Hili jukwaa limepunguza sana mvuto tofauti na kipindi cha nyuma nini tatizo?

Hili jukwaa limepunguza sana mvuto tofauti na kipindi cha nyuma nini tatizo?

Kipindi cha nyuma kulikuwaga na mijadala migumu sana humu,
Kulikuwa na hamasa sana, watu nakumbuka walikuwa hadi wanakutana kwa Chai day na wana discus Biashara hasa kilimo,

Idea ya Jamii Saccos ilianzishwa na wadau wa humu na Saccos ikaanzishwa,Wadau humu nakumbuka wakina Chasa, Liverpool, Madinimadini na wengineo wali fanya hadi mkutano mkubwa pale Rombo green view hotel.

Kulikuwa na wadau kama Malila, sijui wako wapi siku hizi wanachungulia tu na kusepa.

Jukwaa limevamiwa na watoto, limevamiwa na watu ambao humu ni sehemu ya kujipumzisha, humu huja kana kwamba wamepotea njia.

Jukwaa halina kash kash kama za enzi zile ambapo kulijjwa na mijadala migumu sana na pia watu walikuwa wanakutana kufanya mikutano na pia watu walilima pamoja,

Ile nguvu sidhanii kama itarudigi make now day wengi wanao ingia humu kuchangia na kupost utaona kabisa uwezo wao ni mdogo sana na wengi wanakuja kupumzika tu,

Nawakumbuka sana watu kama Malila, ELININO na wengineo Watu kama Liverpol watu kama chasa

Humu lazima watu wabadilike watu wawe kweli na nia.

Mkuu kuna wakati wa kujadili mada then wale walio BOLD huwa wanamove forward na kufanya action, labda nikuulize wewe ulitaka watu wawe wanajadili stori tu kila siku? Labda nikujulishe tu: Huyo Chasha Poultry Farm unayemtaja next month tutakuwa naye kwenye safari to Nairobi kucheki maonyesho ya kilimo; Mkuu Malila unayemtaja mimi binafsi ninashiriki naye pamoja na wadau wengine kwenye miradi mikubwa zaidi ya mitatu ambayo ilijadiliwa humu humu toka mwaka 2010; Mkuu ONTARIO ana project inarun sasaivi na watu wanapiga shule; Mkuu Zainab Tamim saccos yetu inarun sasaivi na watu tushaanza kununua hisa. SASA LABDA NIKUULIZE KWA HERUFI KUBWA; UNATAKA WATU WAWE WANAJADILI TU KWA MANENO? TAKE ACTION.

NB: Wakuu nilowataja hapo juu mniwie radhi nimeshindwa kujizuia kuwataja coz you guys can break mountains with your courage.....salute to you all.
 
Hili jukwaa limenifunza mengi yahusio ujasiri Mali.
Ukweli zamani jukaaa lilikuwa bora zaidi.
Lakini nashukuru bado Chasha Poultry Farm tuko nae bila kumsahau The Consult hao wengine wamekuwa wakichungulia.
 
Mkuu kuna wakati wa kujadili mada then wale walio BOLD huwa wanamove forward na kufanya action, labda nikuulize wewe ulitaka watu wawe wanajadili stori tu kila siku? Labda nikujulishe tu: Huyo Chasha Poultry Farm unayemtaja next month tutakuwa naye kwenye safari to Nairobi kucheki maonyesho ya kilimo; Mkuu Malila unayemtaja mimi binafsi ninashiriki naye pamoja na wadau wengine kwenye miradi mikubwa zaidi ya mitatu ambayo ilijadiliwa humu humu toka mwaka 2010; Mkuu ONTARIO ana project inarun sasaivi na watu wanapiga shule; Mkuu Zainab Tamim saccos yetu inarun sasaivi na watu tushaanza kununua hisa. SASA LABDA NIKUULIZE KWA HERUFI KUBWA; UNATAKA WATU WAWE WANAJADILI TU KWA MANENO? TAKE ACTION.

NB: Wakuu nilowataja hapo juu mniwie radhi nimeshindwa kujizuia kuwataja coz you guys can break mountains with your courage.....salute to you all.
Asante kwa kututaja, tumefurahi sana na kuona kumbe tumo.

Sasa hivi tuna mradi mpya na mzuri sana kwa ataependa kujiunga nasi. Usomeni hapa: Sasa tumewaletea uwekezaji mpya unaolipa kihalali
 
Hamasa Haziendani na Hali halisi ya Biashara.. Kuna Watu wanazungumza like if Hela ni rahisi sana kuipata... But in reality una Haso sanaa
 
Mnashangaza mno mnaolazimisha mambo ya zamani kuwa ya leo. Zamani kulikuwa na Leyland bus, leo kuna Zhengzhou Yutong bus. Hata hivyo hizo mada za kilimo mbona zipo?

Kuna thread inaendelea kuhusu Kuporomoka kwa zao la Mbaazi. Ndo maana kuna member akasema hakuna aliyekatazwa kuleta mada hizo. Acheni lawama haisadii kitu
Uko sahihi. Pia ikumbukwe,biashara nyingi ziko taabani ukianza na ya mazao. Kwa hali hiyo,hata mawazo nayo yanakuwa down.
 
Back
Top Bottom