Hili chapuo analopigiwa Lugumi ili kumsafisha linatia shaka. Mamlaka zisichukulie kama jambo la kawaida!

Hili chapuo analopigiwa Lugumi ili kumsafisha linatia shaka. Mamlaka zisichukulie kama jambo la kawaida!

Cute Wife

JF-Expert Member
Joined
Nov 17, 2023
Posts
1,906
Reaction score
5,000
Wakuu,

Kama mmeona sasa hivi karibu kila siku Lugumi yuko kwenye media, mara katoa msaada kwa watoto yatima, mara anajengea yatima nyumba, mara kaalika watoto wanaoishi kwenye mazingira magumu kufanya dua, mara sijui kaenda kulisha wapi, yaani ni heka heka mtindo mmoja.

Na Millard kama kawa kwenye ishu hizi hakosi. Siyo siri kuwa anatumika na watu mbalimbali mashuhuri kuwasafisha kutokana na uozo wanaofanya kwa maslahi binafsi.

Mitume na manabii wenye rekodi za ajabu wanamtumia Millard awasafishe, wanasiasa wapuuzi wakitaka mambo yao yapaishwe kuonekana wema na wanawatumikia watanzania kama mama Teresa Millard ndio kimbilio lao, GSM (Home Shopping Center) wamemtumia vizuri kuwanfanya raia wawaone wema wakati ni wachafu zaidi ya uchafu wenyewe (kupata picha ya ufirauni wa kina GSM soma hapa - .

Millard kafuta habari zote za ufisadi kuhusu Lugumi unafikiri amefanya hivyo bila kuachiwa mzigo? Kwa hili chapuo anafanya kuhakikisha yupo machoni petu kila wakati atakuwa kamegewa mzigo mchafu wa kutosha.

Ninavyofahamu Lugumi ako na skendo za ufisadi wa kutosha, na nasikia ni mafia kwelikweli.

Hili chapuo si bahati mbaya, limekuja ghafla na kwa kasi ya ajabu, inadaiwa anaenda kuingizwa Jeshini (kama bado halijafanyika tayari) na hii ni hatari kwa usalama wa nchi.

Tunaenda kupigwa na kitu kizito jamani, amkeni tukatae mafisadi, hili bomu linalokuja tutabaki mdomo wazi!

Ni kwanini haya yanatokea chini ya Utawala wa Rais Samia?
 
Lugumi enterprises Limited katika shughuli ya kukagua ubora wa bidhaa

1735299939685.jpeg

1735299970892.jpeg

1735300029714.jpeg
 
Tumeona wachafu wote walirudishwa vitini na kisha wakaota mapembe, akaanza kuwatoa.

Sio huyo tu, Jisiemu, Mangji, Seedti, Kinamna, Roastharm...mara Abdibull naye katokezea etc.
  • Maali za mma zikaanza kwenda
  • Pesa za wageni zikapotea
  • Mpaka Laisy akawa anatunza pesa za wageni kama wafanyavyo akina papaa.
  • Mitandoni Mashuka ya mmasai yakaanza kutapanywa
  • Gambling imekuwa ni mchezo wa kutangazwa kwa nguvu na Chawaz wanaomtaja mzazi!

Boom, Lungumi naye huyo...Biometric vituo vya raia hamna, pesa katia kibindoni, leo ni mtu huru tu uraiani!

Ndoto ilipozidi kuwa ya kutisha, nikashtuka....
 
Jamii bado anapiga deal mkuu. Kuna jamaa aliingia kwenye cycle yake kipindi cha magu yani jamaa now ana ela hata punda habebi.

Sijui walikuwa wana tenda ya kusupply silaha nadhani bunduki ndivyo nilivyosikia ila siko sure kama ni kwa jeshi la polisi wa Tanzania au kwingine au zilikuwa sound. Ila jamaa wanapiga pesa ndefu sna.
 
Mheshimiwa alijaribu kumtikisa akakuta ni mti wa zege, akaachana naye... Na ile kesi yake ya mashine za Finger Print kwa vituo vya polisi nchi nzima iliishayeyuka...

Kangi alimpiga mkwara Mbuzi akapotea yeye...

Eti tajiri ajenge tu jengo la ghorofa nane kwa ajili ya watoto yatima? Miaka ijayo tutakuja kujua kunani kuhusu hawa watoto 800 na hilo jengo.. :ALIENALIENALIENALIENALIEN: Tusisahau ya Cambiaso na Football Academy.
 
Tumeona wachafu wote walirudishwa vitini na kisha wakaota mapembe, akaanza kuwatoa.

Sio huyo tu, Jisiemu, Mangji, Seedti, Kinamna, Roastharm...mara Abdibull naye katokezea etc.
  • Maali za mma zikaanza kwenda
  • Pesa za wageni zikapotea
  • Mpaka Laisy akawa anatunza pesa za wageni kama wafanyavyo akina papaa.
  • Mitandoni Mashuka ya mmasai yakaanza kutapanywa
  • Gambling imekuwa ni mchezo wa kutangazwa kwa nguvu na Chawaz wanaomtaja mzazi!

Boom, Lungumi naye huyo...Biometric vituo vya raia hamna, pesa katia kibindoni, leo ni mtu huru tu uraiani!

Ndoto ilipozidi kuwa ya kutisha, nikashtuka....
Ndoto kama ndoto, ni huzuni
 
Mheshimiwa alijaribu kumtikisa akakuta ni mti wa zege, akaachana naye... Na ile kesi yake ya mashine za Finger Print kwa vituo vya polisi nchi nzima iliishayeyuka...

Kangi alimpiga mkwara Mbuzi akapotea yeye...

Eti tajiri ajenge tu jengo la ghorofa nane kwa ajili ya watoto yatima? Miaka ijayo tutakuja kujua kunani kuhusu hawa watoto 800 na hilo jengo.. :ALIENALIENALIENALIENALIEN: Tusisahau ya Cambiaso na Football Academy.
Au na wenyewe wanasetiwa kutumika kwenye dili zake chafu?!
 
Lugumi ni mchafu sana ni fisadi alitajirika kutokana na ufisadi uliofanyika na watz walivyo wajinga leo hii wanamuona wa maana japo analofanya ni la maana lakn haiondoi ukwel ni mchafu na usikute hata anaosha hela tu kupitia hio misaada
 
Back
Top Bottom