hiki ni kile si hicho, kile kisichokuwako
Hakuna cha mgao, kilichoko ni historia;
Ya mgao!
Aliyesema hakiko, kwamba hakitakuwapo,
Yeye mwenyewe hayuko, alichosema hakipo,
Huyu bwana yuko yuko, kama popo mwenye pepo,
Hakuna cha mgao, kilichoko ni historia;
Ya mgao!
Wanachogawa hakipo, kwani kisingekuwepo,
Ugawe vipi hakipo, hakipo huko mlipo,
Kama wafuata upepo, ndugu zangu mpo mpo,
Hakuna cha mgao, kilichoko ni historia;
Ya Mgao!
Cha nini hki cha nani, kwanini tena ni nini?
Tutamuuliza nani, kinaendelea nini?
Tunakuwa kama nyani, kujenga nyumba mtini!
Hakuna cha mgao, kilichoko ni historia;
Ya Mgao!
Tukubalini watani, janja ya jiwe ya nini?
Hili jambo siyo geni, linarudia kwa nini?
Ahadi zao jamani, twaamini kama dini!
Hakuna cha mgao, kilichoko ni historia;
Ya Mgao!
Na. M. M. Mwanakijiji (Sauti ya Kijiji)